Follow us

MAOMBI MAALUMU YA KUOMBEA UCHUMI MPAKA MAFANIKIO 2024

Tangazo

 

MCHUNGAJI LAURENT MPOMA
NCHI YA UKOMBOZI MINISTRY
(HEMA LA MAOMBI NA MAOMBEZI)

Tunaomba sana kuhusu uchumi kwasababu twajua kuwa Mungu anataka tubarikiwe mno lakini sasa adui amekuwa akizuia baraka zetu na hata kutusahaulisha nafasi yetu ndani ya KRISTO.

Mithali 10:22

[22]Baraka ya BWANA hutajirisha,

Wala hachanganyi huzuni nayo.

Ee Bwana Yesu, naomba Baraka zako ulizonibariki ROHONI ziwe halisi katika ulimwengu unaooneka kwa jina la Yesu.

Mithali 21:5

[5]Mawazo ya wenye bidii huuelekea utajiri tu;

Bali kila mwenye pupa huuelekea uhitaji.

Bwana Yesu, ninaomba mawazo yangu na maneno ya kinywa changu yapate kibali mbele zako. Mawazo yangu yawe ya mtu mwenye bidii, mawazo yangu yavute utajiri na heshima kwa jina la Yesu.

Kila mahali ambapo fedha na utajiri na heshima yangu imefichwa naamuru moto ufike hapo kwa jina la Yesu.

Kila tumbo lililoficha hazina ya utajiri na fedha zangu. Naamuru  lipasuke lizitapike mali zangu na Baraka za Bwana juu yangu kwa jina la Yesu

Ninakataa kuwa mhitaji kwa jina la Yesu, Bwana wewe ni mchungaji wangu, nakataa kupungukiwa na kitu.

Njoo kwenye maono, njoo kwenye ndoto, njoo kwenye mawazo. Unipe hekima kuyaelekea maji ya utulivu, nipe macho ya kuona malisho ya hatma yangu kwa jina la Yesu.

Roho Mtakatifu, naomba uutengeneze upya moyo wangu.

 Ondoa tabia ya pupa ndani yangu ili nisiangukie kwenye kundi la wahitaji na masikini. Bwana Yesu, nakusihi kwa mamlaka yako, niumbie moyo mpya wenye utulivu ndani yangu.

 Nijulishe hekima kwa siri, nifanye kuwa mtu mkuu kwa utukufu wako kwa jina la Yesu

Mithali 21:6

[6]Kupata akiba ya mali kwa ulimi wa uongo

Ni moshi upeperushwao; ni kutafuta mauti.

Bwana nakuomba unifunge kinywa nisinene kwa uongo. Naomba mauti iniepuke kwa jina la Yesu.

Mauti ya biashara, mauti ya mtaji, mauti ya kazi na kibali futika kwa jina la Yesu.

Nakuomba Bwana wangu, unirehemu na unisamehe. Mahala popote nilipotumia uongo ili kujipatia fedha na akiba unisaidie nisipatikane na madhara.

Natubu na naacha uongo . Ee Bwana uniinue na kunisimamisha kiuchumi kwa jina la Yesu.

Mithali 22:4

[4]Thawabu ya unyenyekevu ambao ni kumcha BWANA

Ni utajiri, na heshima, nayo ni uzima.

Bwana, unifanikishe kwa hekima yako na nguvu zako. Unijaze moyo wa unyenyekevu na haki yako.

Unihuishe na kukifuta kiburi cha moyo wangu kwa jina la Yesu.

 Achilia Baraka kwenye maisha yangu na uniinue kutoka katika umasikini kwa jina la Yesu.

Mithali 23:4

[4]Usijitaabishe ili kupata utajiri;

Acha kuzitegemea akili zako mwenyewe.

Bwana nimejua leo kwamba utajiri wa kweli unatoka kwako.

Ninaomba unijaze maarifa yako na nguvu zako, nakataa kujitumainia, nahamisha ufahamu na akili yangu kwako. Unishike kwa hekima yako.

Nakataa utajiri wa mateso, unibariki na kunitajirisha kwa jina la Yesu

Isaya 60:5

[5]Ndipo utakapoona na kutiwa nuru,

Na moyo wako utatetemeka na kukunjuka;

Kwa kuwa wingi wa bahari utageuzwa kukujia,

Utajiri wa mataifa utakuwasilia.

Bwana, unabii huu utimie kwenye maisha yangu haraka kwa jina la Yesu.

Utajiri wa mataifa na uje juu yangu leo kwa jina la Yesu.

Kila kilichokuwa kinazuia fedha zangu mahali naamuru kianguke kwa jina la Yesu.

Uchumi wangu,

Isaya 60:11

[11]Malango yako nayo yatakuwa wazi daima;

Hayatafungwa mchana wala usiku;

Ili watu wapate kukuletea utajiri wa mataifa,

Na wafalme wao wakiongozwa pamoja nao.

Ee Malango yangu, sikia Neno la Bwana.

Funguka na uache utajiri wangu uje. Funguka na uache heshima yangu ionekane.

Kila hazina iliyokuwa imefichwa, naipa macho, ianze kuona mlango ulio wazi kunifuata kuanzia sasa.

Hazina za fedha, hazina za uzima  na afya, hazina ya amani na furaha, hazina ya mali na utajiri.

Nakubariki wewe na familia yako, kuanzia saa hii mpaka saa tatu usiku siku ya leo kila atakayesoma hapa na kuamini maneno haya hataona njaa

Nawabariki wote  kwa jina la Yesu.

MCHUNGAJI LAURENT MPOMA

NCHI YA UKOMBOZI MINISTRY

(HEMA LA MAOMBI NA MAOMBEZI)

MWAJA KITOPE SINGIDA MJINI

+255714890889

WHATSAP: +255762756542

TUMA MAHITAJI YAKO KWA NAMBA HAPO JUU.

 

UNAWEZA KUCHANGIA SADAKA YAKO KWA AJILI YA UJENZI WA KANISA KATIKA VITU VIFUATAVYO:

1.        VITI 20 @ 20,000/=

2.        MAIKI 2= 150,000/=

3.        ENEO LA KANISA  500,000/=

4.        SIKA 2 = 1900,000/=

5.        VITAMBAA VYA MADHABAHU.= 100,000/=


TIGO PESA: +255714890889................JINA: LAURENT MPOMA

M-PESA: +255762756542.....................JINA: LAURENT MPOMA

AIRTEL MONEY: +255782859946.........JINA: LAURENT MPOMA


MCHUNGAJI ATAKUOMBEA .


MUNGU AKUBARIKI SANA WEWE UNAYECHANGIA KWA AJILI YA MUNGU NA AKUFUNGULIE MALANGO YAKO YA UCHUMI.

Post a Comment

0 Comments