Follow us

JE UMEJIANDAAJE KUKABILI MWAKA 2022?

Tangazo

MCH:LAURENT MPOMA

Lakini Je kama Mkristo umejiandaaje kukabili mwaka 2022? Biblia inasemaje kuhusu majira, nyakati na mwaka aliotupa Bwana?

Biblia inatuambia katika kitabu cha Mhubiri 3:1-8  ‘kwa kila jambo kuna majira yake, na wakati wa kila kusudi chini ya mbingu; Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung'oa yaliyopandwa; Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga; Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza; Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe; Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia; Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza; Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa; Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia; Wakati wa vita, na wakati wa amani.’

Katika mistari hiyo tunaona Biblia ikielezea vitu vingi ambavyo Mungu ameviumba na kuviweka chini ya mbingu LAKINI vyote vimewekwa katika WAKATI (TIME) yake ndani ya kusudi maalumu la Mungu. Maana yake ni kwamba kila kitu ambacho Mungu amekiweka chini ya mbingu kipo/kimefungwa ndani ya muda/wakati wake maalumu na haiwezekani kukatokea muingiliano, kwani wakati ndio UFUNGUO au ndio unao amuru kitu gani kiwepo au kisiwepo. Huu ndio utaratibu wa Mungu aliouweka.

Kwanini Mungu ameweka utaratibu? Ipo siri ya Mungu na muda, Muda na Mungu ni marafiki tena wana mahusiano mazuri sana. Muda anaongoza maamuzi ya Mungu na Mungu anaongoza matumizi ya muda kwa kuiweka mipango yake ndani ya mtu au kuachilia majira Fulani katika mwaka na kumwagiza mwanadamu atekeleze hiyo mipango/majira ndani muda sahihi aliokusudia.

Ukisoma 1 Wakorinto 2:9 -10 ‘Lakini, kama ilivyoandikwa, mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, (wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,) mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao. Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchungza yote, hata mafumbo ya Mungu’. Kwahiyo njia peke ni kumuliza Roho wa Mungu peke yake ndiye aliye na uwezo wa kutufunulia yote ili tuweze kujua.

MUNGU AKUBARIKI SANA

Post a Comment

0 Comments