Shetani
hupigana dhidi yetu na mbinu yake moja ni kutufanya tuhisi vibaya kujihusu.
Hutukumbusha kuhusu kutofaulu na udhaifu wetu wote, lakini tunahitaji kukumbuka
kwamba Mungu anajua mambo yote kutuhusu na hata hivyo anatupenda.
Tunapigana
vita vingi, lakini pengine vita vikuu tunavyopigana ni vile tunavyopigana nasi
wenyewe. Huenda tukang’ang’ana na hisia kwamba tungefikia mengi maishani kuliko
yale tuliyo nayo; huenda tukahisi kwamba tumekosa kufaulu kwa njia nyingi.
Hatuwezi kubadilisha lolote kwa kusikitika na kung’ang’ana ndani yetu. Ni Mungu
tu anayeweza kutubadilisha tunapomwamini. Atapigana vita vyetu na kushinda.
Jukumu letu ni kuamini, kushirikiana naye, na kufuata uongozi wa Roho
Mtakatifu.
Ni vigumu
kufikia mahali ambapo tunaweza kujiambia ukweli kuhusu dhambi zetu na
kutofaulu, kutoweza na makosa yetu ilhali huku tukijua kwamba tunaonekana kuwa
hatuna maksoa mbele ya Mungu kwa sababu ya kile Yesu alifanya kwa niaba yetu
alipotufia na kufufuka kutoka wafu. Iwapo una vita ndani yako, kujua kuwa wewe
ni mwenye haki wa Mungu ndani ya Kristo ni ufunguo wenye uwezo mkuu wa
kukuingiza katika amani na uwezo wa kiroho.
Tunaweza
kubadilishwa tunapoabudu na kumtazama Mungu—sio tunapojitazama, tukijiongezea
udhaifu wetu mwingi.

0 Comments