Follow us

YAFUATAYO NI BAADHI YA MAMBO MUHIMU AMBAYO ROHO WA MUNGU AMENIFUNULIA TUJUE MUNGU ALIVYOKUSUDIA KWA AJILI YETU WATOTO WAKE:-

Tangazo

 


YAFUATAYO NI BAADHI YA MAMBO MUHIMU AMBAYO ROHO WA MUNGU AMENIFUNULIA TUJUE MUNGU ALIVYOKUSUDIA KWA AJILI YETU WATOTO WAKE:-

1.   Ni mwaka wa kuwekeza na kukusanya (kuweka akiba) Zaidi kwa kuwa kuna mabadiliko ya kiuchumi yanakuja.

Biblia katika kitabu cha Mwanzo 41:35-36 inasema ‘Na wakusanye chakula chote cha miaka hii myema ijayo, wakaweke akiba ya nafaka mikononi mwa Farao wakakilinde kuwa chakula katika miji. Na hicho chakula kitakuwa akiba ya nchi kwa ajili ya miaka hiyo saba ya njaa, itakayokuwa katika nchi ya Misri, nchi isiharibike kwa njaa’.

2.   Ni mwaka wa kucheka kwa kuwa BWANA anaenda kuwafurahisha watu wake wale wanaomtegemea.

Ayubu 42:10 ‘Kisha BWANA akageuza uteka wa Ayubu, hapo alipowaombea rafiki zake; BWANA naye akampa Ayubu mara mbili kuliko hayo aliyokuwa nayo kwanza’.  Ukisoma kitabu cha Ayubu sura 1-2 utaona habari za Ayubu na jinsi Shetani alivyoharibu maisha yake kwa ujumla. Kilikuwa ni kipindi kigumu sana kwa Ayubu, hata hivyo hizo ndio nyakati zilizokuwa zimeruhusiwa juu yake. Maandiko yanaonyesha kuwa baada ya Ayubu kusimama vizuri na Mungu wake katika kipindi hicho kigumu, BWANA alimrejeshea Ayubu maradufu kila kilichokuwa kimeharibiwa na Shetani yaani furaha, afya, watoto na mali zake zote.

3.   Ni mwaka wa amani utakaokupa fursa ya kujijenga na kutimiza mapenzi ya Mungu kwa mwaka husika.

1 Waflme 5: 3-5, ‘Umemjua Daudi baba yangu jinsi asivyoweza kujenga nyumba kwa jina la Bwana, Mungu wake, kwa sababu ya vita vilivyomzunguka pande zote, hata Bwana alipowatia watu chini ya nyayo zake. Ila leo Bwana, Mungu wangu, amenipa amani kila upande; hakuna adui, wala tukio baya. Nami, tazama, nakusudia kujenga nyumba kwa jina la Bwana, Mungu wangu, kama Bwana alivyomwambia Daudi baba yangu, akisema, Mwana wako, nitakayemweka katika kiti chake cha enzi mahali pako, ndiye atakayeijenga nyumba kwa jina langu’.

Maneno haya yalisemwa na Sulemani baada ya kutawazwa kuwa mfalme kufuatia kifo cha baba yake Daudi. Ukisoma Biblia yako vema utagundua kwamba utawala wa Daudi ulikuwa na vita sana, na kwa sababu ya vita na damu nyingi iliyomwagika katika kipindi chake BWANA alimzuia Daudi asimjengee Hakalu. Hekalu lilijengwa kipindi cha mwanawe Sulemani.  Naam ili Sulemani aweze kujenga hekalu vema, BWANA akampa amani pande zote na kazuia baya lolote lisitokee.

MUNGU AKUBARIKI SANA

Post a Comment

0 Comments