Follow us

MAMBO SABA (7) YA KUZINGATIA ILI MAOMBI YAKO YAJIBIWE

Tangazo

 

MCHUNGAJI LAURENT MPOMA
HUDUMA YA NCHI YA UKOMBOZI
(HEMA LA MAOMBI NA MAOMBEZI)

1. KUKAA NDANI YA KRISTO.

Ni ngumu kuishi nje y mzabibu na kuzaa matunda hivyo ili maombi yako yapate majibu lazima ukubali kuishi ndani ya wigo na uongozi wa kumkubari Kristo na yeye kuwa sababu ya matokeo yako unayohitaji kupitia maombi.Kuwa ndani ya wigo kutakufanya usiwe kinyume nq yale maelekezo anayotoa

Yohana 15:7

7 Ninyi mkikaa ndani yangu na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni lo lote mtakalo nanyi mtatendewa.

 Kukaa ndani yake na neno lake kukaa ndani yetu basi ni rahisi kupokea as long kuna utimilifu wa vitu hivi vyote tunavyojifunza sasa.

2. Imani ni moja ya mambo saba ambayo ukiwa huna huwezi kupata majibu sawasawa na unacho omba na wakati mwingine kutindikiwa na imani hufanya maombi kuharibika na kubaki ukisubiri kitu ambacho imani yako ilishatindika.

Matayo 14:26-28

26 Lakini wanafunzi wake walipom wona akitembea juu ya maji, waliingiwa na hofu kuu. Wakasema, “Ni mzimu.” Wakapiga mayowe kwa hofu. 27 Lakini mara moja Yesu akasema nao, akawaambia, “Jipeni moyo. Ni mimi; msiogope.”

28 Petro akamjibu, “Bwana, kama ni wewe, niambie nije kwako nikitembea juu ya maji.

Kupunguka kwa imani ya Peter ndipo kulipoleta ule uzamaji wake ukisoma mistari ya hapo chini.Hivyo Mungu qnaweza kutoa jibu la maombi yako ila kinachoharibu ni baada ya wewe kuanza kuwaza yale nilioomba kweli Mungu atafanya?basi unasababisha malaika aliyekua ametumwa kuleta taarifa zenye tumaini kurudi mbinguni.imani ikipung7q qu kuweka tashwishwi basi ni moja ya kufanya kile tunachokiomba kisitoe majibu.

Waebrania 11:6

6 Na pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu kwa maana kila mtu anayemjia ni lazima aamini kuwa yupo na kwamba yeye huwapa tuzo wale wanaomtafuta kwa bidii.

Marko 11:24

Kwa hiyo nawaambieni, mnaposali na kuomba kitu, aminini kwamba mmekipokea, nanyi mtapewa.

Ukiweka shaka basi tayari unachafua na kuharibu maombi yako.

3. OMBA KATIKA ROHO.

Kuomba kusiko na kikomo huomba kuliko na uendelevu,ukimruhusu roho mtakatifu akufundishe namna ya kuomba huwezi kuacha kuomba kila muda hata umelala utashangaa unaomba katika roho,hauchoki na hii inakua constantly,mtumishi mmoja anasema kuomba Yesu alijua lazima kila mkristo aombe ila kule kunakoleta majibu ni kudumu kutika kuzungumza na Mungu sababu kila unapomkumbusha nini unahitaji ni rahisi kupewa kile kilichobora.

Waefeso 6:18

Salini daima, mkiomba msaada wa Mungu. Salini kila wakati kwa nguvu ya Roho. Kesheni bila kuchoka mkisali kwa ajili ya watu wote wa Mungu.

Ukiweka limitations katika kumtafuta Mungu basi nayeye ataweka limitations pia hivyo hebu kuomba kwetu kunakoleta majibu sio mpk watumishi humu ndani wasema maombi wakati mwingine ona maisha yangu kama mjori wa Kristo nahitaji kumtafuta Mungu.kuna vitu haviwi vyetu kama hatujavilazimisha kuwa vyetu kujenga utarstibu au mazoea ya kuongea na mpenzi Yesu.

Nguvu ya roho: hii nimeona mara nyingi kwa upande wangu najua hata kwako unaiona umelala unashituka unakuta ulikua unaomba rohoni na kuna muda unashangaa umeshurutishwa kuomba sio kwa kuzungumza bali kwa moyo hutoi maneno ila unaomba na unaona unahitaji kuwa katika hali hio kwa muda mrefu.kikawaida unaweza usielewe ila Roho Mtakatifu kuna mambo anakuvusha na anakupa ushindi kwa kisemo rahisi wa goli la mkono bila kutumia nguvu nyingi.

4. KUSIMAMA KATIKA KATIKA NENO.

Maombi yako ili yapate kujibiwa yanahitaji neno la Mungu,umewekeza nini unachokijua juu yako mbele za Mungu ukitumie kukidai,je haki zako unazifahamu na unazitumiaje kuomba.

Zaburi 119:105-106

Neno lako ni taa ya kuniongoza, na mwanga katika njia yangu. Nimeapa na kuthibitisha kiapo changu, kwamba nitashika maagizo yako adili.

Neno litasimama kukutengeneza au kukuelekezq nini unapashwa kuomba mbele za Bwana

Niliwahi kusikiliza ushuhuda wa mtu anasema kuna maombi yanahitaji majibu ya papo kwa papo na kuna yale yanahitaji muda ili kutokea hivyo yale yanayotokea papo kwa hapo basi yasikufanye unapoomba maombi ya kutokea baada ya miaka 10 yakufanye usiamini Mungu atajibu,jambo zuri ni kuishi ndani ya neno na kutokutoka kwenye kile ulichoomba na kuamini utapokea.

5. UWE MTU MWENYE KUSHUKURU.

Kuna mambo Mungu anatufanyia bila kumuomba basi hata kwa hayo tuwe na neema ya kumshukuru maana katika yale mambo madogo ayafanyayo basi kutafanya kuyanyunyiza yale mambo makubwa kutokea.

Mathayo 11:25-26

Wakati huo Yesu alisema, “Nakushukuru ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, maana umewaficha wenye hekima na wenye elimu mambo haya, ukawafunulia wadogo. Naam, Baba, ndivyo ilivyokupendeza.

Kuna mambo hayafiki sababu hujajua namna ya kumshukuru Mungu hebu mrudishie utukufu kwa vile alivyofanya kwako na kwa ule umbali aliokutoa ili vile vilivyokua vimesubiria wewe kushukuru viachiliwe

Kuna watu sio tu hawajui kumshukuru Mungu hata watu waliofanya vitu kwenye maisha yao hawajawahi kuwambia asanteh hivyo inawawia ungumu kujua kama huyu mtu alifurahia vacation niliyompa au extra bonus ya mshahara wake niliyoongeza hakupenda?ndoa nyingi zinaonekana za kizamani sababu baadhi ya wanandoa wanasahau asanteh ndio siraha ya kufichua hazina zingine kutoka kwa wenzi wao.

 Ilivyo kwa baba,mama,dada,kaka na watu wengine Mungu mwenyewe anapenda tumshukuru kwa afya zetu,uhai ambao hatuna uwezo wa kulipia hata kwa saa moja hewa yake hivi vyote vinaweza kukuangezea usikivu kwa Mungu akupe vile vyenye thamani ambavyo umeomba.

6. UWE NA KAZI UNAFANYA.

Katika utekelezaji wowote wa maombi yanahitaji mtu awe na kitu ili kupitia kile anachoomba kibarikiwe na kifike kule wewe muombaji unaomba.Kuna watu wanaomba kuwa wafanyabiashara wazuri wakati hata mtaji wa kuuzq karanga hana unampa kazi Mungu ya kuangalia aanze wapi kukubariki,maombi yanahitaji utendaji huwezi kutaka kuwa mtu fulani bila kuwepo na maandalizi.Anahitaji abariki uimbaji wako anza kuimba ainue watu watakaokaa upande wako watembee na wewe,unahitaji gari basi uwe na mradi unaoweza kukupa milioni 10 au zaidi kutokana na kile unachohitaji,wengi tumebaki kuamini katika miujizq na kusahau kufanya kazi.

2 Wathesalonike 3:6-8

Onyo Kuhusu Uvivu

6 Ndugu wapendwa, katika jina la Bwana Yesu Kristo, tuna waagiza mjitenge na kila ndugu ambaye ni mvivu na ambaye haishi kufuatana na maagizo tuliyowapeni. 7 Maana ninyi wenyewe mnafa hamu jinsi mnavyopaswa kuiga mfano wetu. Sisi hatukuwa wavivu tulipokuwa nanyi 8 wala hatukula chakula cha mtu ye yote pasipo kulipa. Bali tulifanya kazi kwa juhudi usiku na mchana ili tusimlemee mtu ye yote kati yenu.

Katika maombi mengi tunayoomba yamejaa uhitaji hivyo ili kufullfill uhitaji wetu lazima tufanye kazi tusiwe wavivu kuwaza miujiza only doing work gives us, our aspects of living.Hivyo ni vizuri kuwa na jambo unafanya ili kile unachoomba kisione hata wewe muombaji unaupungufu sehemu.baraka zinatazama nini unacho kwa ajiri ya kuikamilisha baraka ya kile ulichoomba

7. KUISHI MAISHA YALIYOJAA UPENDO.

Kuna watu wanaomba masaa ya kutosha lakini kwa habari ya upendo kuwatendea wengine hawana,na ubaya mkubwa wamejaa kisasi na kutokuachilia.Maombi unayoomba hayawezi kuleta impact yoyote kama huwezi kuuapply upendo kwa watu.

1 Wakorintho 13

Upendo

13 Kama ningekuwa na uwezo wa kusema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa kama kelele ya kengele au toazi. 2 Na kama nina uwezo wa unabii, na kuelewa siri zote na maarifa yote; na hata kama nina imani kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, mimi si kitu. 3 Kama nikitoa mali yote niliyo nayo, na kama nikitoa mwili wangu uchomwe moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu.

4 Upendo huvumilia, upendo hufadhili; upendo hauna wivu au majivuno.

5 Upendo hauna kiburi na haukosi kuwa na adabu. Upendo hau tafuti kujipendeza nafsi; haukasiriki upesi, hauweki orodha ya mabaya. 6 Upendo haufurahii mabaya, bali hufurahia kweli. 7 Upendo huvumilia yote, huamini yote, hutumaini yote, hustahim ili yote.

8 Upendo hauna mwisho. Lakini penye unabii, utakoma; zikiwepo lugha zitakoma; yakiwepo maarifa yatakwisha.

Unaweza kuomba na kufanya mambo mengi yaliyo ya haki lakinj bado ukishindwa kuwa mtu wa upendo bado huwezi kujibiwa unachokiomba,upendo huambatana na kusamehe ukishindwa kupenda basi hata kusamehe kwako kunakua shida.

Mt 18:22

Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.

Yesu alijua wengi kusamehe ni ngumu hivyo alisema kuwa watu wenye kusamehe ili kusababisha yale yafungwayo kwa kutokusamehe yasiwe kwazo kwetu.

 

MUNGU AKUBARIKI SANA KWA KUJIFUNZA MANENO YA MUNGU.

>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>

Unaweza changia huduma hii kwa njia ya sadaka ili kuwezesha huduma kuendelea na Mungu atakutana na wewe na kujibu hitaji lako.

TUNA UNUNUZI WA:-

1. KIWANJA CHA KANISA -----1,500,000/=

2. SPIKA...................................900,000/= 

3. MAIKI....................................150,000/=

4. MIXER...................................400,000/=

5. BATI......................................30

6. MACHUMA YA HEMA...........10 

7. MBAO........................................30

KABLA HUJATUMA WASILIANA NA MCHUNGAJI KIONGOZI LAURENT MPOMA.

KAMA UKO NJE YA SINGIDA MJINI TUMIA NAMBA HIZI KUTUMA MCHANGO WAKO.

TIGO PESA 0714890889....................JINA: LAURENT MPOMA

M -PESA  0762756542.......................JINA: LAURENT MPOMA

AIRTEL MONEY - 0782859946.......JINA: LAURENT MPOMA


Mchungaji Kiongozi Laurent Mpoma atakuombea moja kwa moja na Mungu wa mbinguni atakuponya na kukurejeshea na kukuvusha kwenye hilo unalopitia.

BARIKIWA SANA.


Post a Comment

0 Comments