ILI UWEZE KUWA HODARI KATIKA MUNGU
1. Vaa silaha za MUNGU.
Waefeso 6:11
"Vaeni silaha zote za MUNGU, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani."
Baada ya wewe kumpokea YESU KRISTO kama Mwokozi wako
inakupasa sana kufanya mambo ya Kibiblia yanaweza kukufanya uwe hodari katika
MUNGU na katika uweza wa nguvu zake.
Silaha za MUNGU zinaweza kukufanya uwe hodari katika MUNGU
maana MUNGU hatakuwa kinyume na wewe.
Silaha hizi za MUNGU tunazivaa kwa kuziishi na sio kuzitaja
tu.
2. Mpokee ROHO MTAKATIFU.
Yohana 14:26 " Lakini huyo Msaidizi, huyo ROHO MTAKATIFU,
ambaye BABA atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote
niliyowaambia."
Ukimpokea ROHO MTAKATIFU hakika utapokea na yote yaayomhusu.
Utapokea nguvu, utapokea maelekezo ya kukusaidia, utapokea
kibali kikuu kwa MUNGU n.k
3. Lifanyie kazi Neno la MUNGU.
Yakobo 1:22
"Lakini iweni watendaji wa neno, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya
nafsi zenu."
4. Nyenyekea kwa MUNGU katika KRISTO YESU.
1 Petro 5:6 "Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa MUNGU
ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake;"
5. Ishi maisha ya kuongozwa na ROHO MTAKATIFU utashinda kila
nguvu za kishetani.
1 Yohana 4:4
"Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na MUNGU nanyi mmewashinda, kwa sababu
yeye(ROHO MTAKATIFU) aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye(Shetani) aliye katika
dunia."
6. Zitafute nguvu za MUNGU kwa maombi
yanayoambatana na maisha matakatifu.
Waefeso 6:18
"kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika ROHO, mkikesha kwa
jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;"
Maombi ni njia mojawapo kuu ya kukufanya uwe hodari katika
MUNGU maana maombi yatakufanya uwe mshindi daima.
Maombi yapo ya aina mbili yaani maombi ya bila kufunga na
kisha kuna maombi ya kufunga(Mathayo 17:21), haya nayo ni ya muhimu sana sana
ili uwe mshindi mwenye nguvu daima.
Hivyo tafuta daima nguvu za MUNGU.
1 Nyakati 16:11 "Mtakeni BWANA na nguvu zake; Utafuteni
uso wake siku zote."
7. Mtumikie Bwana YESU Mwokozi.
Danieli 11:32b "
lakini watu wamjuao MUNGU wao watakuwa hodari, na kutenda mambo makuu."
Ukimtumikia MUNGU kwa
usahihi katika KRISTO YESU lazima uwe hodari.
1 Wakorintho 15:58 "Basi, ndugu zangu wapendwa,
mwimarike, msitikisike, mkazidi sana kutenda kazi ya BWANA sikuzote, kwa kuwa
mwajua ya kwamba taabu yenu siyo bure katika BWANA."
Nguvu za MUNGU kubwa sana huwa zinaambatana na Neno la MUNGU, hivyo unavyomtumikia Bwana YESU ujue nguvu za MUNGU lazima ziambatane na wewe.
MUNGU AKUBARIKI SANA
MAOMBI NA MAOMBEZI
PIGA +255714890889
0 Comments