MAMBO 10 YANAYOWEZA KUHARIBU UHUSIANOWETU NA MUNGU.
2. Vyombo ya habari na Mitandao yaKijamii
Internet,
Magaeti,Tv, simu n.k tunapaswa tutumie kwa kiasi. Tusipokuwa makini tutajikuta
muda wote tunautumia kwa kuchat, mtu ataanzia facebook, anaenda Instagram,
baadaye Twitter kisha Snapchat, WhatsApp, Telegram, IMO, Wechat, Palmchat n.k
hadi anakuja kumaliza kutembelea mitandao hiyo yote tayari siku imepita.
Hebu tuwe namuda maalum wa kuwa katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii pia.
Watu wengihuamini Dini kuliko kumwamini Yesu kristo aliye njia, kweli na uzima.
Nenda
kanisani na uishi kwa kulifuata neno la Mungu na so mapokeo ya kanisa au Dini.
Mahusiano
yetu kati ya wazazi,ndugu,jamaa,wafadhili wetu, watoto,wafanyakazi
wenzetu,wakuu wetu wa kazi, boyfriends/girlfriends ……hawa wote wanauwezo mkubwa
wa kututenga au kupoza upendo wetu kati yetu na Mungu. Ni asili yetu wanadamu
kuwa na Mahusiano, lakini tusiruhusu moja ya uhusiano huu kuwa kuwa na nguvu
kuliko Mungu .
Uhusiano wa
girlfriends, boyfriends na wakuu wetu wa
kazi ni uhusiano hatari sana ambao una 100% za kutuweka mbali na Mungu wetu.
Tuwe makini na wakuu wetu wa kazi na tusiwe na girlfriends au boyfriends kwani
ni dhambi.
WAEFESO 5:3 “Lakini uasherati usitajwe kwenu
kamwe, wala uchafu wo wote wa kutamani, kama iwastahilivyo watakatifu;”
Hakikishaunatenga muda wa kuwa na Mungu wetu.
Katika
ratiba zetu lazima kuwepo na muda wa Kusoma neno na kuomba. Na mruhusu Mungu
akuongoze.
Kazi zetu
hutufanya kuwa mbali na Mungu. Kwa maana watu wengi huwa tunatumia muda mwingi
kwa kazi na kumsahau Mungu. Wakati mwingine tunajikuta katika wakati mugumu
tunapokuwa kazini. Tufanye kazi kwa bidii na tutenge muda wa kuwa na Mungu wetu
pia.Tusiwe kama Martha Bali tuwe kama Mariam LUKA 10:38-42
Our hobbies
can consume a lot of time.
Hobby ni
jambo alipendalo mtu.
Hobbies zetu
hutuchukulia muda mwingi sana.
Tunapaswa
tuwe na kiasi katika hobby . 2 TIMOTHEO
4:5 “Bali wewe, uwe na kiasi katika mambo yote, vumilia mabaya, fanya kazi
ya mhubiri wa Injili, timiliza huduma yako.”
Pia kuna
hobbies zingine ambazo moja kwa moja ziko kinyume na mapenzi ya Mungu. Hivyo
tunapaswa kuziacha mara moja katika Jina la Yesu, sema Amen kama umeelewa.
8. Kuhitaji baraka za Mungu
kuliko Mungu mwenyewe
Tuutafute
kwanza ufalme wa Mungu na hayo mengine
yaani baraka tutazidishiwa.
Tunapaswa
tumtafute Mwenye vitu na siyo vitu. Tukimpata mwenye vitu tujue tumeshapata
vitu.
MATHAYO 6:33“Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.”
Wachungajinao wanaweza kututenga na Mungu.
Wachungaji
wengi huaminisha waumini kuwa wao Ndio wanajua kila kitu…….na sababu hiyo husema hakuna haja ya kuhangaika kusoma
Vitabu vya neno la Mungu tukiwa nyumbani.
Je, unaweza
kuishi juma zima kwa kula mlo mmoja tu kwa siku zote hizo? Hapana haiwezekani.
Kama haiwezekani vivyo hivyo kwa Roho zetu ni ngumu kuishi kwa mlo mmoja tu kwa
juma lote.
Hata kama
umezingwa na shughuli jitahidi kupangilia ratiba yako ili baada ya Nazi uwe na
muda wa Kusoma Biblià na kuomba.
KUMBUKA: Siwajibu wa wachungaji kutulisha kila tunachohitaji Kiroho Bali ni Wajibu wetu.
Kwa asili tuwenye dhambi na tunapofuata asili yetu tuna kuwa mbali na Mungu.
Kwa
sababu hiyo nasi ni vyema tukaishi kwa
kumfuata Mungu wala tusifuatishe matakwa ya miili yetu.(tamaa zetu wenyewe).
Tujikane na tuishi ndani ya Kristo WARUMI7:15-21
TumruhusuMungu aichunguze na kuitengeneza mioyo yetu. ZABURI 139:23-24.
MUNGU AKUBARIKI SANA KUJIFUNZA MANENO YA MUNGU KUPITIA BLOG HII YA nchiyaukomboziministrytz.blogspot.com
PIGA/TUMA MESEJI HAPA +255714890889
UNAWEZA KUTUMA SADAKA YAKO KWA AJILI YA HUDUMA
TUNA UNUNUZI WA VIFAA VYA HUDUMA .
1. VITI
2. SPIKA
3. VITAMBAA VYA MADHABAHU
4. UPANUZI WA KIWANJA CHA KANISA
KIASI CHOCHOTE TUNAPOKEA NA MUNGU ATAKUBARIKI.
KABLA HUJATUMA WASILIANA NA MCHUNGAJI KWA NAMBA HAPO JUU.
0 Comments