1. 1. MUNGU.
Kwa maombi yako na kukaa kwenye utakatifu na kuliishi kusudi la MUNGU na
kumtolea MUNGU zaka na sadaka kwa usahihi na upendo, MUNGU atafungua milango ya
baraka kwako. Kumb 28:8 ''BWANA ataiamuru baraka ije juu yako katika ghala
zako, na mambo yote utakayotia mkono wako; naye atakubarikia katika nchi
akupayo BWANA, Mungu wako.'' MUNGU anapoiamuru baraka fulani ije kwako hufungua
mlango wa baraka hiyo kuja kwako. Ona Mfano hapa ambapo MUNGU aliamuru baraka
ya chakula cha mbinguni ishuke kwa wana wa Israeli. Biblia inasema Zaburi
78:23-25 '' Lakini aliyaamuru mawingu juu; Akaifungua milango ya mbinguni;
Akawanyeshea mana ili wale; Akawapa nafaka ya mbinguni. Mwanadamu akala chakula
cha mashujaa; Aliwapelekea chakula cha kuwashibisha.''
2.
Wewe mwenyewe.
Kujitambua kiroho, kuomba, kuzijua haki zako
kwa MUNGU, maisha matakatifu na ya haki na kubaki katika Eneo ambalo MUNGU
amekufungulia mlango wa baraka yako.
Mwanzo 22:17-18 '' katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha
nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na
uzao wako utamiliki mlango wa adui zao; na katika uzao wako mataifa yote ya
dunia watajibarikia; kwa sababu umetii sauti yangu.'' Ibrahimu kama mwanadamu
alipomtii MUNGU alibarikiwa, kwa sababu milango ya baraka ilifunguliwa kwake.
Milango ya baraka ambayo adui walikuwa wameikalia MUNGU alisema uzao wa
Ibrahimu utaimiliki hiyo milango ambayo adui walikuwa wameichukua. Hata wewe
adui zako wanaweza kuifunga milango yako ya baraka, adui zako wanaweza
kuichukua milango yako ya baraka. Kazi yako ni kumtii MUNGU sasa na kumcha yeye
pekee, Kuishi maisha matakatifu ya Wokovu na kuomba katika KRISTO YESU ili
uimiliki tena hiyo Milango ambayo adui zako waliichukua.
2. Wazazi wako.
Wazazi wako wanaweza kukufungulia mlango wako wa baraka kwa malezi yao,
kukusomesha na kukufundisha jinsi ya kumtegemea MUNGU.
4.Watumishi wa MUNGU.
Watumishi wa MUNGU wanaweza kukufungulia mlango wako wa baraka kwa kukufundisha Neno la MUNGU na kukufunulia kanuni za MUNGU za kukufanya mlango wako wa baraka ufunguke na Kukuombea.
Mithali 18:20-21 ''Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake; Atashiba mazao ya midomo yake. Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake.''
Mungu
akubariki sana
Maombi na
maombezi
Mchungaji
Laurent Mpoma
(NCHI YA
UKOMBOZI MINISTRY TZ)
Piga 0762756542
0 Comments