Follow us

KUOMBEA HALI YA KIROHO YA ARDHI ILI UFANIKIWE KIMAISHA

Tangazo

 

MCHUNGAJI LAURENT MPOMA

SOMO: KUOMBEA HALI YA KIROHO YA ARDHI ILI UFANIKIWE KIMAISHA.

Kuna uhusiano sana kati ya ardhi na mafanikio yako kwa hiyo ni muhimu sana kulifuatilia kwa karibu sana somo hili

MFANO WA KWANZA

Mwanzo 3:17-19

"Akamwambia Adamu, Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nalikuagiza, nikisema, Usiyale; ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako; michongoma na miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni; kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi"

Laana maana yake ni

>>>Kutostawi

>>>Kutofanikiwa

>>>Kutokuwa na Furaha

>>>Kutofikia kiwango cha mafanikio ambacho Mungu kakikusudia kwa ajili yako. Na Laana ni kinyume cha baraka.

Mungu aliposema ardhi imelaaniwa alikuwa anataka kumuambia Adamu kuwa ukitaka kujua kitu gani umebeba kwa kutofuata maelekezo yangu kuwa kuna laana iliyoko kwenye maisha yako na utakapoilima ardhi haitakuzalia matunda yake.

MFANO WA PILI

Mwanzo 4:11-12

"Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako; utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani."

Laana ya hapa sura ya nne ni tofauti na ile sura ya tatu kwa sababu laana ya Adamu ilikuwa ndani ya Adamu lakini katika sura ya nne tunaona kuwa laana ipo kwenye ardhi moja kwa moja.Maana yake kwa kila mtu atakaye kanyaga eneo hili anapata ile laana iliyoachiliwa kwenye ardhi .

MFANO WA TATU

2 Mambo ya Nyakati 7:11-14

"Nikizifunga mbingu isiwe mvua, tena nikiamuru nzige kula nchi, au nikiwapelekea watu wangu tauni; ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao"

 

Uponyaji tunaoungalia hapa ni uponyaji wa ardhi na nchi ni ardhi yenye mipaka halali ya kiumiliki,biblia inaposema kuwa nchi maana yake ni ardhi na sio watu au taifa. Taifa ni ni kundi la watu waliokubaliana na mfumo wa uongozi na wakae kwa pamoja. Kwenye biblia unaona kabila linageuka kuwa Taifa au familia kuwa taifa. (Angalia katika Kitabu cha Mwanzo 49)

Mwanzo 49:1,28

­"Yakobo akawaita wanawe, akasema, Kusanyikeni, ili niwaambie yatakayowapata siku za mwisho.Hizo zote ndizo kabila za Israeli kumi na mbili. Na hayo ndiyo aliyowaambia baba yao, na kuwabariki; mmoja mmoja kwa mbaraka wake aliwabariki"

Hapa biblia haizungumzii uponyaji wa watu bali ni ardhi .Biblia inasema tena nikiamuru nzige kula nchi maana nzige ni wadudu waharibifu na wanaoharibu mazao au udongo na Tauni ni ugonjwa wa kuambukiza na kibiblia ikitokea ugonjwa wa kuambukiza ina maana kunakuwa na shida kwenye ardhi.

Ukitokea ugonjwa wa kuambukiza katika eneo fulani huwa wanaweka karantini na kufunga mipaka. Kitendo cha kuweka mpaka ni Roho Mtakatifu anawajulisha kuwa shida hii imeishia mpaka hapa.

Suala hili la kufunga mipaka ili kuzuia maambukizo ya ugonjwa ni ya kiroho kwanza kabla hayajawa ya kimwili.

MFANO WA NNE

Yeremia 22:29-30

"Ee nchi, nchi, nchi, lisikie neno la Bwana. Bwana asema hivi, Andikeni habari za mtu huyu kwamba hana watoto, kwamba mtu huyu hatafanikiwa siku zake zote; maana hapana mtu katika wazao wake atakayefanikiwa, akiketi katika kiti cha enzi cha Daudi, na kutawala tena katika Yuda."

Huyu ni Mungu anazungumza na nchi (ardhi yenye mipaka halali ya kiumiliki) anaposema

>>>Ee nchi ,nchi sikia ---- ina maana nchi inasikia

>>>Andika maana yake inaweza tunza kumbukumbu

>>>Kuwa hatafanikiwa maana yake ni kuwa inaweza fuatilia

Wakati adhabu inatolewa kwa mtu huyu alikuwa bado hana watoto, lakini kumbukumbu iliandikwa kwenye ardhi kuwa hata watoto wake wakija nao wasifanikiwe. Adhabu ilitolewa kwa sababu gani; angalia mstari wa 21 Mimi nalisema nawe wakati wa kufanikiwa kwako; lakini ulisema, Sitaki kusikia. Hii ndiyo iliyokuwa desturi yako tangu ujana wako, kutokuitii sauti yangu.

Fikiria wewe ni mtoto na umeingia kwenye adhabu ya baba au mama na unatafuta kufanikiwa na haufaninikiwi sio kwamba akili huna bali unazo lakini umezuiliwa kufanikiwa na ardhi kwa sababu ya kosa la baba yako na mama yako je unaombaje?

 MFANO WA TANO

Mwanzo 28: 10-20

"10-13"Yakobo akatoka Beer-sheba , kwenda harani. Akafika mahali Fulani akalala huko usiku kucha , maana jua lilikuwa limekuchwa ,akatwaa jiwe moja la mahali pale akaliweka chini ya kichwa chake , akalala usingizi palapale. Akaota ndoto, na tazama ngazi imesimamishwa juu ya nchi, na ncha yake yafika mbinguni .Tena tazama malaika wanapanda na kushuaka juu ya yake. Na tazama Bwana amesimama juu yake , akasema mimi ni Bwana, Mungu wa Ibrahim baba yako na Mungu wa Isaka , nchi hii uilalayo ntakupa wewe na uzao wako"

Lile Neno nchi hii ulalayo Kwa lugha nyingine ardhi unayolala iwe ni nyumba uliyojenga au hoteli au umejilaza mahali kwa muda mfupi au ni kwenye basi umelala au uko shambani umelala na ghafla unaota ndoto, sio kila mahali angeweza kulala ila eneo lile lilikuwa na umiliki kamili wa Mungu.

MUNGU AKUBARIKI SANA KUJIFUNZA MANENO YA MUNGU

MAOMBI NA MAOMBEZI

WASILIANA NA MCHUNGAJI LAURENT MPOMA

NCHI YA UKOMBOZI MINISTRY

(HEMA LA MAOMBI NA MAOMBEZI)

PHONE: +255714890889

WHATSAP: +255762756542

TUMA MAHITAJI YAKO LEO MCHUNGAJI ATAKUOMBEA NA KUKUPATIA USHAURI.

>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>

SOMA : (2 MAMBO YA NYAKATI 1:7:  Usiku ule Mungu akamtokea sulemani, akamwambia, omba utakalo nikupe).

Tunaupanuzi wa kiwanja cha kanisa ambacho kinahitaji shilingi milioni tatu (3,000,000/=). Kiasi chochote tunapokea. MUNGU akubariki sana kwa utoaji wako. Hakika Amini Mungu anakwenda kukutana na wewe kama sulemani alivyotokewa usiku ule sasa ni zamu yako.

UNAWEZA KUTUMA HAPA

MPESA: +255762756542……………..JINA: LAURENT MPOMA

TIGO PESA: +255714890889…………JINA: LAURENT MPOMA

AIRTEL MONEY: +255782859946…….JINA :LAURENT MPOMA

CRDB BANK: 0152363022800………LAURENT ELIAS MPOMA

NMB BANK: 50810025078……..LAURENT ELIAS MPOMA

 

 MUNGU AKUBARIKI SANA.

 

Post a Comment

0 Comments