Follow us

KUKOMBOLEWA KUTOKA KATIKA NGUVU ZA GIZA

Tangazo

PASTOR : LAURENT
NCHI YA UKOMBOZI MINISTRY

Nikusudi la Mungu mwanadamu aishi maisha mazuri na yakumpendeza yeye,tena Mungu alimuweka mwanadamu kuwa mtawala katika ulimwengu huu ambao Mungu aliuumba ila tu mwanadamu alipoteza nafasi hiyo baada ya kufanya dhambi (Yer.5:25)lakini Mungu kwa neema yake na upendo wake alimtuma Mwanawe wa pekee Yesu Kristo awakomboe wanadamu(Yoh.3:16) nakuwapatanisha na Mungu na hivyo kuirudisha nafasi ile ambayo Mungu alimuwekea mwanadamu ila shetani kwa ujanja  wake aliichukua(Mwanz.3:13)

Fuatana nami  katika mafundisho haya,tafakari kwa kina kisha chukua hatua

Ukisoma katika Uf.12:17 utaona kuwa shetani amekasirika dhidi ya mwanamke na amedhamiria kufanya vita juu ya uzao wa mwanamke lakini hasira yake ni juu ya wale wazishikao sheria za Mungu na wenye ushuhuda wa Yesu (Ebra.12:1); nia yake ni atawale kizazi cha mwanamke,wale wasiompinga hana hasira nao maana wanakuwa chini yake (Ef.2:1-3).

Katika Mwanzo 3 tunaona kuwa Wazazi wetu wa kwanza,adamu na hawa,walimkabidhi shetani dunia waliyopewa na Mungu (2Kor.4:3-4), hivyo basi shetani akatumia hila na uongo (Yoh.8:44) ili awafunge waweke patano/mkataba nao

Shetani ni mwerevu mwenye ngazi ya kimalaika,kumbuka hapo mwanzo alikuwa malaika mwenye cheo kizuri huko Mbinguni(Isa.14:9-17),anafahamu tabia za Mungu na mambo yote mazuri ambayo Mungu ameyaweka kwaajili ya mwanadamu ndio maana alitaka kumpindua Mungu akashindwa na badala yake amekusudia kumpotosha mwanadamu ili asipate yale ambayo Mungu ameweka kwaajili ya wanadamu

Kumbuka mwanadamu nizaidi ya malaika ndio maana malaika hakupewa kutawala na Mungu isipokuwa mwanadamu(Mwanz.1:26, 1Kor.6:3).

Shetani naye anatamani kuabudiwa na kuogopwa na mwanadamu ndio maana anafanya yote haya(Isa.14:13); biblia inasema shetani alipambana na malaika,hivyo mwanadamu peke yako huwezi kupambana naye  isipokuwa ukiwa na Nguvu za Mungu na kwa kumkubali Yesu katika maisha yako maana yeye ni Jemedari wa vita(Rum.10:9-10).

Shetani anaelewa kwamba Mungu ni wa maagano,na agano linadumu kizazi hata kizazi (Torati 8:18,Zab.102:12) Shetani anafanya mbinu za kuwadanganya wanadamu wapuuze mkataba wao na Mungu halafu anawashawishi kuanzisha mkataba mpya nao(2Tim.2:26)

·         Falme na mamlaka

·         Wakuu wa giza hili

·         Jeshi la pepo wabaya


MUNGU AKUBARIKI SANA

M

Post a Comment

0 Comments