JINSI NGUVU ZA GIZA ZINAVYOINGIA
NDANI YA MTU AU KUITESA FAMILIA BILA MTU KUJUA AU FAMILIA KUJUA
MUNGU
alivyoumuumba Mwanadamu Kusudi na Lengo lake kuu lilikuwa sio tu kumpa Dunia
hii aitawale; Bali Lengo lilikuwa ni KUABUDIWA.
Shetani (Lucifer
au Joka) Aliyekuwa Mbinguni kama Malaika Mkuu wa Sifa;Alikitamani Kiti Cha Enzi
cha MUNGU BABA,akatupwa Chini yeye na Malaika(Ambao leo ndio Majini na Mapepo)
waliomuunga mkono kwenye Kampeni zake za Uasi dhidi ya MUNGU. (Ufunuo 12:7-)
Unatakiwa kujua
kitu kimoja Muhimu:
MUNGU hana
damu na Nyama,[Kama mimi na wewe] YEYE NI ROHO.(Yohana 4:24)
Mathayo 10:28 isema Msiwaogope wauao mwili
wasiweze kuiua roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho
na pia katika jehanamu.
Sasa Ibilisi Shetani na Mapepo,Majini pia
Roho.Hawafanani na MUNGU moja kwa moja ila wana sifa moja iko kama MUNGU; nao
hawana mwili wa damu na Nyama.
Kuna jambo moja la ajabu sana ambalo wanadamu
wengi hawalijui na pia Ibilisi hataki walitambue.
MUNGU katika
kitu anakiheshimu na huwa haendi kinyume nacho "NI NENO LAKE" na huwa
hageuzi.
Alipowapa
malaka wanadamu kwa kusema "WAKATAWALE" katika (Mwanzo 1:28)
alimaanisha kabisa kwa Kumpa mwanadamu Milki yote ya Dunia hii.Yaani kama vile
Yeye anavyotawala Mbinguni, ndivyo alitaka mwanadamu atawale hapa dunia kwa
asilimia 100.( Zaburi 115:16)
Kwanini
Mwanadamu alipewa Kumiliki hii dunia ?!
1.Aliundwa (Designed) au kuumbwa kutokana na
Mavumbi (Kitu ambacho roho haina)
2.Sababu nyingine ni Kumzuia Shetani asitawale
hapa dunia.Kwasababu mahali pake ni kuzimu 3.Sababu ya Tatu ilikuwa ni Mapenzi
yake yatimize hapa duniani(Kupitia Mwanadamu) kama kule Mbinguni.
Sasa katika
kitu ambacho Wanadamu wengi wamefungwa fahamu kutokukijua;Ni kwamba MUNGU
pamoja na UUNGU wake hawezi kumtawala Mwanadamu kwa Nguvu (Pamoja na kwamba
amemuumba yeye) Hawezi bila ruhusa ya Mwanadamu mwenyewe kukubali Kutawaliwa
naye.
Sababu Kuu
ya kwanza, ni Kwasababu Mungu ALIMUUMBA MWANADAMU NA UTASHI (Maamuzi ya Kufanya
au Kuamua Jambo)
Sababu ya pili.
MUNGU
anaheshimu Mamlaka sana.
Sababu ya tatu;
MUNGU ni
ROHO.
Roho haziwezi kuishi hapa duniani
kwasababu kuu mbili
1.Ili uishi
hapa duniani lazima uwe Damu na Nyama.
2. Roho
haziwezi kuishi hapa kwasababu hazitengenezwa au kuumbwa kuhimili hali ya hewa
na mazingira ya hapa duniani.
Kwahiyo ili
MUNGU atawale hapa duniani ni lazima "AVAE MWILI" (Yaani Aingie ndani
ya Mwanadamu)
Vivyo hivyo
Shetani ili atawale hapa duniani ni lazima auingie mwili wa mwanadamu ili
afanikishe malengo yake.
NJIA AMBAZO MASHETANI HUTUMIA KUMWINGIA MWANADAMU.
1.Madhabahu
na Kafara za koo.
2.Ibada za
sanamu(Kuabudu miungu na wafu)
3.Uchawi wa
kurithi au kununua
4.Kutokuwa
na Ulinzi wa Nguvu za MUNGU ndani ya Mtu.
5.Kuwaza
kupitiliza na kuruhusu Moyo ujae Uchungu.
6.Kutokumpa
YESU Maisha Ayatawale
7.Tamaa ya
Mali (Kuwa na Fedha Cheo nk)
8.Vyakula
(Vya kishetani kulishwa kwenye ndoto au kutegewa)
9.Manukato
(Pepo linaweza likakuingia kupitia harufu flani ya perfumu,Spray ambazo zina
roho za kishetani ndani yake.
Kwa mfano
kuna Perfurme unaweza kuisikia kwa mtu(Mwanaume au mwanamke) na ghafla ukaanza
kupata hisia za kingono.
(Takasa
manukato kila unapoyanunua kabla hujayatumia)
10.Mifugo
(Pepo linaweza kuingia kupitia Nyama( Kwasababu yanaweza kuishi ndani yake)
(Mathayo 8:31)
11.Yanaweza
yakaiingia Familia yako kupitia wasaidizi wa ndani.(Mdada wa Kazi au Shamba
boi)
12.Ngono
(Kukutana kimwili na mtu yeyote asiye sahihi katika maisha yako,ni moja ya njia
kuu ya mapepo,Yenye nuksi,magonjwa na mabalaa kukuingia mwanadamu.
13.Aina
fulani ya Musiki wenye maneno ya kuhamasisha Mambo ya kishetani
(Ngono,Pombe,Uvutaji wa Bangi,sigara shisha,Madawa ya kulevya nk)
Nikipata
Wakati nitakufundisha Jinsi ya Kujilinda Kupambana na haya Madudu(Madhabahu za
Kishetani na Jinsi ya kujichomoa huko na Matumizi ya Damu ya Yesu; pamoja na
Jinsi ya kuwatumia au kufanya kazi na Malaika wa Vita.(Zaburi 91:11) (Waebrania
12:22)
UBARIKIWE
SANA
MAOMBI NA
MAOMBEZI
WASILIANA NA
MCHUNGAJI LAURENT MPOMA
+255714890889
WHATSAP:
+255762756542

0 Comments