MAOMBI YA UREJESHO
UREJESHO KWENYE NDOA NA MAHUSIANO
Malaki 2:13-16. Mungu anachukia kuachana. Mungu
hapendi mvurugano kwenye ndoa. Dhumuni la Mungu kuwapa ndoa ni kwamba mumzalie
mtoto atakayemcha Yeye. Mwambie Mungu kuhusu ahadi hiyo na kwamba arejeshe ndoa
na mahusiano yenu kwa maana yeye mwenyewe hataki kuachana kwa wana ndoa.
UREJESHO KWENYE UCHUMI NA MAISHA YAKO
AMBAYO YAMEKUWA DUNI
Ruth 4:15 mwambie Mungu arejeshe uchumi katika
maisha yako ambayo unayaona sasa yamekuwa duni. Naomi aliishi maisha duni sana
baada ya mume wake na watoto wake kufariki. Mungu aweza kukurejeshea uchumi na
maisha bora na kukung’arisha kama Naomi.
Pia angalia
ahadi ya Mungu katika Isaya 58:12
UREJESHO KWENYE MAGONJWA
Yeremia. 30:17 “Lakini nitakurudishia afya yako na
kuyaponya majeraha yako asema BWANA”.
Omba mwambie Mungu umeahidi kunirudia afya yangu sawa sawa na neno lako.
Yesu yule yule aliyeponya maelfu elfu bado anaponya hata leo maana yeye
hajabadili Ebrania 13:8
UREJESHO KWENYE MIAKA ILIYOPOTEA
Yoeli 2:25. Mwambie Mungu rejesha miaka yangu
yote niliyopoteza. Mungu hurejesha muda wote tulioupoteza kinyume na mapenzi
yake tukimrudia.
UREJESHO KATIKA MOYO ULIOJERUHIWA
Zaburi 34:17-19. Mungu hurejesha upya roho za watu waliopita
kwenye mateso na kuvunjika moyo sababu ya taabu mbalimbali za dunia. Ikiwa ni
katika ndoa, kazini au kwenye jamii. Mungu yuko karibu nawe uliyevunjika moyo
na Bwana yuko tayari kukuokoa. Pia Zaburi
51:12.
ENDELEA KUFUATILIA BLOGSPOT HII ITAKUFUNGUA
KWA MAANDIKO YALIYOPO NDANI YAKE.
+255762756542
WATSAP: +255762756542
0 Comments