Follow us

SOMO: MAOMBI YA KUTENGUA VIAPO

Tangazo


SOMO: MAOMBI YA KUTENGUA VIAPO

Kiapo kinaweza kumfunga mtu kwa lile jambo aliloliapia. Watu wengi maisha yao yameharibika kwasababu ya kutokutimiza viapo vyao walivyoapa.

wachawi ni binadamu kama wewe lakini nao huapa. Huloga watu hatakama hawapendi kwasababu ya viapo vya uchawi walivyoapa leo tunajifunza maana ya kiapo na nguvu zake baadae tunakwenda kuomba kwa jina la Yesu.

Kiapo ni maneno yaliyotamkwa yanayoweza kuleta laana juu ya mtu au familia.

Yoshua 6:26-27 “Naye Yoshua akawaapisha kiapo wakati ule, akasema, Na alaaniwe mbele za Bwana mtu yule atakayeinuka na kuujenga tena mji huu wa Yeriko; ataweka msingi wake kwa kufiliwa na mzaliwa wa kwanza wake, tena atayasimamisha malango yake kwa kufiliwa na mtoto wake mwanamume aliye mdogo.Basi Bwana alikuwa pamoja na Yoshua; sifa zake zikaenea katika nchi ile yote.”

Siku hizi utakuta familia kila mwaka anakufa mtu maana yake kuna viapo vya kifamilia. Ukirudi nyuma miaka ya nyuma tulikua hatumjui Mungu hivyo wazazi wetu walikua wanafanya viapo kwa miungu na mashetani, viapo vile vimefata familia zetu mpaja leo hii.

1 Wafalme 16:30-34 “Ahabu mwana wa Omri akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana kuliko wote waliomtangulia.Ikawa, kama ingalikuwa neno dogo tu kuyaendea makosa ya Yeroboamu mwana wa Nebati, akamwoa Yezebeli binti Ethbaali, mfalme wa Wasidoni, akaenda akamtumikia Baali, akamsujudia.Akamjengea Baali madhabahu katika nyumba ya Baali, aliyoijenga huko Samaria.Ahabu akaifanya Ashera; Ahabu akazidi kumghadhibisha Bwana, Mungu wa Israeli, kuliko wafalme wote wa Israeli waliomtangulia.Katika siku zake, Hieli Mbetheli akajenga Yeriko; akatia misingi yake kwa kufiwa na Abiramu mzaliwa wake wa kwanza, na kuyaweka malango yake kwa kufiwa na mwana wake mdogo Segubu; sawasawa na neno la Bwana alilolinena kwa Yoshua mwana wa Nuni.”

Kiapo ni maneno mamlaka ya mwisho ya kutoa. Unapomuona mtu amefikia kwenye kiapo maana yake ni mamlaka yake ya mwisho inambidi aape kwanza ndio aanze jambo fulani, hapa watu wengi wameshikiliwa.

Unakuta mtu analambabudongo anaapa au anaapa “haki ya Mungu kabisa nakuapia” na baadae hatimizi lile alilosema ndipo matatizo yanaanza kumpata. Mtu anatoa kiapo ili aeleweke, akubalike au afahamike kwa wakati ule.

Kama ulimwengu huu wa mwili unavyoongozwa na sheria ndivyo na kwenye ulimwengu wa roho unaongozwa na sheria. Sheria hizi sio kwamba zinamgandamiza mtu hapana bali zimewekwa ili kumlinda.

Mfano sheria za barabarani zimewekwa ili uwe mwangalifu usipatwe na ajali, wewe ukisema “mimi ni mtaalam na uzoefu Roho wa Bwana atanilinda ntalala na mia, ninaharaka, nataka niwahi” utajikuta umewahi mbinguni kama umeokoka au jehanam kama hujaokoka.

Biblia inasema mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi mkikataa mtaangamizwa kwa upanga. Unapojiingiza kwenye kiapo uwe inajua au hujui mashetani yanakukamata yanaangalia jambo gani likupate sababu umeapa au kuna mtu ameapa mambo fulani yakupate.

Mungu akitaka kufanya jambo na mtu anaapa kwamba anachokisema lazima kitatimia.

Isaya 45:22-23 “Niangalieni mimi, mkaokolewe, enyi ncha zote za dunia; maana mimi ni Mungu; hapana mwingine.Kwa nafsi yangu nimeapa, neno hili limetoka kinywani mwangu katika haki, wala halitarudi, ya kwamba mbele zangu kila goti litapigwa, kila ulimi utaapa.”

Waebrania 6:13-16 “Kwa maana Mungu, alipompa Ibrahimu ahadi, kwa sababu alikuwa hana mkubwa kuliko yeye mwenyewe wa kumwapa, aliapa kwa nafsi yake,akisema, Hakika yangu kubariki nitakubariki, na kuongeza nitakuongeza.Na hivyo kwa kuvumilia akaipata ile ahadi.Maana wanadamu huapa kwa yeye aliye mkuu kuliko wao; na kwao ukomo wa mashindano yote ya maneno ni kiapo, kwa kuyathibitisha.”

Uharibifu huletwa ndani ya kiapo ikiwa aliyeapa kutenda jambo fulani hajalitimiza. Leo hii kuna viapo vinawasumbua watu na wengibe hawajui wanateseka kwasababu ya viapo flani walivyofanya.

UKIRI

Kila kiapo kilichofanywa juu yangu ili kuniletea uharibifu nakisambaratisha kwa jina la Yesu Amen

 MUNGU AKUBARIKI SANA KWA KUENDELEA KUJIFUNZA MANENO YA MUNGU .

>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>

KANISA LA ELIM PENTEKOSTE NCHI YA UKOMBOZI- MUHAWA SINGIDA MJINI.

(NENO, MAOMBI NA MAOMBEZI)

Tuna ununuzi wa vifaa kwa ajili ya Mkutano wa Injili. Unaweza kuchangia kwa ajili ya kuhubiri injili na Mungu atakutana na wewe na kuzungumza na wewe na atatenda mambo makubwa sana kwenye maisha yako kuanzia leo.

TUNAHITAJI KUNUNUA.

1. VITAMBAA VYA MADHABAHU........TSHS, 60000/=

2.MAIKI WIRELESS....4......TSHS, 240,000/=

3. MAIKI ZA WIRE......4.......TSHS, 100,000/=

4. TRUBAI...........4..........TSHS, 60,000/=

5. MABATI  20@ 27,000......JUMLA NI TSHS, 540,000/=

6. DRAMS......1........TSHS, 1,100,000/=

7.SPEAKER FIDEK 3......TSHS, 2,100,000/=

WASILIANA NA MCHUNGAJI ILI MCHUNGAJI AKUOMBEE PAPO HAPO UTAKAPOCHANGIA KIMOJA WAPO KATI YA HIVYO HAPO JUU AU CHOCHOTE ULICHO NACHO TUNAPOKEA.

MUNGU AKUBARIKI SANA, AKUFUNGUE KWENYE HILO UNALOPITIA, MUNGU AKUINUE KATIKA FAMILIA, UCHUMI, KAZI NA MENGINEYO UNAYOHITAJI KATIKA MOYO WAKO.

NAMBA ZINAZOTUMIKA KATIKA MCHANGO NI NAMBA ZA MCHUNGAJI TU.

1. M-PESA  0762756542.....JINA: LAURENT MPOMA

2. AIRTEL MONEY: 0782859946....JINA: LAURENT MPOMA

3: TIGO PESA: 0714890889.....JINA : LAURENT MPOMA

>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>

KWA MSAADA ZAIDI NA MAOMBEZI:

WASILIANA NA MCHUNGAJI AU

FIKA KANISANI,

KANISA LA ELIM PENTEKOSTE NCHI YA UKOMBOZI

(NENO, MAOMBI NA MAOMBEZI)

AU WASILIANA NASI KUPITIA

FACEBOOK: nchi ya ukombozi ministry

Follow us on YOUTUBE: Upenyo Wa Mungu Tv

TELEPHONE: +255762756542

WHATSAP: +255762756542

BLOGSPOT: NCHI YA UKOMBOZI MINISTRY

http:// nchiyaukomboziministrytz.blogspot.com/

MUNGU AKUBARIKI SANA KWA KUJIFUNZA MANENO YA MUNGU.

 

 

Post a Comment

0 Comments