Follow us

MAMBO KUMI YA KUFANYA ILI UWEZE KUPATA KIBALI MBELE ZA MUNGU

Tangazo

 


MAMBO KUMI YA KUFANYA ILI UWEZE KUPATA KIBALI MBELE ZA MUNGU 

1: KUTENDA MEMA

Matendo mema huleta kibali MUNGU alipokuwa anaona wivu kwa ajili ya  ndugu yake Habili . Mwanzo 4:7 Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.

Mpendwa wangu tenda mema utapata kibali.Fanya mema kuliko wenine nawe utaona kibali chako kikiongezeka . Pokea uwezo huo wa kutenda mema kwa uweza wa jina la YESU.

2: KUSHIKA  NENO LA MUNGU.

Katika mithali Sura 3 unaona mambo makuu mawili ili uweze kupata  KIBALI NA AKILI NZURI. Mungu wetu anayo hazina ya Kibali na akili nzuri kwa  watu watakaolishika  na wale  watakaotembea katika rehema na kweli.

Mithali 3:1-4

1 Mwanangu, usiisahau sheria yangu, Bali moyo wako uzishike amri zangu.

2.Maana zitakuongezea wingi wa siku. Na miaka ya uzima, na amani.

 3 Rehema na kweli zisifarakane nawe; Zifunge shingoni mwako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.

 4 Ndivyo utakavyopata kibali na akili nzuri, Mbele za Mungu na mbele ya mwanadamu

Neno Rehema limetafsiriwa kwa lugha ya kingereza kama huruma  ndio maana unakuta unapowauhurumia wengine uwe na uhakika kwamba utakuwa na kibali.Kinyume chake ni kweli kwa mtu  mkatili asiye na huruma watu huwa wanamuogopa na kuwa mbali naye.

3: KIBALI KUTOKANA NA  KUTUMIKI KUSUDI LA MUNGU .

weza kulitambua kusudi la kuumbwa kwako uwe na  uhakika kabisa kibali cha MUNGU kitaachiliwa kwako kuhakisha kwamba unalifanikisha. Kbali hiki kilikuwa juu ya MUSA Kutoka 11:3 Bwana akawapa watu hao kibali machoni pa Wamisri. Zaidi ya hayo, huyo Musa alikuwa ni mkuu sana katika nchi ya Misri, machoni pa watumishi wa Farao, na mabalbali choni pa watu wake.

Ukisoma kwa utulivu kuanzia mstari wa pili utagundua kwamba MUNGU aliachilia kibali kwamba kila walichokihtaji kutoka kwa Wamisri wakaweza kupatiwa. Hiki ndicho kibali alichokipata Nehemia mbele ya mfalme na kuruhusiwa  kupewa vitu kwa ajili ya ujenzi wa ukuta wa Yerusalemu.

Mungu wetu ambaye hhabadiliki na akuachilie kibali hiki sawa na lile kusudi la kuumbwa kwako katika jina la Yesu.

4: KIBALI  HUJA KWA MAOMBI.

Kuna watu wanasema kibali hakiombwi lakini utamuona Esta na Wayahudi wakiomba kibali kwa MUNGU aweze kupata kibali mbele za Mfalme. Uende ukawakusanye Wayahudi wote waliopo hapa Shushani, mkafunge kwa ajili yangu; msile wala kunywa muda wa siku tatu, usiku wala mchana, nami na wajakazi wangu tutafunga vile vile; kisha nitaingia kwa mfalme, kinyume cha sheria; nami nikiangamia, na niangamie.  Esta 4:16

 

MUNGU AKUBARIKI SANA

MAOMBI NA MAOMBEZI

WASILIANA NA MCHUNGAJI LAURENT MPOMA

+255714890889

WHATSAP: +255762756542

YOUTUBE: youtube.com/channel/UCjXjSSDOweHXL3YE5edBNIg

Post a Comment

0 Comments