SOMO: KUVUNJA MAAGANO
YA KICHAWI
Maagano: ni makubaliano au mikataba au mafungamano
yanayowekwa kati ya pande kuu mbili au zaid ya mbili ili kupata kitu fulani au
kufikia hatua fulani..
Maagano yanaweza kufanyika katika
majina, vyakula, sehemu watu wanayoishi, uzao fulani n.k
mwanzo 17:1-8, mwanzo 15:4-7, mwanzo 21:18.
Koo nyingi ndani ya africa zilikuwa
zikitumaini katika miungu kama vile mawe,miti mirefu,nyoka wakubwa,vinyago na
aina nyingine nyingi za miungu kutokana na mazingira waliokuwa nayo.lakini
ukweli na kwamba hizo zote n njia tofauti tofaut za kumuabudu shetani...akitoa
baraka zake kupitia vitu hivo ambavyo waanzilishi wa koo zetu walikuwa wameweka
tumaini.
Kila agano la kiimani lina matokeo
yake: nayo matokeo hayo yanadumu katika vizazi vinne (kutoka 20:5, yoeli1:3)
MATOKEO YA MAAGANO KATI
YA SHETANI NA MWANADAMU:
1). Magonjwa ya kurithi
2). Matukio mabaya ya kurithi kama
vile ajali katika mtindo fulani, kupata ukilema,majanga ya kufanana
yanayojirudia rudia katika kizazi fulani..n.k
3). Kuishi sehemu/mji mmoja tu ukoo
mzma.
4). Kuvunjika kwa ndoa kwa watu wa
vizazi vya ukoo husika.
5). Kufanya kazi moja tu hatakama
inawafanya kuwa maskini,,,,mfano....kama mwanzilish wa uko alikiri kwa kinywa
chake kuwa yeye na uzao wake kazi yao n kilimo cha jembe la mkono tu, au n
wapiga debe tu n.k
6). Kutofanikiwa katika ajira, masomo
na shughuli zingine( kama mmoja kati ya waanzilishi wa ukoo husika aliudhiwa na
kutamka kuwa"na tuone kama watafanikiwa" ambayo n maagano katika
maneno.
FAIDA ZA MAAGANO KATI
YA MUNGU NA MWANADAMU:
1).Utabarikiwa kama vile mjini,
mashambani, utoKapo, Uingiapo n.k
2). Uzao wa tumbo lako utabarikiwa,
3).kapu lako la kukandia (maana
nyumba yako haitaon Njaa kamwe.
4).utaheshimishwa n.k
Yoeli 2:12, torati 28
SIFA ZA MAAGANO
Maagano lazima yawekwe kwa gharama
kubwa na pia hulindwa kwa gharama pia.
Kwa mfano maagano kati ya koo zetu za
kiafrika na shetani kupitia mawakala wake kama vile mawe, milima,miti
mikubwa,vibuyu na masanamu, yaliweza kuwekwa kwa kutumia sadaka ambazo n kama
vile damu ya wanyama, fedha, vyakula, pombe, maneno ya kujifunga n.k
Hapo wakisaidiwa kupata mvua, mavuno
mazuri na kuishi salama kumbe huo ulikuwa n ubatili wa shetani na mtego wa
kuzinasa koo zetu katika utawala wake
Tofauti kati ya maagano baina ya
Mungu na shetani :
1).Agano kati ya shetani na
Mwanadamu:
1.
Faida zake hudumu muda mfupi na
madhara yake n ya muda mrefu zaidi.
2.
lengo lake n kuzima mafanikio ya
mwanadamu kwani anajuwa ukifanikiwa utaweza kufanya mamb ya kumdharirisha kama
vile kujenga nyumba za ibada, kusaidia wajane, kutojihusisha na dhamb kama vile
dhuluma, wizi ni
2) sifa zaAgano kati ya mwanadamu na
Mungu.
1.
Faida zake hudumu milele hata milele.
2.
Hufanywa kwa hiari na uhuru wa
kuchagua
3.
Daima hulinda utakatifu wa Mungu.
Kama vile ambavyo nchi haiwez kukaa
bila uongozi na hivo hivo ukoo/familia haiwezi kukaa bila uongozi:
Kwahio ni muhimu kujitambua kuwa nyie
mupo katika uongozi wa nan ?? N Mungu au shetani?? Kama hamuridhik na uongoz wa
roho moja kati ya hizo ndipo harakti za kuvunja mmoja na kujenga mwingine
huanza mara moja kisha wahusika waendelee mbele katika maisha yao ya
ndoa,kiuchumi,kisiasa na mengine yenye mafanikio na baraka tele.
Bila shaka watu huvunja uongozi wa
shetani na kujenga uingozi wa kimungu katika koo/familia zao!
namna ya kuvunja maagano ya
kishetani/mizimu.
1). Hatua ya kwanza lazima wahusika
wa ukoo huo wawepo na kama sio wote wawepo hata wawakilishi wake wakiume kwa
maana urithi upo kwa ukoo wa baba na sio mama (evidenced@ Daniel 9, nehemia1:1...,
2). Kukiri kwa vinywa vyenu kuwa
mumetenda uovu mwingi kwa kumtegemea shetani/mizimu na sio Mungu wa mbinguni
mukitaja na hayo yaliofanywa kwa wakati huo kama mulisimuliwa au munakumbuka.
3). Kusogeza sadaka toka katika vitu
vyenu mulivovipata kiharali kama vile pesa,sehemu ya mazao yenu kama
mchele,mahindi mihogo n.k kwani babu zetu walitumia hivyo kuweka maagano na
shetani ilaa sisi tunavikusanya leo kwajili ya kuvunja. Pia ipo sadaka kubwa
kupita zote nayo n damu ya Yesu. Munatakiwa kuiita kwa imani ili ishuke...hivo
itapendeza kama wote au baadhi yenu mutakuwa mumefunga na kujitakasa. Hiyo damu
ya yesu itatumika kuvunja na kubomoa ufalme wa mizimu.
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
MAOMBI NA MAOMBEZI
WASILIANA NA MCHUNGAJI MPOMA 0762756542
WATSAP 0762756542
TUMA MAHITAJI KWA E-MAIL: mchungajilaurent@gmail.com
fika : NCHI YA UKOMBOZI MINISTRY - MWAJA KITOPE SINGIDA MJINI.
0 Comments