NGUVU YA MAOMBI YATOKANAYO NA MUNGU MWENYEWE
Mathayo 7:7 Ombeni, nanyi mtapewa;
tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa.
Kinyume chake ni kuwa usipoomba
hauwezi kupewa kitu hivyo kwa mwana wa Mungu anayehitaji kukua kila siku kiroho
na kimwili anapaswa kuwa muombaji.
Aina hizo za maombi ni kama ifuatavyo
1.MAOMBI YA AKILI
Haya ni maombi ambayo mtu anapanga
vitu ambavyo anahitaji Mungu amtendee na anakwenda navyo kwenye maombi yake
Mtu anaweza akawa anahitaji Mungu
ampe Mme au mke mwema, ajira, kibali n.k kwahiyo anavipangia mda wa kuviombea
vipaumbele hivi
Zaburi 5:3 Bwana, asubuhi utaisikia
sauti yangu, Asubuhi nitakupangia dua yangu na kutazamia.*
Kwa maana nyingine unamuita Mungu
muumbaji ili akusaidie mambo yako uliyoshindwa kwa akili zako na nguvu zako
Zaburi 57:2 Nitamwita MUNGU Aliye
juu, Mungu anitimiziaye mambo yangu.
Kwahiyo utaona yakwamba haya ni
maombi yatokanayo na akili za mtu.
Lakini kuna aina nyingine ya maombi
ambayo kimusingi ndiyo yaliyobeba Ujumbe huu
2.MAOMBI YATOKANAYO NA
MUNGU MWENYEWE*
Haya ni maombi yanayokuja nje ya
ratiba na vipaumbele vya mtu
Yaani mtu anajikuta anaombea kitu
ambacho hakukipanga tena wakati mwingine kwa mda ambao hakupanga aombe
Kibiblia aina hii ya maombi
inatambulika pia kama
➡Maombi ya roho*
➡Au maombi ya kinabii*
Biblia inasema nitaomba kwa roho tena
nitaomba kwa akili pia
1 kor 14:15 Imekuwaje, basi? Nitaomba
kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia; mtaimba kwa roho, tena nitaimba kwa
akili pia.
Kwahiyo kuna maombi ya akili na
maombi ya roho
Maombi ya roho ni maombi yatokanayo
na Mungu na haya ndiyo maombi yenye nguvu maana yanagusa kwenye kiini cha
maisha ya mtu moja kwa moja
Maombi ya roho ni maombi yenye uvuvio
maalumu wa Roho mtakatifu, mtu anajikuta anabubujika rohoni kwaajili yake au
wengine.
MAOMBI NA MAOMBEZI
TMA MAHITAJI HAPA
0762756542
WHATSAP 0762756542
0 Comments