Follow us

MAMBO YANAYOTOKEA UKIISHI KATIKA MAOMBI

Tangazo

 

MCHUNGAJI LAURENT MPOMA
NCHI YA UKOMBOZI MINISTRY
(HEMA LA MAOMBI NA MAOMBEZI)

MAMBO YANAYOTOKEA UKIISHI KATIKA MAOMBI

Nguvu na Matokeo Makubwa Kwenye Maombi haipo Kwenye KUOMBA Bali NIDHAMU KUBWA KATIKA KUOMBA KWA MWENDELEZO

Kwa sababu Kanuni Mojawapo inayosababisha Na Kuleta Matokeo Makubwa Kwenye Maombi ni NIDHAMU ALIYONAYO MTU YA KUOMBA KWA MWENDELEZO

Sasa nataka tuangalie kidogo Mambo kadhaa Yanayotokea Pale Mtu anapoishi Maisha Ya Maombi Kwa MWENDELEZO

(1) MAISHA YA MAOMBI  HUSABABISHA MTU APATE MAJIBU YAKE KUTOKA KWA BWANA

Luka 11:8

[8]Nawaambia ya kwamba, ijapokuwa haondoki ampe kwa kuwa ni rafiki yake, lakini kwa vile asivyoacha kumwomba, ataondoka na kumpa kadiri ya haja yake.

Hakuna Namna ambavyo utaishi Maisha Ya Maombi Kwa MWENDELEZO halafu usipate Majibu Yako Kutoka Kwa MUNGU Kwa Yale ambayo unayaombea

Unapokuwa na Maisha Ya MWENDELEZO Katika Maombi ni lazima tu utakuwa ni Mtu mwenye kujibiwa na BWANA

(2) MAISHA YA MAOMBI HUSABABISHA UWEPO WA MUNGU KUYAZINGIRA MAISHA YAKO

Zaburi 91:1

[1]Aketiye mahali pa siri pake Aliye juu

Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.

Hakuna namna ambavyo utaishi Maisha Ya Maombi Kwa MWENDELEZO halafu Uwepo Wa MUNGU Usiwe Pamoja nawe

Hakuna namna ambavyo utaishi Maisha Ya Maombi Kwa MWENDELEZO halafu Uwepo Wa MUNGU Usiwe halisi Kwenye Maisha Yako

Maana unapokuwa na Nidhamu Kubwa kuhakikisha Kila Siku ,Kila Siku unakuwa na Muda mwingi Sana Wa KUOMBA hiyo hali Huwa inatengeza Uwepo Wa MUNGU Kuwa Halisi na Kuyazingira Maisha Yako

(3) MAISHA YA MAOMBI HUSABABISHA USHINDI HAIJALISHI UTAKUTANA NA NINI

Kama nilivyosema Kwenye point namba 2 Kuwa Ukiishi Maisha Ya Maombi Kwa MWENDELEZO Huwa Uwepo Wa MUNGU unakuwa nawe

Sasa huo Uwepo Wa MUNGU Huwa unasababisha Upate Ushindi Haijalishi utakutana na Nini , Haijalishi utasongwa na Nini

Aaah kilichompa Ushindi Daniel Kwenye tundu la simba ni ILE NIDHAMU KUBWA ALIYOKUWA NAYO YA KUOMBA KWA MWENDELEZO

Daniel alikuwa anaomba mara 3 Kwa Siku Kila Siku,Kila Siku Haijalishi Yuko busy namna gani

Ndugu Yangu Ukiishi Maisha Ya Maombi Kwa MWENDELEZO Haijalishi vita gani ambazo zinawaangusha Wengine Wewe haitakuangusha Kamwe , Haijalishi Majaribu na Changamoto Gani zitakuja mbele Yako ni lazima tu UTAZISHINDA

DANIEL 6:10 , WARUMI 8:37

(4) MAISHA YA MAOMBI HUSABABISHA UWE MBABE KWA SHETANI NA MAWAKALA WAKE

Kamwe Huwezi Kuwa mbabe Kwa Shetani kama hauishi Maisha Ya Maombi

Kamwe hauwezi Kuwa mbabe Kwa Shetani kama una Maombi Ya mara Leo umeomba, Kesho hauombi

Lakini Ukiishi Maisha Ya Maombi Kwa MWENDELEZO Kwa Muda mrefu aah lazima Nguvu za Giza zitakuogopa , lazima Nguvu za Giza zitakukimbia

Maana utakuwa umezungwa na Uwepo na Utukufu Mwingi Wa MUNGU

(5) MAISHA YA MAOMBI HUSABABISHA KUISHI MAISHA MBALI NA HOFU ,MASHAKA , WOGA

Ukiishi Maisha Ya Maombi Kwa MWENDELEZO unatengeneza Uwepo Wa MUNGU Kuwa nawe

Na ule Uwepo Wa MUNGU unasababisha Uwe na ujasiri usiyo Wa kawaida, unasababisha Uwe na Imani isiyo Ya Kawaida

Na Hofu, mashaka, wasiwasi, woga vinakuwa mbali nawe

2 Timotheo 1:7

[7]Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.

Huwezi kukuta Mtu anayeishi Maisha Ya Maombi Kwa MWENDELEZO halafu akawa mwoga mwoga , halafu akawa na mashaka mashaka , Halafu Hofu zikamtawala

(6) MAISHA YA MAOMBI HUSABABISHA USHINDI DHIDI YA KILA DHAMBI

Hakuna Dhambi Yenye Nguvu Ya kumtawala ,kumuendesha Mtu anayeishi Maisha Ya Maombi Ya MWENDELEZO

 

MUNGU AKUBARIKI SANA KUFUATILIA BLOG HII

 

NAITWA MCHUNGAJI LAURENT MPOMA

NCHI YA UKOMBOZI MINISTRY

(HEMA LA MAOMBI NA MAOMBEZI)

KWA MAHITAJI PIGA AU TUMA UJUMBE HAPA 0714890889

WHATSAP: 07627576542

 

>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>> 

TUMA MAHITAJI YAKO KWA NAMBA HAPO JUU.

UNAWEZA KUCHANGIA SADAKA YAKO KWA AJILI YA UJENZI WA KANISA KATIKA VITU VIFUATAVYO:

1.        VITI 20 @ 20,000/=

2.        MAIKI 2= 150,000/=

3.        ENEO LA KANISA  500,000/=

4.        SIKA 2 = 1900,000/=

5.        VITAMBAA VYA MADHABAHU.= 100,000/=

TIGO PESA: +255714890889................JINA: LAURENT MPOMA

M-PESA: +255762756542.....................JINA: LAURENT MPOMA

AIRTEL MONEY: +255782859946.........JINA: LAURENT MPOMA

MCHUNGAJI ATAKUOMBEA .

MUNGU AKUBARIKI SANA WEWE UNAYECHANGIA KWA AJILI YA MUNGU NA AKUFUNGULIE MALANGO YAKO YA UCHUMI.

 

 

Post a Comment

0 Comments