MAMBO 6 YA KUFANYA IKIWA HALI YAKO YA MAOMBI SIO NZURI.
JAMBO LA 1: Omba toba ili Mungu
akusamehe! Ndiyo - omba toba ili Mungu akusamehe kwa kushindwa kuomba! Swali
unaloweza kuuliza, ni kutaka kujua ikiwa kutokumwomba Mungu ni dhambi.
1Samweli
12:23. Iwe ni kutokuwaombea wengine au kutokujiombea wewe - kutokuomba ni
dhambi! Kutokumwomba Mungu si udhaifu bali ni dhambi! Udhaifu katika maombi ni
kule kutokujua jinsi ipasavyo! Ndiyo maana imeandikwa.
1Yohana 3:4
dhambi ni uasi au ni kwenda kinyume cha maelekezo ya Mungu. Kuomba ni agizo na
mwaliko kutoka kwa Mungu, ili upate kuongea naye. Kutokumwomba ni kukataa
mwaliko huo; na ni sawa na kukataa kutii agizo la Mungu. Kwa hiyo kutubu ili
usamehewe kwa kutokumwomba ni hatua sasa. Mungu atakusamehe, na kurudisha ndani
yako hamu ya kuomba.
JAMBO LA 2: Ondoa hali ya kujihukumu
moyoni mwako! Kujihukumu moyoni mwako kunakuondolea ujasiri wa kwenda mbele za
Mungu na kuomba.
1Yohana 3:21,22. "Wapenzi, mioyo yetu
isipotuhukumu, tuna ujasiri kwa Mungu; na lolote tuombalo, twalipokea kwake....(Huu
ni mstari unamhusu yule anayeshindwa kuomba, au kwa sababu anadhani ya kuwa
hata baada ya kutubu Mungu hajamsamehe)
JAMBO LA 3 : "Funga katika nafsi
yako"! Hebu soma mstari huu: "Nalijitesa nafsi yangu kwa kufunga;
maombi yangu yakarejea kifuani mwangu"(Zaburi 35:13).
Daudi
aliyasema hayo alipokuwa anatafuta utatuzi wa yeye kushindwa kuomba kama
alivyokuwa anaomba huko nyuma! Daudi anasema kufunga katika nafsi yake,
kulisaidia kurejesha tena maombi kifuani mwake! Na wewe wewe unaweza ukatumia
mbinu kama hii, ili kurudisha tena uwezo wako wa kuomba!
JAMBO LA 4 : “Fanya maamuzi thabiti
moyoni mwako kuwa utakuwa mwombaji!”
Fahamu hili
ya kuwa: Kufanya maombi ni maamuzi kwanza, kabla hakijawa kitendo! Kufanya
maombi ni jambo la moyoni kwanza, kabla halijawa jambo la mdomoni! Ikiwa huna
maamuzi thabiti moyoni mwako ya kuwa mwombaji, ina maana na kuomba kwako
kutakuwa kwa matatizo.
“Lakini
akiiona ahadi ya Mungu hakusita kwa kutokuamini, bali alitiwa nguvu kwa Imani,
akimtukuza Mungu; huku akijua ya kuwa Mungu aweza kufanya yale aliyoahidi”.
(Warumi 4:20,21).
JAMBO LA 6: Je, umepita au unapita
kwenye taabu maishani mwako, kiasi kwamba huwezi kuomba, kwa sababu nafsi yako
imakataa kufarijika?
Daudi
aliwahi kukumbana na tatizo kama hili maana anatuambia hivi: “Siku ya taabu
yangu nalimtafuta Bwana, mkono wangu ulinyoshwa usiku, haukulegea, nafsi yangu
ilikataa kufarijika. Nilipotaka kumkumbuka Mungu nalifadhaika, nilipotaka
kutafakari roho yangu ilizimia. Ulizishika kope za macho yangu zisifumbike,
naliona mashaka nisiweze kunena” (Zaburi 77:2-4). Ni wazi kwamba taabu
alizokuwa anapitia Daudi, ziliumiza nafsi yake, na nafsi yake ikakataa
kufarijika, na mwisho wake alishindwa kuomba.
MAOMI A MAOMEZI
WASILIANA NA MCHUNGAJI LAURENT MPOMA
SIMU: +255762756542
WATSAP: +255762756542
YOUTUBU : Upenyo wa Mungu Tv
0 Comments