Follow us

KANUNI ZAKUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU

Tangazo

KANUNI ZAKUFANYA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE NA MUNGU

1 Muombajisharti usiwe mwenye dhambi.

    YOHANA 9:31

"Tunajua kwamba Mungu HAWASIKILIZI watu wenye Dhambi, ila humsikiliza yeyote mwenye kumcha na kutimiza mapenzi yake" ( Tafsiri ya Habari Njema )

👉 Umeona kwamba Neno la Mungu limeweka wazi kabisa kwamba unapokuwa mwenye dhambi Mungu hatakusikiliza kabisa wakati unamuomba. Kwahiyo ili Mungu ajibu maombi yako ni lazima uishi maisha ya Utakatifu, achana na kufanya dhambi kwa siri/kujificha.

 

2 Muombajisharti ukae ndani ya kristo Yesu.

    YOHANA 15:7

"NinyiMKIKAA Ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, Ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa"

👉 Mungu hawezi kuyajibu maombi yako kama wewe hujakaa ndani ya Yesu Kristo. Ninaposema kukaa ndani ya Yesu Kristo maana yake nilazima Uokoke sawa.

 

3 Muombajisharti Uombe kwa Bidii sana.

   YAKOBO 5:17

"Eliya alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja na sisi, AKAOMBA kwa BIDII mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya nchi muda wa miaka mitatu na miezi sita"

Eliya aliomba kwa bidii sana kuhusu mvua kutonyesha na Mungu akajibu hayo maombi yake.

   MATENDO 12:5

"Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa LIKAMWOMBA Mungu kwa JUHUDI/BIDII kwa ajili yake"

Hapa tunaliona kanisa likimuombea kwa bidii Petro wakati alipokamwatwa na mfalme Herode na kutokana na kanisa kuomba kwa bidii Mungu alisikia maombi yao akawajibu na kumtoa Perto ndani ya gereza.

Kuomba kwa bidii maana yake ni kuomba bila kukata tamaa aidha kwa kukatishwa na wanadamu au mazingira.

Huwa ili Mungu ajibu maombi yako  ni lazima aione bidii yako wakati unaomba, lakini ukiomba kwa ulegevu hawezi kukujibu.


MAHITAJI AU UNAHITA MAOMBEZI TUMA HAPA

MCHUNGAJI LAURENT MPOMA

NCHI YA UKOMBOZI MINISTRY

(HEMA LA MAOMBI NA MAOMBEZI)

MWAJA KITOPE - SINGIDA MJINI

0714890889

WHATSAP: 0762756542

 

 

 

Post a Comment

0 Comments