SOMO: UKIAMINI YOTE YAWEZEKANA
Maandiko: Marko 9:19-23
19
Akawajibu, akasema, Enyi kizazi kisichoamini, nikae nanyi hata lini?
Nichukuliane nanyi hata lini? Mleteni kwangu 20 Wakamleta kwake; hata
alipomwona, mara yule pepo alimtia kifafa; naye akaanguka chini, akagaa-gaa,
akitokwa na povu. 21 Akamwuliza babaye, Amepatwa na haya tangu lini? Akasema,
Tangu utoto. 22 Na mara nyingi amemtupa katika moto, na katika maji,
amwangamize; lakini ukiweza neno lo lote, utuhurumie, na kutusaidia. 23 Yesu
akamwambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye. 24 Mara babaye yule kijana
akapaza sauti, akasema, Naamini, nisaidie kutokuamini kwangu.
Imani ya
kweli katika Yesu ni msingi imara katika maisha ya kiroho. Ni jibu la mambo
yote. Ni mkono unaochukua majawabu ya mahitaji yetu kutoka ulimwengu
usioonekana na kuyafikisha kwenye ulimwengu wa mwili, tukaona kwa macho na
kushika kwa mikono yetu.
Imani ni
nini?
Basi imani
ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.
(Ebr 11:1)
Imani
inakuthibitishia kuwa kitu unachokihitaji kimepatikana sasa wakati
kinatarijiwa; imani inakiona:kitu halisi na kukikamata wakati hakipo.
Nchi ya
Israeli ilikumbwa na ukame mbaya sana, ikatokea njaa kali, ikasababisha watu
kula watoto wao, punda na mavi ya njiwa. Katika nyakati hizo za ukame nabii
Elisha aliyekuwa na imani katika Mungu alitangaza kuwa kesho kutapatikana unga
tele na nafaka mbalimbali. .Imani iliona mbali ikavuka mipaka ya ufahamu wa
kibinadamu. Askari wa mfalme aliona kmwili Elisha aliona kiroho.
Elisha
akasema, Lisikieni neno la Bwana; Bwana asema hivi, Kesho panapo saa hii,
kipimo cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa
shekeli, langoni pa Samaria (2Fal 7:1)
Kesho yake
kweli yote yalitimia; soma (2Fal 7:1-20) Askari wa mfalme alikufa kwa
kutokuamini.
Imani
inazaliwa na inakua.
Basi imani,
chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo. (Rum 10:17)
Imani ya
kweli inazaliwa kwa kusikia Neno la Kristo. Imani inakua kila wakati
inapotumika kuleta majibu ya mambo magumu. Yesu alifundisha somo la imani
inayoleta matokeo.
(Mathayo
17:20) Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amini,
nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu,
Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana
kwenu.
Imani
inayoweza kuhamisha milima ya matatizo yako yote, inanza na kiasi cha punje ya
haradali iliyo ndogo kuliko punje ya mchicha. Fahamu kuwa punje hiyo ikipandwa
inaota na kukua hadi kuwa mti mkubwa. Na imani yako itakua kwa kadiri
unavyoitumia kutatua matatizo yanayokukabili siku kwa siku.
Daudi
alikuwa na ujasiri wa kukabiliana na Goliathi kwa sababu imani yake ilikua
katika Bwana kwa kuwaua simba na dubu.
(1Sam17:36 )
Mtumishi wako alimwua simba na dubu pia; na huyu Mfilisti asiyetahiriwa atakuwa
kama mmoja wao, kwa sababu amewatukana majeshi ya Mungu aliye hai.
Baba wa
kijana tuliyemsoma hapo juu alimwomba Yesu kwa mashaka akisema, “lakini ukiweza
neno lo lote, utuhurumie, na kutusaidia”. Bwana Yesu alimjibu kwa maneno yake ,
“Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye”. Yule baba alitambua haraka kosa lake
akatubu na kuamini. Yesu akamponya mwanawe saa ileile.
Kizazi chetu
tunafanana na baba huyo; tunafahamu kuwa Yesu anaponya, anaokoa na kutenda
miujiza mingi. Inapokuja kwenye mahitaji yako wewe binafsi imani inapungua.
JiulizeYesu amekufanyia nini? na unamtarajia akufanyie nini katika matatizo
yako? Je unaamini kweli anaweza? Je
moyoni mwako mna mahangaiko na kutangatanga kutafuta ufumbuzi?. Kutokuamini ni
dhambi na kunakukosesha majibu ya mahitaji magumu ya moyo wako. Mungu hashindwi
na neno lolote.
MUNGU AKUBARIKI SANA
MAOMBI NA
MAOMBEZI
WASILIANA NA
MCHUNGAJI LAURENT MPOMA
(NCHI YA
UKOMBOZI MINISTRY)
CALL: +255762756542
WHATSAP:
+255762756542
Youtube>>>Upenyo wa Mungu Tv" kisha SUBSCRIBE
0 Comments