SOMO: VIFUNGO
Kifungo cha
kipepo ni adhabu ya mtu kuwekwa jela kipepo na mawakala wa shetani.
Baadhi ya
vifungo hivyo vimetajwa katika Isaya
42:22 ''Lakini watu hawa ni watu walioibiwa na kutekwa; wote wamenaswa katika
mashimo, wamefichwa katika magereza; wamekuwa mawindo, wala hapana aokoaye;
wamekuwa mateka, wala hapana asemaye, Rudisha. '' acha nikifafanulie.
Vifungo hivyo vya giza ni hivi.
1. Kuibiwa ufahamu kipepo ili ulitumikie kusudi la shetani na sio la
MUNGU.
''Lakini
watu hawa ni watu walioibiwa ''
Kuna watu
wengi fahamu zao zimefunga kipepo kiasi kwamba wanalitumikia kusudi la shetani
na sio la MUNGU, Leo kwa njia ya maombi yako katika jina la YESU KRISTO
hakikisha unakiharibu kifungo hicho cha giza kilichokufunga ufahamu.
Fikra zako
zinatakiwa zimtii KRISTO na sio kutii majini na mizimu.
2 Kor 10:3-5
'' Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya
mwili; (maana silaha za vita vyetu si za
mwili, bali zina uwezo katika MUNGU hata kuangusha ngome;) tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka,
kijiinuacho juu ya elimu ya MUNGU; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii
KRISTO; ''
2. Kutekwa na nguvu za giza.
''Lakini watu hawa ni watu waliotekwa''
Baadhi ya
dalili ya mtu aliye katika kifungo cha kutekwa na nguvu za giza ni kuonewa sana
na majini au wachawi kwa sababu tu wamekuteka katika ulimwengu wa roho.
Somo
linaitwa jinsi ya kutoka kwenye vifungo vya giza, ni muhimu kujua kwamba kila
kifungo kina kanuni zake hadi utoke katika kifungo hicho, kuna vifungo vingine
huhitaji hata maombi bali unahitaji tu kubadilika tabia na kifungo hicho
kinaondoka.
3.Kunaswa katika mashimo ya giza.
''Lakini
watu hawa ni watu walionaswa katika
mashimo''
Inawezekana
wewe uko katika kifungo cha mashimo ya giza.
Inawezekana
uko katika shimo la dhambi.
Inawezekana
wewe uko katika shimo la madeni au kufilisika.
Inawezekana
umenaswa katika shimo la magonjwa na hadi kwa sasa unadhani hutapona kabisa
kulingana na jinsi unavyouona ugonjwa wako.
Inawezekana
uko katika shimo la kifo ili siku chache zijazo upate ajali mbaya waliyoipanga
wachawi na wakuu wa giza ili ikupate.
Wakati
mwingine kupitia ndoto ambazo unaota unakuwa unajulishwa aina ya kifungo
ambacho umefungwa ili ujue jinsi ya kutoka katika kifungo hicho.
Inawezekana
wewe huota ndoto kabisa ukiwa ndani ya shimo refu sana na huoni pa kutokea,
hapo unaonyeshwa aina ya kifungo kinachokutesa.
Ndugu, leo
katika jina la YESU KRISTO nakuomba kimbilia maombezi makanisani na utaombewa
na kifungo hicho kukuacha.
4. Kufichwa katika magereza.
''Lakini
watu hawa ni watu waliofichwa katika magereza ''
Kuna kifungo
cha giza kinaitwa gereza.
Inawezekana
wewe uko katika gereza la magaonjwa, kukataliwa,kudhalauliwa bila sababu,
kutengwa n.k
Inawezekana
ndoa yako iko gerezani, inawezekana uchumba wako uko gerezani, iinawezekana
biashara yako au wito wako viko gerezani
Ndugu leo
hakikisha unandoka katika gereza la kipepo ulimofungwa kipepo.
5. Kuwa Mawindo ya nguvu za giza.
''Lakini
watu hawa ni watu ambaob wamekuwa
mawindo, ''
Kuna kifungo
kinaitwa mawindo, inawezekana wewe siku zote uko katika mawindo ya majini au
wachawi.
Kuna watu
huwa hawalali usiku kwa sababu wako katika mawindo ya wachawi na majini.
Mama mmoja
kutoka nchi jirani siku moja alinipigia simu ili nimuombee, nilipomuombea kesho
yake alituma sadaka kisha akasema hivi ‘’ Mtumishi Mabula huwezi kuamini mimi
na mtoto wangu tuna zaidi ya miezi miwili bila kulala usiku, jana uliponiombea
ndio nilishangaa maana nilipojaribu kulala nikashtuka nikidhani wachawi sasa
wanakuja kumbe ili asubuhi saa mbili yaani nililala salama kwa mara ya kwanza’’
Mathayo 18:18 '' Amin, nawaambieni, yo yote
mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua
duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni. ''
MUNGU
AKUBARIKI SANA.
MAOMBI NA
MAOMBEZI WASILIANA NA MCHUNGAJI LAURENT MPOMA
PIGA:
0762756542, 0714890889
WATSAP:
0762756542
JIFUNZE ZAIDI HAPA>>>"shorturl.at/tFKU9"
0 Comments