Follow us

KUJITOA KWENYE VIFUNGO VYA MANENO MABAYA

Tangazo

 

MCHUNGAJI LAURENT MPOMA
NCHI YA UKOMBOZI MINISTRY 

KUJITOA KWENYE VIFUNGO VYA MANENO MABAYA

4 Je! Umetamka maneno kwa nani? Kisha ni roho ya nani iliyotoka kwako?

Ayubu 26 :4

Neno lolote ulilotamkiwa ni roho

Kama neno hilo ni roho basi ujue kuwa unenewa linafanya kazi maishani mwako sawasawa na lilivyotamkwa.

kwa kuwa neno ni roho , neno lolote baya ulilotamkiwa ujue linakamata mfumo mzima wa maisha yako .

Tambua kuwa neno baya ukitamkiwa ile roho ya uharibifu inakuja kwako kukukamata.

Ukitamkiwa kutokufanikiwa huwezi kufanikiwa kweli kama hujalitubia hilo neno na kulikata lisikukamate .

2 Basi umetegwa kwa maneno ya kinywa chako, Umekamatwa kwa maneno ya kinywa chako,

Mithali 6 :2

 Maneno yanakamata na pia yanashika

Neno lolote la kushindwa ukitamkiwa kama anayekutamkia unamsikia mkanye hapo hapo mwambie maneno yake hayatasimama usipofanya hivo yatathibitika kwako

Kama ulitamkiwa na mtu hutakaa uoe au hutakaa uolewe tambua kuwa unanafasi ya kutubu juu ya maneno hayo na kuyafuta kabisa yasifuatilie maisha yako

Kuna wakati unaweza kuona kuwa mume uliyenaye au mke uliye naye siyo sahihi kwako kumbe kuna mtu alikutamkia kuwa hutakaa kwenye ndoa yako ukaifurahia .

 Ndoa nyingi zinaingia migogoro kwa sababu ya maneno mabaya yaliyotamkwa juu yake .

 29 Ee nchi, nchi, nchi, lisikie neno la Bwana.

Yeremia 22 :29

30 Bwana asema hivi, Andikeni habari za mtu huyu kwamba hana watoto, kwamba mtu huyu hatafanikiwa siku zake zote; maana hapana mtu katika wazao wake atakayefanikiwa, akiketi katika kiti cha enzi cha Daudi, na kutawala tena katika Yuda.

Yeremia 22 :30

Itazame hiyo familia imetamkiwa kutokufanikiwa kabisa

Utaona ardhi ( nchi) imetekeleza yale matamko na kuwafanya watu wakaao hapo kutokufanikiwa kabisa .

Lazima uyafute maneno yote mabaya uliyotamkiwa na watu kwa kusikia na kwa kutokusikia .

Ninakwambia ujifungue utoke kwenye vifungo vya maneno nikimaanisha kuwa neno lolote ukitamkiwa ujue linaumba .

1 Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.

Mwanzo 1 :1

2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.

Mwanzo 1 :2

3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru.

Mwanzo 1 :3

Tambua kuwa Mungu aliumba vitu vyote kwa neno

 1 Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.

Yohana 1 :1

2 Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.

Yohana 1 :2

3 Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.

Yohana 1 :3

4 Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu.

Yohana 1 :4

5 Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza.

Yohana 1 :5

Kwa maana hii basi mtu akikutamkia neno litakuwa sehemu ya maisha yako usipolifuta kwa maombi( toba ).

9 Maana Yeye alisema, ikawa; Na Yeye aliamuru, ikasimama.

Zaburi 33 :9

10 Bwana huyabatilisha mashauri ya mataifa, Huyatangua makusudi ya watu.

Zaburi 33 :10

Neno lolote ukijitamkia au kutamkiwa linasimama juu yako

Ukijitamkia kushindwa utashindwa kweli kweli .

 

Bwana Yesu , ninakuja mbele zako .

Ninakuomba unisamehe maana nimejitamkia maneno mabaya ya kushindwa.

Nirehemu ee BWANA , maana sikukujua lakini sasa nimejua makosa yangu juu ya maneno mabaya niliyojitamkia.

Nakuomba uyafute maneno mabaya niliyojitamkia katika maisha yangu , katika jina la Yesu .

Ninaomba uwasamehe hata wale walionitamkia maneno mabaya juu ya familia yangu , biashara zangu, ndoa yangu , elimu yangu n.k

Ee Mungu uyafute maneno yao mabaya , waliyonitamkia kwa kujua na kwa kutokujua. Kwa damu ya Yesu futa maneno yao kuanzia sasa , maana imeandikwa:

10 Bwana huyabatilisha mashauri ya mataifa, Huyatangua makusudi ya watu.

Zaburi 33 :10

11 Shauri la Bwana lasimama milele, Makusudi ya moyo wake vizazi na vizazi.

Zaburi 33 :11

Nami nakuomba maneno niliyotamkiwa uyafutilie mbali katika maisha yangu , familia yangu , ndoa yangu n.k bali neno lako likasimame daima maishani mwangu katika jina la Yesu .Amen

Katika jina la Yesu , ninasema kama ilivyoandikwa;

7 Bwana MUNGU asema hivi, Neno hili halitasimama wala halitakuwa.

Isaya 7 :7

Ninaamuru kila maneno mabaya kutokusimama katika maisha yangu na ndoa yangu , familia yangu , elimu yangu n.k

10. Fanyeni shauri pamoja, nalo litabatilika; Semeni neno, lakini halitasimama; Kwa maana Mungu yu pamoja nasi.

Isaya 8 :10

ninayaamuru maneno yote mabaya niliyotamkiwa na niliyotamkiwa kuwa batili , katika jina la Yesu.

Ninaamuru kila maneno mabaya na roho ya uharibifu kuachia maisha yangu , katika jina la Yesu nina yavua mavazi ya maneno mabaya kwa damu ya Yesu .

22 Na katika Torati karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na pasipo kumwaga damu hakuna ondoleo.

Waebrania 9 :22

Asante Bwana Yesu kwa kuwa unasikia kuomba kwangu nami najikabidhi mikononi mwako sasa na hata milele .Amen

 

MUNGU AKUBARIKI SANA KWA KUENDELEA KUFUATILIA BLOG HII NA KUJIFUNZA ZAIDI.

MAOMBI NA MAOMBEZI

WASILIANA NA MCHUNGAJI LAURENT MPOMA

PIGA 0762756542

WHATSAP: +255762756542

Post a Comment

0 Comments