Follow us

NJIA MUHIMU KATIKA KUKUA KIROHO

Tangazo

                     

 NJIA MUHIMU KATIKA KUKUA KIROHO

1.KUWA MHUDHURIAJI WA IBADA.

 Isaya 9:6: Yesu ni Mungupamoja na yeye kuwa Mungu katika mwonekano wa kuvaa mwili wa kibinadamu, Yesu Kristo alikuwa akihudhuria kila palipokuwa ni mda wa kusali, alikuwa akienda kusali kwenye masinagogi (makanisa ya Wayahudi )

 Alitambua wazi kuwa Mkristo asipozingatia ibada hawezi kukomaa na kuimarika kiroho pia watu wanapokusanyika kwa ajiri ya Bwana Mungu naye huwepo katika hilo kusanyiko  ( MATHAYO 18:20)

 Tuangalie kitabu cha

KUMBUKUMBU LA TORATI 12:5

mungu anawaagiza wana wa islaeli kuwa mahali atakapo pachagua bwana Mungu aweke jina lake maana ni makao yake "ELEKEZENI NYUSO ZENU PALE NA MWENDE HUKO"

neno hili linatufundisha kwamba sehemu ambayo Mungu amechagua na akajenga madhabahu yake (kanisa) kupitia makuhani Wake (wachungaji) ni lazima tukusanyike pale tumwabudu na kumtukuza yeye maana pale ndio makao yake na anasema nasi kupitia madhabahu yake hiyo (kanisa )tukusanyike pale tumwabudu. Bila ibada kiroho chako kitadumaa kamwe huwezi endelea mbele.

 WAEBRANIA 10:25

neno linaendelea kutuhimiza tusiache kukusanyika kama ilivyo desturi yetu kua siku za ibada ni lazima tukusanyike kanisani tumwabudu Mungu wetu.


2.KUPOKEA KIPAWA CHA ROHO MTAKATIFU

Yesu aliwaagiza wanafunzi wake wasitoke yerusalem waingojee ahadi ya Baba ambayo ni Roho Mtakatifu, akaendelea kusema mtapokea nguvu Roho Mtakatifu atakapo wajiria juu yenu ndipo sasa mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, uyahudi, Samaria na hata mwisho wa nchi.

Kumbe ili tukue kiroho yatupasa tupokee kipawa cha Roho Mtakatifu.

WARUMI 8:9

anasisitiza kusema mtu yeyote asiye na huyo Roho wa Mungu mtu huyo hatambuliwi katika ufalme wa Mungu.  (huyo si Wake kabisa)

3. KUJITOA SADAKA WEWE PAMOJA NA MALI ZAKO  .

WARUMI 12:1-2

paulo anawaandikia kanisa la kumi kuwa "itoeni miili yenu kuwa dhabihu iliyo hai, takatifu ya kumpendeza Mungu.

Neno la Mungu linatufundisha kuitoa miili yetu kuwa dhabihu takatifu yaani mtu ajitoe kwa ajiri ya Yesu, asiangarie mambo yake mwenyewe bali ajitoe,  ajidhabihu mbele za Mungu ajihesabie si kitu bila Yesu na ajitoe kwa kazi ya Mungu kwa moyo wote na kwa mali zake zote alizo nazo

MATENDO 10:1-4

bibilia inazungumza habari za mtu mmoja jina lake aliitwa Kornelio, Kornelio alikuwa akimcha Mungu yeye na nyumba yake daima, Alikuwa akitoa sadaka nyingi na kuwasaidia watu wenye uhitaji.

Ikumbukwe kwamba wakati huo Kornelio alikuwa ni mtu wa mataifa ambao Mungu alikuwa bado hajawapa neema ya kumjua yeye kwani wokovu kwa wakati huo alikuwa ni kwa Wayahudi peke yao.

hivyo ili tufikie mafanikio makubwa sana ya kiroho ni lazima tujitoe na tuwe watoaji wa sadaka mbele za Mungu na ndipo tutakua, tutastawi sana ktk maisha yetu ya kiroho na kimwili.

 Mungu akubariki na kukuzidishia katika kila jambo ufanyalo wewe uliyetoa mda wako kusoma somo hili,  MUNGU ASIKUPUNGUKIE BALI AKUKUMBUKE KATIKA KAZI ZAKO ZOTE  NA UFANIKIWE KATIKA JINA LA YESU KRISTO


MUNGU AKUBARIKI SANA KWA KUJIFUNZA MANENO YA MUNGU

Pakua APP yako sasa iliyijaa mafundisho ya Neno la MUNGU…. Hapa katika link

 hii>>>>https://play.google.com/store/apps/details?id=com.mchungaji.laurent.mpoma

YOUTUBE: KUANGALIA VIDEO ingia hapa >>>>”https://www.youtube.com/channel/UCjXjSSDOweHXL3YE5edBNIg”


MAOMBI NA MAOMBEZI 

WASILIANA NA MCHUNGAJI LAURENT MPOMA

+255763652896

Watsap: +762756542


 


Post a Comment

0 Comments