Katika maombi ni muhimu sana kujua mambo yafuatayo.
1. Kuomba kwa imani
Hivyo ni
lazima uwe na Imani maana pasipo Imani haiwezekani kumwona Mungu.
Hivyo wewe
Muombaji shika kanuni hiyo ya kiroho kwamba ''Pasipo imani siwezi kumpendeza
MUNGU na pasipo utakatifu siwezi kumwona MUNGU''
Biblia
inasema katika Yohana 1:18 '' Hakuna mtu aliyemwona MUNGU wakati wo wote; MUNGU
Mwana pekee aliye katika kifua cha Baba(MUNGU), huyu ndiye aliyemfunua.'' Kumbe Hakuna mwanadamu awezaye kumwona MUNGU
kwa sura lakini Mathayo 5:8 inasema wenye moyo safi yaani watakatifu watamuona
MUNGU, Yaani watakatifu wataingia uzima wa milele na kumwona MUNGU lakini pia
watakatifu watasikiwa na MUNGU na kutendewa muujiza.
A. Kuomba ukilitaja na kulitegemea jina la YESU ili ushinde. Yohana 14:13 ''Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu(YESU KRISTO), hilo nitalifanya, ili Baba(MUNGU) atukuzwe ndani ya Mwana. ''
3. Kuomba katika ROHO MTAKATIFU.
Kuomba katika ROHO MTAKATIFU inajumuisha mambo mawili.
1. Kunena kwa lugha katika ROHO MTAKATIFU. Marko 16:16-17 "Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa. Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; WATASEMA KWA LUGHA MPYA;"
2. Kuomba kwa kuongozwa na ROHO MTAKATIFU au kujulishwa na ROHO MTAKATIFU. Yuda 1:20 "Bali ninyi, wapenzi, mkijijenga juu ya imani yenu iliyo takatifu sana, na kuomba katika ROHO MTAKATIFU,"
0 Comments