SOMO:KUMPENDA MUNGU HAKUKO MDOMONI BALI NI KWA KUISHI MAISHA MATAKATIFU
Tangazo
Bwana Yesu
asifiwe wana wa Mungu ni siku njema tena Bwana ametupa kwa neema yake.Hivyo
hatuna budi kurudisha heshima na utukufu kwake.
Pale
unaposema unampenda Mungu halafu uishi maisha yanayompendeza ni kosa kubwa
sana.Watu wengi wakiulizwa unampenda Mungu kila mtu.atajibu ndio na wala hakuna
atakayesema hapana ata yule mpagani.Mtu Mungu siku ya leo Bwana analo neno Juu
yako usiseme unampenda Mungu wakati maisha unayoishi yanamtukuza Shetani uwe na
uhakika Jehanamu itakumeza.
MATHAYO
15:8"WATU HAWA UNIHESHIMU KWA MIDOMO ILA MIOYO YAO IKO MBALI NAMI"
Nyakati za
leo watu humpenda Mungu kwa midomo yao
ila maisha yao hayako kwa Mungu.uwenda nasema na wewe unayesoma ujumbe huu
unasema unampenda Mungu wakati wewe ni mzinzi/muasherati, unasema unampenda
Mungu wakati wewe ni msengenyani,unasema unampenda Mungu wakati hutoi fungu la
kumi, unasema unampenda Mungu wakati wewe ni mwizi, unasema unampenda Mungu
wakati wewe ni Muongo, unasema unampenda Mungu wakati husaidii wenye shida
,unasema unampenda Mungu wakati wewe mtukanaji, mtu wa Mungu nataka nikwambie
kusema kwako unampenda Mungu halafu njia zako ni ovu uwe na uhakika Jehanamu
utaenda kama usipo tubu leo na kuacha Maovu yako.
Kumpenda
Mungu si swala kusema kutoka mdomoni tu bali la kupasa upendo huo utoke kutoka
moyoni mwako.Kama vile Mungu alivyo
upenda ulimwengu huu hata akamtoa mwanaye wa pekee ili ulimwengu ukombolewe nɗivyo
ivyo yatupasa nasi kumpenda Mungu .
YOHANA
14:15"MKINIPENDA MTAZISHIKA AMRI ZANGU
Tunaona hapo
wana wa Mungu kumbe ukimpenda Mungu lazima uzishike amri zake ,uwezi kusema
unampenda Baba ako halafu anakuagiza jambo unaenda kinyume na alivyosema ,amua
leo mtu wa Mungu kujitenga na mambo ambayo yanakufanya usimpende Mungu toka
moyoni mwako kwani itakuwa ni hasara kubwa watu wanajua unampenda Mungu mwisho
ukajulikani ulikuwa humpendi hakika itakuwa ni aibu kubwa sana.
Ni muda wa
kujitathimin kweli unampenda Mungu au unasema tu ila matendo yako kinyume na
maneno yako.
MITHALI
8:17"NA WAPENDA WALE WANIPENDAO NA WALE WANITAFUTAO KWA BIDII WATANIONA"
Mungu
anasema nawapenda wale wanipendao na ikiwa watanitafuta kwa bidii wataniona,
uwezi kusema unampenda Mungu wakati huna Muda kusoma neno lake, uwezi kusema
unampenɗa Mungu wakati huna Muda wa kuomba ,hapo uwezi sema unampenda wakati
huna wasaa wa kumtafuta.Mtu Mungu amua leo kumpenda Mungu kwa moyo wako wote.
0 Comments