MCHUNGAJI LAURENT MPOMA
Kifungo cha kipepo
Kifungo cha kipepo ni adhabu ya mtu kuwekwa jela kipepo
na mawakala wa shetani.
Wako watu wengi tu wanateswa na vifungo vya giza katika
maisha yao, wengine wanatamani watoke katika vifungo hivyo lakini imeshindikana
maana wanaenenda kimwili na sio kiroho.
Zaburi 142:7 "Uitoe nafsi yangu kifungoni. Nipate
kulishukuru jina lako. Wenye haki watanizunguka, Kwa kuwa Wewe
unanikirimu."
Jambo la kwanza kabisa nataka kukuambia ni kwamba Bwana
YESU alikuja ili kuzivunja na kuziharibu kazi zote za shetani vikiwemo vifungo
vya kipepo.
1 Yohana 3:8b "Kwa kusudi hili Mwana wa MUNGU
alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi."
VIFUNGO
HIVYO VYA GIZA.
1.
Kuibiwa ufahamu kipepo ili ulitumikie kusudi la shetani na sio la MUNGU.
Kuna watu wengi fahamu zao zimefungwa kipepo kiasi kwamba
wanalitumikia kusudi la shetani na sio la MUNGU, Leo kwa njia ya maombi yako
katika jina la YESU KRISTO hakikisha unakiharibu kifungo hicho cha giza
kilichokufunga ufahamu.
2 Wakorintho 10:4-5 " (maana silaha za vita vyetu si
za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)
tukiangusha mawazo
na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya MUNGU; na tukiteka nyara
kila fikira ipate kumtii KRISTO;"
2.
Kutekwa na nguvu za giza.
Baadhi ya dalili ya mtu aliye katika kifungu cha kutekwa
na nguvu za giza ni kuonewa sana na majini au wachawi kwa sababu tu wamekuteka
katika ulimwengu wa roho.
Mathayo 16:19 "Nami nitakupa wewe funguo za ufalme
wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni;
na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni."
4.
Kufichwa katika magereza.
Kuna kifungo cha giza kinaitwa gereza.
Inawezekana wewe uko katika gereza la madeni,
kukataliwa,kudhalauliwa bila sababu, kutengwa n.k
Inawezekana ndoa yako iko gerezani, inawezekana uchumba
wako uko gerezani, iinawezekana biashara yako au wito wako viko gerezani.
Ndugu leo hakikisha unandoka katika gereza la kipepo
ulimofungwa kipepo.
Omba au ombewa na watumishi waaminifu wa KRISTO na
utatoka katika kifungo hicho.
Mathayo 7:7 "Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi
mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa;"
5.
Mawindo.
Kuna kifungo kinaitwa mawindo, inawezekana wewe siku zote
uko katika mawindo ya majini au wachawi.
Kuna watu huwa hawalali usiku kwa sababu wako katika
mawindo ya wachawi na majini.
Mathayo 18:18 "Amin, nawaambieni, yo yote
mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua
duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni."
Ndugu kumbuka kwamba YESU alikuwa anaziamuru nguvu za
giza ziwatoke watu na zinatoka.
Luka 4:36 "Mshangao ukawashika wote, wakasemezana
wakisema, Ni neno gani hili, maana awaamuru pepo wachafu kwa uwezo na nguvu,
nao hutoka."
MUNGU AKUBARIKI SANA KWA KUJIFUNZA MANENO YA MUNGU.
TUNA MCHANGO WA UNUNUZI VIFAA KWA AJILI YA MKUTANO WA INJILI
1: SPIKA-------TSHS, 800,000/=
2: MAIKI 2 ZA WIRELESS....TSHS, 150,000/=
3: MAIKI 2 ZA WIRE......TSHS, 50,000/=
4: VITAMBAA VYA MADHABAHU.....TSHS, 60,000/=
KAMA UTAGUSWA KUCHANGIA KWA AJILI YA KUHUBIRI INJILI WASILIANA NA MCHUNGAJI KWA NAMBA:
AIRTEL: +255782859946.....JINA: LAURENT MPOMA
VODA: +255762756542........JINA: LAURENT MPOMA
TIGO: +255714890889..........JINA: LAURENT MPOMA
Mchungaji atakuombea na Mungu atakufungua....AMINA
===================================================================
MAOMBI NA MAOMBEZI
PIGA: +255762756542
WHATSAP: +255762756542
YOUTUBE: "upenyo Wa Mungu Tv". Kisha bonyeza "SUBSCRIBE"
0 Comments