Follow us

NAMNA YA KUOMBEA HALI YA KIROHO YA ARDHI ILI UFANIKIWE KIMAISHA

Tangazo


 NAMNA YA KUOMBEA HALI YA KIROHO YA ARDHI ILI UFANIKIWE KIMAISHA

 LENGO : Kujifunza mbinu za kuomba ili hali ya kiroho ya Ardhi iliyokwamisha mafanikio yako iondoke na ufanikiwe.

Kuna uhusiano sana kati ya ardhi na mafanikio yako kwa hiyo ni muhimu sana kulifuatilia kwa karibu sana somo hili

Tuangalie mifano inayoonesha uhusiano wa ardhi na kufanikiwa kwa mtu.

MFANO WA KWANZA

Mwanzo 3:17-19

"Akamwambia Adamu, Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nalikuagiza, nikisema, Usiyale; ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako; michongoma na miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni; kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi"

 Laana maana yake ni

Kutostawi

Kutofanikiwa

Kutokuwa na Furaha

Kutofikia kiwango cha mafanikio ambacho Mungu kakikusudia kwa ajili yako. Na Laana ni kinyume cha baraka.

 Mungu aliposema ardhi imelaaniwa alikuwa anataka kumuambia Adamu kuwa ukitaka kujua kitu gani umebeba kwa kutofuata maelekezo yangu kuwa kuna laana iliyoko kwenye maisha yako na utakapoilima ardhi haitakuzalia matunda yake.

 MFANO WA PILI

Mwanzo 4:11-12

"Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako; utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani."

 Laana ya hapa sura ya nne ni tofauti na ile sura ya tatu kwa sababu laana ya Adamu ilikuwa ndani ya Adamu lakini katika sura ya nne tunaona kuwa laana ipo kwenye ardhi moja kwa moja.Maana yake kwa kila mtu atakaye kanyaga eneo hili anapata ile laana iliyoachiliwa kwenye ardhi .

 MFANO WA TATU

2 Mambo ya Nyakati 7:11-14

"Nikizifunga mbingu isiwe mvua, tena nikiamuru nzige kula nchi, au nikiwapelekea watu wangu tauni; ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao"

 Uponyaji tunaoungalia hapa ni uponyaji wa ardhi na nchi ni ardhi yenye mipaka halali ya kiumiliki,biblia inaposema kuwa nchi maana yake ni ardhi na sio watu au taifa. Taifa ni ni kundi la watu waliokubaliana na mfumo wa uongozi na wakae kwa pamoja. Kwenye biblia unaona kabila linageuka kuwa Taifa au familia kuwa taifa. (Angalia katika Kitabu cha Mwanzo 49)

 Mwanzo 49:1,28

­"Yakobo akawaita wanawe, akasema, Kusanyikeni, ili niwaambie yatakayowapata siku za mwisho.Hizo zote ndizo kabila za Israeli kumi na mbili. Na hayo ndiyo aliyowaambia baba yao, na kuwabariki; mmoja mmoja kwa mbaraka wake aliwabariki"

 Hapa biblia haizungumzii uponyaji wa watu bali ni ardhi .Biblia inasema tena nikiamuru nzige kula nchi maana nzige ni wadudu waharibifu na wanaoharibu mazao au udongo na Tauni ni ugonjwa wa kuambukiza na kibiblia ikitokea ugonjwa wa kuambukiza ina maana kunakuwa na shida kwenye ardhi.

 Ukitokea ugonjwa wa kuambukiza katika eneo fulani huwa wanaweka karantini na kufunga mipaka. Kitendo cha kuweka mpaka ni Roho Mtakatifu anawajulisha kuwa shida hii imeishia mpaka hapa.

 Suala hili la kufunga mipaka ili kuzuia maambukizo ya ugonjwa ni ya kiroho kwanza kabla hayajawa ya kimwili.

 MFANO WA NNE

Yeremia 22:29-30

"Ee nchi, nchi, nchi, lisikie neno la Bwana. Bwana asema hivi, Andikeni habari za mtu huyu kwamba hana watoto, kwamba mtu huyu hatafanikiwa siku zake zote; maana hapana mtu katika wazao wake atakayefanikiwa, akiketi katika kiti cha enzi cha Daudi, na kutawala tena katika Yuda."

 Huyu ni Mungu anazungumza na nchi (ardhi yenye mipaka halali ya kiumiliki) anaposema

Ee nchi ,nchi sikia ---- ina maana nchi inasikia

Andika maana yake inaweza tunza kumbukumbu

Kuwa hatafanikiwa maana yake ni kuwa inaweza fuatilia

 Wakati adhabu inatolewa kwa mtu huyu alikuwa bado hana watoto, lakini kumbukumbu iliandikwa kwenye ardhi kuwa hata watoto wake wakija nao wasifanikiwe. Adhabu ilitolewa kwa sababu gani; angalia mstari wa 21 Mimi nalisema nawe wakati wa kufanikiwa kwako; lakini ulisema, Sitaki kusikia. Hii ndiyo iliyokuwa desturi yako tangu ujana wako, kutokuitii sauti yangu.

 Fikiria wewe ni mtoto na umeingia kwenye adhabu ya baba au mama na unatafuta kufanikiwa na haufaninikiwi sio kwamba akili huna bali unazo lakini umezuiliwa kufanikiwa na ardhi kwa sababu ya kosa la baba yako na mama yako je unaombaje?

 MFANO WA TANO

Mwanzo 28: 10-20

"10-13"Yakobo akatoka Beer-sheba , kwenda harani. Akafika mahali Fulani akalala huko usiku kucha , maana jua lilikuwa limekuchwa ,akatwaa jiwe moja la mahali pale akaliweka chini ya kichwa chake , akalala usingizi palapale. Akaota ndoto, na tazama ngazi imesimamishwa juu ya nchi, na ncha yake yafika mbinguni .Tena tazama malaika wanapanda na kushuaka juu ya yake. Na tazama Bwana amesimama juu yake , akasema mimi ni Bwana, Mungu wa Ibrahim baba yako na Mungu wa Isaka , nchi hii uilalayo ntakupa wewe na uzao wako"

 Lile Neno nchi hii ulalayo Kwa lugha nyingine ardhi unayolala iwe ni nyumba uliyojenga au hoteli au umejilaza mahali kwa muda mfupi au ni kwenye basi umelala au uko shambani umelala na ghafla unaota ndoto, sio kila mahali angeweza kulala ila eneo lile lilikuwa na umiliki kamili wa Mungu.

 MFANO WA SITA

2 Samweli 21:1

"Kulikuwa na njaa siku za Daudi muda wa miaka mitatu , mwaka hadi mwaka naye Daudi akautafuta uso wa Bwana , Bwana akasema ni kwa ajili ya Sauli na nyumba yake yenye damu kwa kuwa aliwaua hao wagibeoni­"

 Daudi katika kipindi chake cha uongozi kulitokea shida ya njaa na ilidumu kwa muda wa miaka mitatu. Na alikuwa hajaomba kutafuta sababu na alishindwa kuhusianisha kati ya hali ya kiroho ya ardhi na shida ya njaa iliyotokea.

 Kama ardhi imekugomea jaribu kupanda mahindi na maua na baada ya muda utaona mahindi yananyauka lakini maua yanastawi. ukimuita mtalaamu wa kilimo ataanza kupima unyevu na atakuelekeza na sababu za kitalaam, lakini shida ni kuwa kunakuwa na kitu kwenye ardhi ambacho hakipo sawa.

 MFANO WA SABA

Ufunuo 12:12- 15

"Kwa hiyo shangilieni; enyi mbigu ,nanyi mkaao humo ole wanchi na bahari ! kwa maana Yule ameshuka kwenu kwenye ghadhabu nyingi akijua ya kuwa ana mda mchache tu. Na Yule joka alipoona ametupwa katika nchi alimwudhi mwanamke Yule aliyezaa mtoto mwanaume. Mwanamke Yule akapewa mabawa mawili ya tai Yule mkubwa ili aruke aende zake nyikani , hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati mbali na nyoka huyo,Nyoka akatoa katika kinywa chake nyuma ya huyo mwanamke maji kama moto amfanye kuchukuliwa na mto ule"

 Huyu mama angejuaje kuwa kufanikiwa kwake kulitegema sana msaada wa ardhi ambayo uliumeza mto uliotolewa na Joka. Kwa hiyo hakikisha kila ardhi iko upande wako, iwe ni ya kanisa au unapolala au unapofanya biashara.

 kwenye semina zetu kuwa tunahakikisha mbingu na ardhi inakaa upande wetu ili kumzuia shetani.

 Sasa hujiulizi kwanini kambi nyingine huwa wanachimbia hiziri ardhini?. Jibu ni rahisi kabisa kuwa wanataka msaada wa ardhi

 Kwani wanapofanya mambo ya mila wanapoweka maziwa mdomoni na kuweka na kutemea juu na chini kwenye ardhi wanakuwa wanatafuta nini, wanatafuta msaada wa mbingu na nchi.

 MFANO WA NANE

Yoel 1:9-13

"Sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji Zimekatiliwa mbali na nyumba ya Bwana; Hao makuhani, wahudumu wa Bwana, wanaomboleza. Shamba limeharibika, nchi inaomboleza; maana nafaka imeharibika, divai mpya imekauka, mafuta yamepunguka. Tahayarini, enyi wakulima; Pigeni yowe, enyi watunzaji wa mizabibu; Kwa ajili ya ngano na shayiri, Maana mavuno ya mashamba yamepotea. Mzabibu umesinyaa, mtini nao umevia; Nao mkomamanga na mtende na mtofaa; Naam, miti yote ya mashamba imekauka; Maana furaha imekauka katika wanadamu. Jikazeni mkaomboleze, enyi makuhani; Pigeni yowe, enyi wahudumu wa madhabahu; Njoni mlale usiku kucha katika magunia, Enyi wahudumu wa Mungu wangu; Kwa kuwa sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji Zimezuiwa katika nyumba ya Mungu wenu"

 Unaombaje ikiwa hali ya kiroho ya ardhi imesababisha kuzuiwa kwa sadaka kanisani. Mungu kakataza sadaka ili waombaji waombe ili hali zao za Uchumi ziwe vizuri na watoe sadaka.

 Na kama unafanya semina au mkutano wa nje kama sisi usipojua namna ya kuombea ardhi utakuta watu wanarudi na sadaka nyumbani kwao kwa sababu hali ya kiroho ya ardhi ina uhusiano mkubwa sana na utoaji wa sadaka kwa watu

 MFANO WA TISA

Kumbukumbu la torati 8:7,12

"Kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yuakuingiza katika nchi nzuri, nchi yenye vijito vya maji, na chemchemi, na visima, vibubujikavyo katika mabonde na milima; Angalia, utakapokuwa umekula na kushiba, na kujenga nyumba nzuri na kukaa ndani yake;"

 Kuna uhusianio na Baraka za Mungu na watu waliongizwa kwenye eneo lenye mipaka halali ya kiumiliki. Ndio maana kati ya adhabu mojawapo inaifikia nchi ni miji kubomolewa au kukosa wakazi, kuwa ukiwa.

 Sasa unaweza jiuliza swali hili gumu kuwa kwanini Sauli hakupata adhabu yeye katika kipindi chake baada ya kuwaua wagebeoni. Lakini aliyepata madhara ni Daudi, kwa hiyo si tu kwamba Daudi alirithi kiti bali na ile adhabu iliyokuwa kwenye kiti. Pia kuna uhusiano gani uliopo kati ya ardhi na cheo kosa la kiti na kosa la mtu aliyekaa kwenye kiti na kosa la kiti.

 Kosa la kiti adhabu yake atapata kila mtu atakayekaa kwenye kiti, kwa hiyo kumfukuza kwa jinsi ya mwili kwa sababu amekosea haitatui tatizo la kiroho lililofanya akakose mtu mwingine atakayekuja atajikwaa palepale alipojikwaa wa kwanza.


MUNGU AKUBARIKI SANA

MAOMBI NA MAOMBEZI

 

 

Post a Comment

0 Comments