Adui anakuja
kuiba, kuua na kuharibu kila kitu chetu, ni lazima kuwa tayari kupambana na
maadui, tujue silaha zetu, na kutumia neno la Mungu. Ni lazima kujifunza neno
la Mungu na kulitumia katika maisha yetu ya kila siku.
Baba neno lako katika Yer 23:29 linasema “Je! Neno langu si kama
moto? Asema Bwana; na kama nyundo ivunjayo mawe vipande vipande? ”Nasimama sawa
sawa na neno lako, na kuvunja vipande vipande kila mipango ya kishetani, miradi
na kazi mbaya za adui, katika pepo nne za dunia, katika jina la Yesu.
Baba neno katika Waebrania 4:12 "linasema “Maana Neno la Mungu
li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili.
Nachukua mamlaka ya neno lako ambalo ni upanga na kugawanya nafsi na roho, na
viungo na mafuta yaliyomo ndani ya kila nguvu za uchawi, kila enzi, falme,
mamlaka, wakuu wa giza, mapepo wabaya katika ulimwengu wa roho, mishale ya moto
ya adui, maadui wa siri, maadui wanaojulikana, mapepo ya utambuzi, maadui wa
ndani, na mamlaka zingine zote za adui, kwa kuwafunga na kuwatupa katika shimo
milele, katika jina la Yesu, Amina.
Baba neno lako katika Yer 23:29
linasema “Je! Neno
langu si kama moto? Asema Bwana; na kama nyundo ivunjayo mawe vipande vipande?
”. Natumia moto wa Mungu Mwenyezi, kuchoma kila kazi ya adui kama majivu.
Chochote ambacho kilitumwa kwangu, kinachonifuata, kilichohamishiwa kwangu, au
kwenye kitu chochote ambacho ni changu. Nazifunga, na kuzitupa katika lile ziwa
la moto, sasa na hata milele, katika jina la Yesu.
Baba neno
lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu Zaburi 119: 105. Nasimama
sawa sawa na neno lako, na kutumia mwanga wako kuangaza kila mahali penye giza
ambapo jua haliangazi. Naweka wazi kila matendo mabaya yanayotendeka kwenye
maisha yangu, familia, watoto, fedha za nyumbani, kazi, huduma, ndoa, na yote
ambayo ni yetu. Bwana nakushukuru kwa kufanya kazi za uovu wao kuwa dhaifu,
zife, zifungwe na kufutwa, katika jina la Yesu.
Baba neno lako katika Yakobo 1:22-25 "linasema kwamba neno lako ni
kama kioo" Natumia mamlaka ya neno lako, na kubamiza, kuangamiza vipande
vipande vioo vyote vya mapepo, ambavyo adui hutumia kufuatilia maendeleo yetu,
mafanikio, baraka, na yote yaliyo yetu. Naamrisha maadui, kuona shughuli zao
mbaya, kushindwa, na anguko katika vioo vyao vya kipepo, katika jina la Yesu.
Baba neno
lako ni kama maji ambayo yatusafisha dhambi zote na uovu. Waefeso 5:26-27. Natumia maji ya Bwana Mungu mwenyezi kuwazamisha
maadui, mafarao wote, mayezebeli, goliati na maadui wengine wote wa maendeleo
yetu katika bahari Shamu, sawa sawa na Kutoka sura ya 15
Baba neno
lako linaniambia katika Zaburi 107:20 "Kwamba neno ni kama dawa"
Nasimama sawa sawa na neno lako ambalo ni kama dawa, na kuponya mioyo yetu na
machungu yote, uponyaji wa kimwili, kiakili, kihisia, na kiroho. Naomba neno
lako liturejeshee mara mia moja, kila kitu tulichopoteza, katika jina la Yesu
ASANTE KWA KUJIFUNZA MAANDIKO YA NENO LA MUNGU.
TUNAUNUNUZI WA VIFAA HIVI KWA AJILI YA MKUTANO WA INJILI.
1. SPEAKER.......1....TSHS, 350,000/=
2. VITAA VYA MADHABAHU..........TSHS, 50,000/=
3. MAIKI .......WIRELESS......2.....TSHS, 100,000/=
4. VITI........10......TSHS, 160,000/=
5. MAIKI 2 ….WIRE…..TSHS, 50,000/=
UKIGUSWA KUMTOLEA MUNGU.
WASILIANA NA MCHUNGAJI
TUMIA:
0762756542....M-PESA.......JINA: LAURENT MPOMA
0714890889.....TIGO PESA....JINA: LAURENT MPOMA
0782859946.....AIRTEL MONEY......JINA: LAURENT MPOMA
KUTAKUWA NA MAOMBI KWA KILA MTU ATAKAYE MTOLEA MUNGU.
MUNGU AKUBARIKI SANA
MAOMBI NA MAOMBEZI
PIGA : 0762756542, 0782859942, 0714890889
WATSAP: 076275654.
0714890889


0 Comments