Lakini Je kama Mkristo umejiandaaje kukabili mwaka 2022? Biblia inasemaje kuhusu majira, nyakati na mwaka aliotupa Bwana?
Biblia
inatuambia katika kitabu cha Mhubiri 3:1-8
‘kwa kila jambo kuna majira yake, na wakati wa kila kusudi chini ya
mbingu; Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa
kung'oa yaliyopandwa; Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa,
na wakati wa kujenga; Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa
kuomboleza, na wakati wa kucheza; Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya
mawe; Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia; Wakati wa kutafuta, na
wakati wa kupoteza; Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa; Wakati wa kurarua,
na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;Wakati wa
kupenda, na wakati wa kuchukia; Wakati wa vita, na wakati wa amani.’
Katika
mistari hiyo tunaona Biblia ikielezea vitu vingi ambavyo Mungu ameviumba na
kuviweka chini ya mbingu LAKINI vyote vimewekwa katika WAKATI (TIME) yake ndani
ya kusudi maalumu la Mungu. Maana yake ni kwamba kila kitu ambacho Mungu
amekiweka chini ya mbingu kipo/kimefungwa ndani ya muda/wakati wake maalumu na
haiwezekani kukatokea muingiliano, kwani wakati ndio UFUNGUO au ndio unao amuru
kitu gani kiwepo au kisiwepo. Huu ndio utaratibu wa Mungu aliouweka.
Kwanini
Mungu ameweka utaratibu? Ipo siri ya Mungu na muda, Muda na Mungu ni marafiki
tena wana mahusiano mazuri sana. Muda anaongoza maamuzi ya Mungu na Mungu
anaongoza matumizi ya muda kwa kuiweka mipango yake ndani ya mtu au kuachilia
majira Fulani katika mwaka na kumwagiza mwanadamu atekeleze hiyo mipango/majira
ndani muda sahihi aliokusudia.
Ukisoma 1
Wakorinto 2:9 -10 ‘Lakini, kama ilivyoandikwa, mambo ambayo jicho halikuyaona
wala sikio halikuyasikia, (wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,) mambo
ambayo Mungu aliwaandalia wampendao. Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho.
Maana Roho huchungza yote, hata mafumbo ya Mungu’. Kwahiyo njia peke ni
kumuliza Roho wa Mungu peke yake ndiye aliye na uwezo wa kutufunulia yote ili
tuweze kujua.
MUNGU AKUBARIKI SANA
0 Comments