Follow us

MADHARA YA KUTUNZA UCHUNGU KWENYE MOYO.

Tangazo

 

Mchungaji Laurent Mpoma

MADHARA YA KUTUNZA UCHUNGU KWENYE MOYO.

MITHALI 4:23 "Linda sana moyo wako kuliko yote uyalindayo; maana huko ndiko zitokako chemchemi za uzima" unaona, moyo haukuumbiwa kuingiza vitu, ila kutoa chemchemi za uzima. Kwa mantiki hii, moyo unapoingiza vitu na vikakaa huko ndani, vitu hivyo vinakuwa mzigo na kuanza kuharibu mfumo mzima wa utendaji kazi wake.

MITHALI 12:25 "Uzito katika moyo wa mtu huuinamisha; Bali neno jema huufurahisha" kwa hiyo dalili ya kwanza kwamba moyo wako umeingiza vitu ambavyo havikustahili na umeshindwa kuvibeba ni moyo kuwa mzito! Moyo unakuwaje mzito?

ISAYA 38:15b "Nitakwenda polepole miaka yangu yote, kwasababu ya uchungu wa nafsi yangu" Nisikilize itakusaidia, uzito ndani ya moyo hauwezi kuathiri moyo peke yake! Moyo ukiwa mzito unaenda kuathiri pia mfumo wa akili, na mfumo wa akili ukiathirika na mwili mzima unaathirika, check huyu mtu anasema nitakwenda polepole siku zote za maisha yangu, kinachosababisha aende polepole ni uchungu uliomo moyoni mwake.

Uchungu unapozidi moyoni na moyo ukaelemewa, moyo huanza kusambaza uchungu huo mwilini kama sumu, kutokana na kushindwa kuhimili, kwasababu moyo una kiwango cha kubeba vitu. Ndio maana utamkuta mtu akiwa na uchungu mwingi moyoni kuna wengine huota vidonda mdomoni, hayo ni majibu ya moyo kwamba, alo huku mimi nimezidiwa kwa hiyo kama kuna namna ya kuutoa mzigo huu naomba uutoe.

Sasa unaweza kuelewa kwani Mungu anasema anatusamehe makosa yetu kawaajili yake mwenyewe na si kwaajili yetu ISAYA 43:25, hii ni kanuni ambayo Mungu anataka kutufundisha kwamba tusibebe mizigo ya chuki na uchungu mioyoni mwetu kwa kushindwa kusamehe, kwasababu Mungu anajua athari za kutokusamehe na kutunza uchungu mioyoni mwetu! Ndio maana anatufundisha kwamba, tunaposamehe ni kwa faida yetu wenyewe na wala si ya wale tunaowasamehe.

Ningependa nizungumze mengi sana juu ya hili lakini kwa leo naomba niishie hapa! Kama unahisi shida za mwili wako ulizonazo kama vile magonjwa, na dalili nyingine nilizozitaja hapo juu vimesababishwa na uchungu moyoni mwako, na umeshindwa kabisa kusamehe, mwendee yesu kwa imani na umkabidhi mizigo hiyo sawasawa na MATHAYO 11:28-30 naye ni mwaminifu, atakutua mizigo hiyo na kukupa  raha nafsini mwako. Ubarikiwe sana

MUNGU AKUBARIKI SANA KUJIFUNZA MANENO YA MUNGU

MAOMBI NA MAOMBEZI

WASILIANA NA MCHUNGAJI LAURENT MPOMA

NCHI YA UKOMBOZI MINISTRY

(HEMA LA MAOMBI NA MAOMBEZI)

PHONE: +255714890889

WHATSAP: +255762756542

TUMA MAHITAJI YAKO LEO MCHUNGAJI ATAKUOMBEA NA KUKUPATIA USHAURI.

>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>> 

SOMA : (2 MAMBO YA NYAKATI 1:7:  Usiku ule Mungu akamtokea sulemani, akamwambia, omba utakalo nikupe).

Tunaupanuzi wa kiwanja cha kanisa ambacho kinahitaji shilingi milioni tatu (3,000,000/=). Kiasi chochote tunapokea. MUNGU akubariki sana kwa utoaji wako. Hakika Amini Mungu anakwenda kukutana na wewe kama sulemani alivyotokewa usiku ule sasa ni zamu yako.

UNAWEZA KUTUMA HAPA

MPESA: +255762756542……………..JINA: LAURENT MPOMA

TIGO PESA: +255714890889…………JINA: LAURENT MPOMA

AIRTEL MONEY: +255782859946…….JINA :LAURENT MPOMA

CRDB BANK: 0152363022800………LAURENT ELIAS MPOMA

NMB BANK: 50810025078……..LAURENT ELIAS MPOMA

 

 

Post a Comment

0 Comments