SOMO: MAOMBI YA KUTENGUA VIAPO
Kiapo kinaweza kumfunga mtu kwa lile jambo
aliloliapia. Watu wengi maisha yao yameharibika kwasababu ya kutokutimiza viapo
vyao walivyoapa.
wachawi ni
binadamu kama wewe lakini nao huapa. Huloga watu hatakama hawapendi kwasababu
ya viapo vya uchawi walivyoapa leo tunajifunza maana ya kiapo na nguvu zake
baadae tunakwenda kuomba kwa jina la Yesu.
Kiapo ni
maneno yaliyotamkwa yanayoweza kuleta laana juu ya mtu au familia.
Yoshua 6:26-27 “Naye Yoshua akawaapisha kiapo wakati
ule, akasema, Na alaaniwe mbele za Bwana mtu yule atakayeinuka na kuujenga tena
mji huu wa Yeriko; ataweka msingi wake kwa kufiliwa na mzaliwa wa kwanza wake,
tena atayasimamisha malango yake kwa kufiliwa na mtoto wake mwanamume aliye
mdogo.Basi Bwana alikuwa pamoja na Yoshua; sifa zake zikaenea katika nchi ile
yote.”
Siku hizi
utakuta familia kila mwaka anakufa mtu maana yake kuna viapo vya kifamilia.
Ukirudi nyuma miaka ya nyuma tulikua hatumjui Mungu hivyo wazazi wetu walikua
wanafanya viapo kwa miungu na mashetani, viapo vile vimefata familia zetu mpaja
leo hii.
1 Wafalme 16:30-34 “Ahabu mwana wa Omri akafanya yaliyo
mabaya machoni pa Bwana kuliko wote waliomtangulia.Ikawa, kama ingalikuwa neno
dogo tu kuyaendea makosa ya Yeroboamu mwana wa Nebati, akamwoa Yezebeli binti
Ethbaali, mfalme wa Wasidoni, akaenda akamtumikia Baali, akamsujudia.Akamjengea
Baali madhabahu katika nyumba ya Baali, aliyoijenga huko Samaria.Ahabu
akaifanya Ashera; Ahabu akazidi kumghadhibisha Bwana, Mungu wa Israeli, kuliko
wafalme wote wa Israeli waliomtangulia.Katika siku zake, Hieli Mbetheli
akajenga Yeriko; akatia misingi yake kwa kufiwa na Abiramu mzaliwa wake wa
kwanza, na kuyaweka malango yake kwa kufiwa na mwana wake mdogo Segubu;
sawasawa na neno la Bwana alilolinena kwa Yoshua mwana wa Nuni.”
Kiapo ni
maneno mamlaka ya mwisho ya kutoa. Unapomuona mtu amefikia kwenye kiapo maana
yake ni mamlaka yake ya mwisho inambidi aape kwanza ndio aanze jambo fulani,
hapa watu wengi wameshikiliwa.
Unakuta mtu
analambabudongo anaapa au anaapa “haki ya Mungu kabisa nakuapia” na baadae
hatimizi lile alilosema ndipo matatizo yanaanza kumpata. Mtu anatoa kiapo ili
aeleweke, akubalike au afahamike kwa wakati ule.
Kama
ulimwengu huu wa mwili unavyoongozwa na sheria ndivyo na kwenye ulimwengu wa
roho unaongozwa na sheria. Sheria hizi sio kwamba zinamgandamiza mtu hapana
bali zimewekwa ili kumlinda.
Mfano sheria
za barabarani zimewekwa ili uwe mwangalifu usipatwe na ajali, wewe ukisema
“mimi ni mtaalam na uzoefu Roho wa Bwana atanilinda ntalala na mia, ninaharaka,
nataka niwahi” utajikuta umewahi mbinguni kama umeokoka au jehanam kama
hujaokoka.
Biblia
inasema mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi mkikataa mtaangamizwa kwa
upanga. Unapojiingiza kwenye kiapo uwe inajua au hujui mashetani yanakukamata
yanaangalia jambo gani likupate sababu umeapa au kuna mtu ameapa mambo fulani
yakupate.
Mungu
akitaka kufanya jambo na mtu anaapa kwamba anachokisema lazima kitatimia.
Isaya 45:22-23 “Niangalieni mimi, mkaokolewe, enyi
ncha zote za dunia; maana mimi ni Mungu; hapana mwingine.Kwa nafsi yangu
nimeapa, neno hili limetoka kinywani mwangu katika haki, wala halitarudi, ya
kwamba mbele zangu kila goti litapigwa, kila ulimi utaapa.”
Waebrania 6:13-16 “Kwa maana Mungu, alipompa Ibrahimu
ahadi, kwa sababu alikuwa hana mkubwa kuliko yeye mwenyewe wa kumwapa, aliapa
kwa nafsi yake,akisema, Hakika yangu kubariki nitakubariki, na kuongeza
nitakuongeza.Na hivyo kwa kuvumilia akaipata ile ahadi.Maana wanadamu huapa kwa
yeye aliye mkuu kuliko wao; na kwao ukomo wa mashindano yote ya maneno ni
kiapo, kwa kuyathibitisha.”
Uharibifu
huletwa ndani ya kiapo ikiwa aliyeapa kutenda jambo fulani hajalitimiza. Leo
hii kuna viapo vinawasumbua watu na wengibe hawajui wanateseka kwasababu ya
viapo flani walivyofanya.
UKIRI
Kila kiapo
kilichofanywa juu yangu ili kuniletea uharibifu nakisambaratisha kwa jina la
Yesu Amen
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
KANISA LA
ELIM PENTEKOSTE NCHI YA UKOMBOZI- MUHAWA SINGIDA MJINI.
(NENO,
MAOMBI NA MAOMBEZI)
Tuna ununuzi
wa vifaa kwa ajili ya Mkutano wa Injili. Unaweza kuchangia kwa ajili ya
kuhubiri injili na Mungu atakutana na wewe na kuzungumza na wewe na atatenda
mambo makubwa sana kwenye maisha yako kuanzia leo.
TUNAHITAJI
KUNUNUA.
1. VITAMBAA
VYA MADHABAHU........TSHS, 60000/=
2.MAIKI
WIRELESS....4......TSHS, 240,000/=
3. MAIKI ZA
WIRE......4.......TSHS, 100,000/=
4.
TRUBAI...........4..........TSHS, 60,000/=
5.
MABATI 20@ 27,000......JUMLA NI TSHS,
540,000/=
6.
DRAMS......1........TSHS, 1,100,000/=
7.SPEAKER
FIDEK 3......TSHS, 2,100,000/=
WASILIANA NA
MCHUNGAJI ILI MCHUNGAJI AKUOMBEE PAPO HAPO UTAKAPOCHANGIA KIMOJA WAPO KATI YA
HIVYO HAPO JUU AU CHOCHOTE ULICHO NACHO TUNAPOKEA.
MUNGU
AKUBARIKI SANA, AKUFUNGUE KWENYE HILO UNALOPITIA, MUNGU AKUINUE KATIKA FAMILIA,
UCHUMI, KAZI NA MENGINEYO UNAYOHITAJI KATIKA MOYO WAKO.
NAMBA
ZINAZOTUMIKA KATIKA MCHANGO NI NAMBA ZA MCHUNGAJI TU.
1.
M-PESA 0762756542.....JINA: LAURENT
MPOMA
2. AIRTEL
MONEY: 0782859946....JINA: LAURENT MPOMA
3: TIGO
PESA: 0714890889.....JINA : LAURENT MPOMA
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
KWA MSAADA
ZAIDI NA MAOMBEZI:
WASILIANA NA
MCHUNGAJI AU
FIKA
KANISANI,
KANISA LA
ELIM PENTEKOSTE NCHI YA UKOMBOZI
(NENO,
MAOMBI NA MAOMBEZI)
AU WASILIANA
NASI KUPITIA
FACEBOOK:
nchi ya ukombozi ministry
Follow us on
YOUTUBE: Upenyo Wa Mungu Tv
TELEPHONE:
+255762756542
WHATSAP:
+255762756542
BLOGSPOT:
NCHI YA UKOMBOZI MINISTRY
http://
nchiyaukomboziministrytz.blogspot.com/
MUNGU
AKUBARIKI SANA KWA KUJIFUNZA MANENO YA MUNGU.
0 Comments