Follow us

SOMO:LAANA NI NINI? NA NINI MADHARA YAKE

Tangazo

 


SOMO: LAANA NI NINI? NA NINI MADHARA YAKE

Laana ni nini?

Laana ni ukosefu wa radhi za MUNGU katika jambo fulani.

Radhi ni nini?

Radhi ni msamaha.

Hivyo laana ni ukosefu wa msamaha wa MUNGU katika jambo fulani.

Hiyo ni maana ya kwanza ya laana.

Maana ya pili ya laana.

Laana ni nini?

Laana ni apizo alitoalo mtu kwa mtu mwingine ili afikwe na mabaya?

Wakristo wengi hujitanganya kwamba hawana laana kwa sababu wamewakombolewa kutoka kwenye laana ya torati.

Wagalatia 3:13-14 '' KRISTO  alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti;

ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika YESU KRISTO, tupate kupokea ahadi ya ROHO  kwa njia ya imani.''

Hiyo haina maana kwamba tufanye maovu yanayoleta laana tukijifariji kwamba tumekombelewa kutoka laana ya torati.

Aliyekuambia kwamba torati kazi yake ni kulaani ni nani?

Biblia hapo imeweka wazi kwamba tumekombolewa na laana ya torati ILI BARAKA YA IBRAHIMU AMBAYO MWANZO ILIKUWA NI YA WAISRAELI PEKEYAO, SASA KWA NJIA YA KRISTO YESU BARAKA HIYO INAHUSU WATU WOTE WALIOKOMBOLEWA KWA DAMU YA YESU KRISTO.

Jambo la kujua ni kwamba tumekombolewa kutoka laana ya kutengwa na MUNGU na sasa kwa njia ya KRISTO tunatambuliwa na MUNGU kama warithi sawasawa na ahadi aliyopewa Ibrahimu kwa wanaye.

Wagalatia 3:26-29 '' Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa MUNGU  kwa njia ya imani katika KRISTO YESU . Maana ninyi nyote mliobatizwa katika KRISTO  mmemvaa KRISTO. Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala huru. Hapana mtu mume wala mtu mke. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika KRISTO. Na kama ninyi ni wa KRISTO, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.''

Kumbe kabla ya Bwana YESU kutuokoa hatukuwa uzao wa Ibrahimu na hiyo ilikuwa ni laana lakini wana YESU ametufanya sisi kuwa uzao wa Ibrahimu warithi sawasawa na ahadi aliyoapiwa Ibrahimu na MUNGU.

Laana ilipofutika tulihesabiwa haki kama Ibrahimu alivyohesabiwa haki kwa kumwamini MUNGU.

Leo andiko la Wagalatia 3:13 wakristo wengi hulitumia kuonyesha kwamba hawana laana lakini wakati mwingine maisha yao yana laana.

Kuna laana ambazo hutolewa na wanadamu kama maapizo, ndio maana ya pili ya laana na laana hizo zimewakamata wengi kwa sababu hawaombi na hawajui haki zao kwa MUNGU, Wameteswa sana na laana hizo huku wakijifariji kwamba wamekombolewa kutoka laana.

Ndugu zangu ni muhimu kujua kwamba YESU anaweza kukutenga na laana lakini hadi ukiamua wewe kumwita, usipomwita utabaki na laana yako.

Kuna mambo umeyaona kwenye ndoto au maono yakionyesha wachawi au wakuu wa giza wanakulaani, Usipoomba hakika laana hiyo itakupata huku wewe ukibaki kujifariji kwamba umekombolewa kutoka laana.

YESU alisemea ''Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa-Luka 18:1''

Kama huombi hakika laana inaweza kukupata na kukutesa huku ukiendelea kujifariji.

Ndugu mmoja alilaaniwa kwamba  hataolewa, ilipita miaka mingi hadi alipojua kuombea kufuta laana hiyo ndipo aliolewa.

Watumishi wengi kwa sababu labda hawajawahi kupitia laana ndio maana hufundisha kwamba hakuna laana.

Wengine husema kwamba agano jipya halijazungumzia laana lakini wanasahau kwamba Bwana YESU alisema kwamba wenye laana ya MUNGU wataenda jehanamu.

Mathayo 25:41 '' Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;''

>>>LAANA KUTOKA KWA MUNGU INATENGENEZWA NA DHAMBI USIZOTUBIA HADI KIFO CHAKO.

Kumb 28:20 '' BWANA  atakuletea laana na mashaka, na kukemewa, katika yote utakayotia mkono wako kuyafanya, hata uangamie na kupotea kwa upesi; kwa ule uovu wa matendo yako, uliyoniacha kwayo.''

=>> LAANA YA MUNGU PIA UNAWEZA UKAIPATA KWA SABABU YA KUTOKUTOA FUNGU LA KUMI.

Malaki 3:9 '' Ninyi mmelaaniwa kwa laana; maana mnaniibia mimi, naam, taifa hili lote.''

Kutokutoa zaka kamili ni kumwibia MUNGU na jambo hilo hutengeneza laana.

Wengi hawatoi fungu la kumi wakisingizia kwamba wamekombolewa kutoka laana ya torati wakati Fungu la kumi lipo kabla ya torati. Akina Ibarahimu walitoa Fungu la kumi kwa akina Melkizedeki kipindi ambacho hata torati hajapewa Musa.

Akina Yakobo walitoa Fungu la kumi kabla hata Waisraeli hawajaenda utumwani Misri.

Mathayo 25:41 kwamba waliolaaniwa na MUNGU watakwenda jehanamu huwa naogopa sana.

Njia ya mbinguni ni nyembamba ndio maana hata kwa zaka tu watu hupishana na njia hiyo ya uzima.

Laana za wanadamu au majini au wakuu wa giza haziwezi kumfanya mtu asiende uzima wa milele lakini laana kutoka kwa MUNGU inaweza kumfanya mtu asiende uzima wa milele.

Laana kutoka kwa wanadamu na mawakala wa shetani zinaweza kusababisha ukateseka katika maisha ya duniani, hivyo ukihisi kuna laana inakufuatilia iwe ni kutoka kwa babu au bibi au mama au baba au mjomba au shangazi au kaka au dada au mtoto wako hakikisha tu unatubu kwa sababu ya kisababishi cha laana hiyo kisha ifute laana hiyo kwa maombi katika jina la YESU KRISTO.

Laana ni jambo baya sana.

Hata makosa ya akina adamu hayakumfanya MUNGU awalaani bali aliilaani ardhi na sio wao.

Je ni lini uliiombea ardhi yao iliyolaaniwa ili laana iondoke kwa damu ya YESU na ufaidike na mazao yanayotokana na ardhi yako?

Bwana YESU analifundisha kanisa lake kupitia Mtume Paulo akisema tusiwe watu wa kulaani watu wengine, ni heri tuwabariki na sio kuwalaani, kuna madhara makubwa yanayotokana na laana hivyo ni heri kubariki tu.

Warumi 12:14-17 '' Wabarikini wanaowaudhi; barikini, wala msilaani. Furahini pamoja nao wafurahio; lieni pamoja nao waliao. Mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi. Msinie yaliyo makuu, lakini mkubali kushughulishwa na mambo manyonge. Msiwe watu wa kujivunia akili.Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote.''

Laana ni kitu kinachokukamata ili usifanikiwe kwenye jambo fulani maishani mwako.

Hakikisha laana inaondoka maishani mwako.

Kama ni laana kutoka kwa MUNGU tubu na acha uovu huo kwa kuanza kutenda mema ayatakayo MUNGU.

ZINGATIA HIYO ITAKUSAIDIA.

Biblia inasema mtu akilaani mjini basi hata mashambani yaani kijijini atakuwa amelaani.

Kama unasumbuliwa na laana unaweza ukajaribu kufanya biashara mjini lakini hufanikiwi. Baadaea unaweza ukajaribu kwenda kijijini labda huko utafanikiwa, kwa sababu ya laana iliyo juu yako hakika hata kijijini hutafanikiwa.

Kuna watu hukimbilia mijini labda wakidhani huko watafanikiwa lakini kama laana inawasumbua hakika hata waende wapi hawatafanikiwa.

Kumb. La torati  28:16 ''Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani.''

Dawa ya kuondoa laana sio kuhama eneo bali ni kutubu na kutengeneza kwa KRISTO YESU Mfalme wa uzima.

UNATAKA KUJIJUA KAMA UNA LAANA?

Kumb 28 itatujibu.

MTU MWENYE LAANA YUKO HIVI;

1. Hata ahamie eneo jingine lolote hatafanikiwa.

Kumbukumbu la torati 28:16 ''Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani. ''

2. Chanzo chake cha kipato hakimpi faida yeyote.

Kumbukumbu  la torati  28:17 '' Litalaaniwa kapu lako na chombo chako cha kukandia.''

3. Uzao wake unakuwa chini ya laana na pia  Biashara au mradi anaoanzisha hafanikiwi kwa sababu viko chini ya laana

Kumbukumbu la torati 28:18 ''Utalaaniwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, maongeo ya ng'ombe wako, na wadogo wa kondoo zako. ''

4. Kwa kosa la kumkosea MUNGU basi mtu huyo atakuwa mtu wa kuwa na mashaka mashaka, hukemewa, Kudhalilishwa na kutishwa bila kosa kwa sababu ya laana aliyonayo.

Kumbukumbu la torati 28:19-20 '' Utalaaniwa uingiapo, utalaaniwa na utokapo, BWANA atakuletea laana na mashaka, na kukemewa, katika yote utakayotia mkono wako kuyafanya, hata uangamie na kupotea kwa upesi; kwa ule uovu wa matendo yako, uliyoniacha kwayo.''

5. Kwa Kumkosea MUNGU basi Laana yake inaweza kutengeneza magonjwa mabaya.

Kumbukumbu la torati  28:22 ''BWANA atakupiga kwa kifua kikuu, na kwa homa, na kwa kuwashwa, na kwa hari ya moto, na kwa upanga, na kwa ukaufu, na kwa koga; navyo vitakufukuza hata uangamie.''

6. Kufungwa kwa baraka kutoka kwa MUNGU.

Kumb 28:23 ''Na mbingu zako zilizo juu ya kichwa chako zitakuwa shaba, na nchi iliyo chini yako itakuwa chuma.''

7. Kwa kumkosea MUNGU basi Mazuri anayoyatarajia yatageuka kuwa mabaya

Kumbukumbu la torati  28:24 '' BWANA  atafanya mvua ya nchi yako iwe vumbi na mchanga; itakujilia juu yako kutoka mbinguni hata uangamie.''

8. Kwa Kumkosea MUNGU basi Adui kwenye ulimwengu wa roho watampiga.

Kumbukumbu la torati  28:25 '' BWANA atakufanya upigwe mbele ya adui zako; utawatokea juu yao kwa njia moja, lakini utakimbia mbele yao kwa njia saba; nawe utatupwa huko na huko katika falme zote za duniani.''

9. Atakuwa mtu wa kuonewa.

Kumbukumbu la torati  28:29 ''  utakwenda kwa kupapasa-papasa mchana, kama apapasavyo kipofu gizani, wala hufanikiwi katika njia zako; nawe sikuzote utaonewa na kutekwa nyara, wala hapatakuwa na mtu wa kukuokoa.''

10.  Kupata Hasara zisizoisha.

Kumbukumbu la torati  28:38-39 '' Mbegu nyingi utazichukua nje shambani, lakini utavuna haba, kwa kuwa nzige watazila. Utapanda mizabibu na kuitengeza, wala hutakunywa katika divai yake, wala kuichuma kwani italiwa na mabuu.''

11. Wageni au watu wapya wakija wanafanikiwa lakini yeye yuko pale pale, Pia atateswa na madeni

Kumbukumbu la torati  28:43-44 '' Mgeni aliye kati yako atazidi kupaa juu yako; nawe utazidi kushuka chini.Yeye atakukopesha, wala wewe usimkopeshe; yeye atakuwa ni kichwa, wewe utakuwa mkia. ''

12. Akipata mali au pesa wanatokea walaji ili asifanye chochote cha kimaendeleo.

Kumbukumbu la torati  28:50-51 ''taifa lenye uso mkali, ambalo haliangalii uso wa mzee, wala halipendelei kijana; naye atakula uzao wa ng'ombe wako wa mifugo, na uzao wa nchi yako mpaka utakapokwisha kuangamizwa;''

Hizi ni alama chache tu za mtu anayesumbuliwa na laana.

Ndugu yangu ni muhimu kujua kwamba damu ya YESU inaweza kufuta laana zote lakini ni mpaka uombe na sio kujifariji tu.

Kanuni ya laana ni kwamba mkubwa anamlaani mdogo hivyo na kuondoka laana kunahitajika nguvu kubwa kuliko mtoa laana wa kidunia.

Kama laana imetoka kwa MUNGU basi dawa ni kutubu tu kwa MUNGU na kutengeneza njia zako kwa kuanza kutenda yale ayatayo MUNGU.

YESU KRISTO ana uwezo wa kukuweka huru kweli kweli mbali na laana, lakini hadi uamue wewe kuwekwa huru.

Yohana 8:36 '' Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli.''

Ewe mteule wa MUNGU nakuomba Mche MUNGU na timiza utakatifu wako kwa kumtii MUNGU hata katika matoleo.

Pia usitumie ulimi wako kulaani watu wa MUNGU bali laani shetani na jeshi lake.

Yakobo 3:9-10 ''Kwa huo(Ulimi) twamhimidi MUNGU  Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa MUNGU.

Laana ni nini?

Laana ni ukosefu wa radhi za MUNGU katika jambo fulani.

Radhi ni nini?

Radhi ni msamaha.

Hivyo laana ni ukosefu wa msamaha wa MUNGU katika jambo fulani.

Hiyo ni maana ya kwanza ya laana.

Maana ya pili ya laana.

Laana ni nini?

Laana ni apizo alitoalo mtu kwa mtu mwingine ili afikwe na mabaya?

Wakristo wengi hujitanganya kwamba hawana laana kwa sababu wamewakombolewa kutoka kwenye laana ya torati.

Wagalatia 3:13-14 '' KRISTO  alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti;

ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika YESU KRISTO, tupate kupokea ahadi ya ROHO  kwa njia ya imani.''

Hiyo haina maana kwamba tufanye maovu yanayoleta laana tukijifariji kwamba tumekombelewa kutoka laana ya torati.

Aliyekuambia kwamba torati kazi yake ni kulaani ni nani?

Biblia hapo imeweka wazi kwamba tumekombolewa na laana ya torati ILI BARAKA YA IBRAHIMU AMBAYO MWANZO ILIKUWA NI YA WAISRAELI PEKEYAO, SASA KWA NJIA YA KRISTO YESU BARAKA HIYO INAHUSU WATU WOTE WALIOKOMBOLEWA KWA DAMU YA YESU KRISTO.

Jambo la kujua ni kwamba tumekombolewa kutoka laana ya kutengwa na MUNGU na sasa kwa njia ya KRISTO tunatambuliwa na MUNGU kama warithi sawasawa na ahadi aliyopewa Ibrahimu kwa wanaye.

Wagalatia 3:26-29 '' Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa MUNGU  kwa njia ya imani katika KRISTO YESU . Maana ninyi nyote mliobatizwa katika KRISTO  mmemvaa KRISTO. Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala huru. Hapana mtu mume wala mtu mke. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika KRISTO. Na kama ninyi ni wa KRISTO, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.''

Kumbe kabla ya Bwana YESU kutuokoa hatukuwa uzao wa Ibrahimu na hiyo ilikuwa ni laana lakini wana YESU ametufanya sisi kuwa uzao wa Ibrahimu warithi sawasawa na ahadi aliyoapiwa Ibrahimu na MUNGU.

Laana ilipofutika tulihesabiwa haki kama Ibrahimu alivyohesabiwa haki kwa kumwamini MUNGU.

Leo andiko la Wagalatia 3:13 wakristo wengi hulitumia kuonyesha kwamba hawana laana lakini wakati mwingine maisha yao yana laana.

Kuna laana ambazo hutolewa na wanadamu kama maapizo, ndio maana ya pili ya laana na laana hizo zimewakamata wengi kwa sababu hawaombi na hawajui haki zao kwa MUNGU, Wameteswa sana na laana hizo huku wakijifariji kwamba wamekombolewa kutoka laana.

Ndugu zangu ni muhimu kujua kwamba YESU anaweza kukutenga na laana lakini hadi ukiamua wewe kumwita, usipomwita utabaki na laana yako.

Kuna mambo umeyaona kwenye ndoto au maono yakionyesha wachawi au wakuu wa giza wanakulaani, Usipoomba hakika laana hiyo itakupata huku wewe ukibaki kujifariji kwamba umekombolewa kutoka laana.

YESU alisemea ''Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa-Luka 18:1''

Kama huombi hakika laana inaweza kukupata na kukutesa huku ukiendelea kujifariji.

Ndugu mmoja alilaaniwa kwamba  hataolewa, ilipita miaka mingi hadi alipojua kuombea kufuta laana hiyo ndipo aliolewa.

Watumishi wengi kwa sababu labda hawajawahi kupitia laana ndio maana hufundisha kwamba hakuna laana.

Wengine husema kwamba agano jipya halijazungumzia laana lakini wanasahau kwamba Bwana YESU alisema kwamba wenye laana ya MUNGU wataenda jehanamu.

Mathayo 25:41 '' Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;''

>>>LAANA KUTOKA KWA MUNGU INATENGENEZWA NA DHAMBI USIZOTUBIA HADI KIFO CHAKO.

Kumb 28:20 '' BWANA  atakuletea laana na mashaka, na kukemewa, katika yote utakayotia mkono wako kuyafanya, hata uangamie na kupotea kwa upesi; kwa ule uovu wa matendo yako, uliyoniacha kwayo.''

=>> LAANA YA MUNGU PIA UNAWEZA UKAIPATA KWA SABABU YA KUTOKUTOA FUNGU LA KUMI.

Malaki 3:9 '' Ninyi mmelaaniwa kwa laana; maana mnaniibia mimi, naam, taifa hili lote.''

Kutokutoa zaka kamili ni kumwibia MUNGU na jambo hilo hutengeneza laana.

Wengi hawatoi fungu la kumi wakisingizia kwamba wamekombolewa kutoka laana ya torati wakati Fungu la kumi lipo kabla ya torati. Akina Ibarahimu walitoa Fungu la kumi kwa akina Melkizedeki kipindi ambacho hata torati hajapewa Musa.

Akina Yakobo walitoa Fungu la kumi kabla hata Waisraeli hawajaenda utumwani Misri.

Mathayo 25:41 kwamba waliolaaniwa na MUNGU watakwenda jehanamu huwa naogopa sana.

Njia ya mbinguni ni nyembamba ndio maana hata kwa zaka tu watu hupishana na njia hiyo ya uzima.

Laana za wanadamu au majini au wakuu wa giza haziwezi kumfanya mtu asiende uzima wa milele lakini laana kutoka kwa MUNGU inaweza kumfanya mtu asiende uzima wa milele.

Laana kutoka kwa wanadamu na mawakala wa shetani zinaweza kusababisha ukateseka katika maisha ya duniani, hivyo ukihisi kuna laana inakufuatilia iwe ni kutoka kwa babu au bibi au mama au baba au mjomba au shangazi au kaka au dada au mtoto wako hakikisha tu unatubu kwa sababu ya kisababishi cha laana hiyo kisha ifute laana hiyo kwa maombi katika jina la YESU KRISTO.

Laana ni jambo baya sana.

Hata makosa ya akina adamu hayakumfanya MUNGU awalaani bali aliilaani ardhi na sio wao.

Je ni lini uliiombea ardhi yao iliyolaaniwa ili laana iondoke kwa damu ya YESU na ufaidike na mazao yanayotokana na ardhi yako?

Bwana YESU analifundisha kanisa lake kupitia Mtume Paulo akisema tusiwe watu wa kulaani watu wengine, ni heri tuwabariki na sio kuwalaani, kuna madhara makubwa yanayotokana na laana hivyo ni heri kubariki tu.

Warumi 12:14-17 '' Wabarikini wanaowaudhi; barikini, wala msilaani. Furahini pamoja nao wafurahio; lieni pamoja nao waliao. Mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi. Msinie yaliyo makuu, lakini mkubali kushughulishwa na mambo manyonge. Msiwe watu wa kujivunia akili.Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote.''

Laana ni kitu kinachokukamata ili usifanikiwe kwenye jambo fulani maishani mwako.

Hakikisha laana inaondoka maishani mwako.

Kama ni laana kutoka kwa MUNGU tubu na acha uovu huo kwa kuanza kutenda mema ayatakayo MUNGU.

ZINGATIA HIYO ITAKUSAIDIA.

Biblia inasema mtu akilaani mjini basi hata mashambani yaani kijijini atakuwa amelaani.

Kama unasumbuliwa na laana unaweza ukajaribu kufanya biashara mjini lakini hufanikiwi. Baadaea unaweza ukajaribu kwenda kijijini labda huko utafanikiwa, kwa sababu ya laana iliyo juu yako hakika hata kijijini hutafanikiwa.

Kuna watu hukimbilia mijini labda wakidhani huko watafanikiwa lakini kama laana inawasumbua hakika hata waende wapi hawatafanikiwa.

Kumb. La torati  28:16 ''Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani.''

Dawa ya kuondoa laana sio kuhama eneo bali ni kutubu na kutengeneza kwa KRISTO YESU Mfalme wa uzima.

UNATAKA KUJIJUA KAMA UNA LAANA?

Kumb 28 itatujibu.

MTU MWENYE LAANA YUKO HIVI;

1. Hata ahamie eneo jingine lolote hatafanikiwa.

Kumbukumbu la torati 28:16 ''Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani. ''

2. Chanzo chake cha kipato hakimpi faida yeyote.

Kumbukumbu  la torati  28:17 '' Litalaaniwa kapu lako na chombo chako cha kukandia.''

3. Uzao wake unakuwa chini ya laana na pia  Biashara au mradi anaoanzisha hafanikiwi kwa sababu viko chini ya laana

Kumbukumbu la torati 28:18 ''Utalaaniwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, maongeo ya ng'ombe wako, na wadogo wa kondoo zako. ''

4. Kwa kosa la kumkosea MUNGU basi mtu huyo atakuwa mtu wa kuwa na mashaka mashaka, hukemewa, Kudhalilishwa na kutishwa bila kosa kwa sababu ya laana aliyonayo.

Kumbukumbu la torati 28:19-20 '' Utalaaniwa uingiapo, utalaaniwa na utokapo, BWANA atakuletea laana na mashaka, na kukemewa, katika yote utakayotia mkono wako kuyafanya, hata uangamie na kupotea kwa upesi; kwa ule uovu wa matendo yako, uliyoniacha kwayo.''

5. Kwa Kumkosea MUNGU basi Laana yake inaweza kutengeneza magonjwa mabaya.

Kumbukumbu la torati  28:22 ''BWANA atakupiga kwa kifua kikuu, na kwa homa, na kwa kuwashwa, na kwa hari ya moto, na kwa upanga, na kwa ukaufu, na kwa koga; navyo vitakufukuza hata uangamie.''

6. Kufungwa kwa baraka kutoka kwa MUNGU.

Kumb 28:23 ''Na mbingu zako zilizo juu ya kichwa chako zitakuwa shaba, na nchi iliyo chini yako itakuwa chuma.''

7. Kwa kumkosea MUNGU basi Mazuri anayoyatarajia yatageuka kuwa mabaya

Kumbukumbu la torati  28:24 '' BWANA  atafanya mvua ya nchi yako iwe vumbi na mchanga; itakujilia juu yako kutoka mbinguni hata uangamie.''

8. Kwa Kumkosea MUNGU basi Adui kwenye ulimwengu wa roho watampiga.

Kumbukumbu la torati  28:25 '' BWANA atakufanya upigwe mbele ya adui zako; utawatokea juu yao kwa njia moja, lakini utakimbia mbele yao kwa njia saba; nawe utatupwa huko na huko katika falme zote za duniani.''

9. Atakuwa mtu wa kuonewa.

Kumbukumbu la torati  28:29 ''  utakwenda kwa kupapasa-papasa mchana, kama apapasavyo kipofu gizani, wala hufanikiwi katika njia zako; nawe sikuzote utaonewa na kutekwa nyara, wala hapatakuwa na mtu wa kukuokoa.''

10.  Kupata Hasara zisizoisha.

Kumbukumbu la torati  28:38-39 '' Mbegu nyingi utazichukua nje shambani, lakini utavuna haba, kwa kuwa nzige watazila. Utapanda mizabibu na kuitengeza, wala hutakunywa katika divai yake, wala kuichuma kwani italiwa na mabuu.''

11. Wageni au watu wapya wakija wanafanikiwa lakini yeye yuko pale pale, Pia atateswa na madeni

Kumbukumbu la torati  28:43-44 '' Mgeni aliye kati yako atazidi kupaa juu yako; nawe utazidi kushuka chini.Yeye atakukopesha, wala wewe usimkopeshe; yeye atakuwa ni kichwa, wewe utakuwa mkia. ''

12. Akipata mali au pesa wanatokea walaji ili asifanye chochote cha kimaendeleo.

Kumbukumbu la torati  28:50-51 ''taifa lenye uso mkali, ambalo haliangalii uso wa mzee, wala halipendelei kijana; naye atakula uzao wa ng'ombe wako wa mifugo, na uzao wa nchi yako mpaka utakapokwisha kuangamizwa;''

Hizi ni alama chache tu za mtu anayesumbuliwa na laana.

Ndugu yangu ni muhimu kujua kwamba damu ya YESU inaweza kufuta laana zote lakini ni mpaka uombe na sio kujifariji tu.

Kanuni ya laana ni kwamba mkubwa anamlaani mdogo hivyo na kuondoka laana kunahitajika nguvu kubwa kuliko mtoa laana wa kidunia.

Kama laana imetoka kwa MUNGU basi dawa ni kutubu tu kwa MUNGU na kutengeneza njia zako kwa kuanza kutenda yale ayatayo MUNGU.

YESU KRISTO ana uwezo wa kukuweka huru kweli kweli mbali na laana, lakini hadi uamue wewe kuwekwa huru.

Yohana 8:36 '' Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli.''

Ewe mteule wa MUNGU nakuomba Mche MUNGU na timiza utakatifu wako kwa kumtii MUNGU hata katika matoleo.

Pia usitumie ulimi wako kulaani watu wa MUNGU bali laani shetani na jeshi lake.

Yakobo 3:9-10 ''Kwa huo(Ulimi) twamhimidi MUNGU  Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa MUNGU.


<<<<<MUNGU AKUBARIKI SANA KWA KUJIFUNZA MANENO YA MUNGU>>>>>>>>>>

SOMA UJUMBE HUU NI MUHIMU SANA KATIKA MAISHA YAKO LEO ILI MUNGU AKUPANDISHE VIWANGO VYA JUU.

2 Mambo ya Nyakati 1:7-12

Usiku ule Mungu akamtokea Sulemani, akamwambia, Omba utakalo nikupe. Sulemani akamwambia Mungu, Umemfanyia baba yangu Daudi fadhili kuu, nawe umenimilikisha mimi badala yake. Basi sasa, Ee BWANA Mungu, na limyakinie baba yangu Daudi neno lako; maana umenitawaza niwe mfalme juu ya watu wengi kama mavumbi ya nchi. Basi sasa nipe hekima na maarifa, nijue kutoka na kuingia mbele ya watu hawa; kwa kuwa ni nani awezaye kuwatawala watu wako hawa walio wengi? Naye Mungu akamwambia Sulemani, Kwa sababu neno hili lilikuwamo moyoni mwako, wala hukujitakia mali, wala utajiri, wala utukufu, wala maisha ya wakuchukiao, wala hukujitakia maisha ya siku nyingi; bali umejitakia hekima na maarifa, upate kuwatawala watu wangu, niliokutawaza juu yao; basi hekima na maarifa umepewa; nami nitakupa mali, na utajiri, na utukufu, kupita walivyokuwa navyo wafalme wote waliokuwa kabla yako, wala baada yako hapatakuwa na mtu atakayekuwa navyo.

>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>

KANISA LA ELIM PENTEKOSTE NCHI YA UKOMBOZI- MUHAWA SINGIDA MJINI.

(NENO, MAOMBI NA MAOMBEZI)

Tuna ununuzi wa vifaa kwa ajili ya Mkutano wa Injili. Unaweza kuchangia kwa ajili ya kuhubiri injili na Mungu atakutana na wewe na kuzungumza na wewe na atatenda mambo makubwa sana kwenye maisha yako kuanzia leo.

TUNAHITAJI KUNUNUA.

1. VITAMBAA VYA MADHABAHU........TSHS, 60000/=

2.MAIKI WIRELESS....4......TSHS, 240,000/=

3. MAIKI ZA WIRE......4.......TSHS, 100,000/=

4. TRUBAI...........4..........TSHS, 60,000/=

5. MABATI  20@ 27,000......JUMLA NI TSHS, 540,000/=

6. DRAMS......1........TSHS, 1,100,000/=

7.SPEAKER FIDEK 3......TSHS, 2,100,000/=

WASILIANA NA MCHUNGAJI ILI MCHUNGAJI AKUOMBEE PAPO HAPO UTAKAPOCHANGIA KIMOJA WAPO KATI YA HIVYO HAPO JUU AU CHOCHOTE ULICHO NACHO TUNAPOKEA.

MUNGU AKUBARIKI SANA, AKUFUNGUE KWENYE HILO UNALOPITIA, MUNGU AKUINUE KATIKA FAMILIA, UCHUMI, KAZI NA MENGINEYO UNAYOHITAJI KATIKA MOYO WAKO.

NAMBA ZINAZOTUMIKA KATIKA MCHANGO NI NAMBA ZA MCHUNGAJI TU.

1. M-PESA  0762756542.....JINA: LAURENT MPOMA

2. AIRTEL MONEY: 0782859946....JINA: LAURENT MPOMA

3: TIGO PESA: 0714890889.....JINA : LAURENT MPOMA

KABLA YA KUTUMA WASILIANA NA MCHUNGAJI KWA NAMBA HIZO.

MCHUNGAJI ATAFANYA MAOMBI KWA AJILI YAKO.

>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>

KWA MSAADA ZAIDI NA MAOMBEZI:

WASILIANA NA MCHUNGAJI AU

FIKA KANISANI,

KANISA LA ELIM PENTEKOSTE NCHI YA UKOMBOZI

(NENO, MAOMBI NA MAOMBEZI)

AU WASILIANA NASI KUPITIA

FACEBOOK: nchi ya ukombozi ministry

Follow us on YOUTUBE: Upenyo Wa Mungu Tv

TELEPHONE: +255762756542

WHATSAP: +255762756542

BLOG: NCHI YA UKOMBOZI MINISTRY

http:// nchiyaukomboziministrytz.blogspot.com/


MUNGU AKUBARIKI SANA KWA KUJIFUNZA MANENO YA MUNGU.

 

Post a Comment

0 Comments