Follow us

NGUVU YA IBADA

Tangazo

 

Ili tuwe na ibada nzuri ya pamoja ( kanisani) lazima mtu mmoja mmoja awe na ibada binafsi na Muumba wake. Watu wengi tunatamani matokeo ya pamoja tukiwa wengi lakini hatuko tayali kuwa na matokeo binafsi! Jaribu kufikiri kanisa lenye watu mia tano wenye maandalizi ya ibada ( ibada binafsi) wanapokutana pamoja nini kitatokea? Ndio kile Paulo anasema watakaokuja kwenye kusanyiko hilo watamwabudu Mungu kifudifudi.

Tumekwama hapo maana tumewekeza sana kwenye ibada za makundi na tumeacha kule ibada zinakoanzia, waimbaji tumewekeza kumwimbia na kumwabudu Mungu kwenye makundi au makusanyiko makubwa kuliko kuwa na ibada binafsi na Mungu, waombaji wako busy kuandaa program za maombi ya makusanyiko ila hawana mada binafsi za maombi na Mungu, wanandoa wako bize kufanya ibada za pamoja ambazo ni njema sana ila ibada ya mmoja mmoja na Mungu haipo.

Kwa sababu hii, hata ibada zetu za makusanyiko zimekuwa za kuchosha sana, za kukimbizana na muda mpaka unajiuliza tunakimbilia wapi? Zimekuwa ibada za kukaguana nani kahubiri vizuri, nani kaimba vizuri, nani kavaaje, nani anavuta muda, matangazo yanachukua muda mwingi,


MUNGU AKUBARIKI SANA



Post a Comment

0 Comments