Follow us

SOMO: MBINU ZA MAFANIKIO YA KIROHO NA KIMWILI

Tangazo

 

MCHUNGAJI LAURENT MPOMA

SOMO: MBINU ZA MAFANIKIO YA  KIROHO NA KIMWILI

1. IMARISHA FAHAMU YA IMANI

–Pasipo Imani haiwezekani kumpendeza Mungu, Imani ni kutokuwa na mashaka akilini mwako. Zaidi ya milango mitano ya fahamu yaani kuona, kunusa, kuonja, kusikia na kuhisi LAKINI Imani ni mlango wa sita (Japokuwa kwangu Mimi Gustaph ni wakwanza). Maisha yakijawa na Imani kwa kila jambo unalofanya huwezi kukwama.. 2Petro 1:5-8

“Kwa sababu hii, jitahidini sana kuongeza wema katika imani yenu; na katika wema ongezeni maarifa;  na katika maarifa ongezeni kiasi; na katika kiasi ongezeni ustahimilivu; na katika ustahimilivu ongezeni kumcha Mungu;  na katika kumcha Mungu ongezeni upendano wa kindugu; na katika upendano wa kindugu ongezeni upendo.  Maana mkiwa na sifa hizi kwa wingi zitawawe zesha kuwa wenye bidii na wenye kuzaa matunda katika kumfahamu Bwana wetu Yesu Kristo.

-katika Imani yenu tieni na WEMA, wewe amua kuweka wema maana hii ni kazi yako, usiseme Mimi ndivyo nilivyo, KATAA UBAYA

2. JIHESABU KAMA MUNGU ANAVYOKUHESABU.

Hapo sasa ni kuweka nia ya Kristo katika MWENDO. Wafilipi 4:13 ”Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu”.

-Umekubali kutembea kandokando ya mto, basi utakutana na bahari unayohitaji. Nia yako lazima iungwe mkono kwa vitendo. Kutokuruhusu nia itafsiriwe kwa vitendo ndiko kunakomtofautisha mtu anayefanikiwa na ambaye hafanikiwi. Wengi wakiruhusu matendo  yao yafunue nia zao za kufànikiwa watakuwa na maendeleo makubwa.

3. BATILISHA FIKRA ZA KITOTO NA UAMUE KUKUA.

1wakorinto 13:11 “Nilipokuwa mtoto mchanga, nilisema kama mtoto mchanga, nalifahamu kama mtoto mchanga, nalifikiri kama mtoto mchanga, tokea hapa nilipokuwa mtu mzima; nimeyabatilisha mambo ya kitoto”.

Paulo anasema alipokuwa sasa, yaani tokea amekuwa mtu mzima amebatilisha fikra za kitoto. Maana ya kubatilisha ni kukichukua kitu na kukiweka pembeni kwa lengo la kutokukitumia tena, kimekuwa batili ina maana hakiruhusiwi kutumika tena na inatakiwa sasa hapo kikae mbali kidogo.

1Wakorinto 14:20  ”Ndugu zangu, msiwe watoto katika akili zenu, lakini katika uovu mgeuzwe watoto wachanga, Bali katika akili zenu mkawe watu wazima”.  -Utoto unaozungumziwa hapa ni utoto wa akili, soma Waefeso 4:14.

4. USIKATAE FURSA ZA KUWA MDOGO.

Mathayo 20:26-27 “Lakini haitakuwa hivyo kwenu, bali mtu yeyote anayetaka kuwa mkubwa kwenu na awe mtumishi wenu; Na mtu yeyote anayetaka kuwa wa Kwanza kwenu na awe mtumwa wenu”.

-Anza kuwatumikia wengine kwanza, anza kuwapatia MEMA wanayopenda kwanza na utakuwa umewatawala bila wao kujijua. Angalia wafalme walivyojishusha na walivyofanikiwa, mfano Yesu Kristo.

5. UNALOTAKA UTENDEWE WATENDEE KWANZA WENGINE.

Mathayo 7:12 ” Basi yoyote mtakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo; maana hiyo ndiyo torati na manabii”.

–Mara nyingi watu WEMA wanabeba mizigo mingi kupita kawaida, kubali kufunua hekima zako kupitia uvumilivu ili uwavute waamini unachoelewa. Au yafaa nini mwanadamu unapenda kuheshimiwa halafu wewe huheshimu wenzako?

“DAWA YA MOTO NI MAJI”, kwanini ubebe moto kifuani mwako ili uzime moto uliowashwa na mwenzako?.

6. FANYA JAMBO ZURI UNALOLIHOFU.

Hofu na mashaka ni silaha kubwa sana ambayo shetani huitumia kuwafanya watu washindwe kupata majibu ya maombi ya miujiza yao kutoka kwa MUNGU. Shetani anafahamu kwamba imeandikwa;

” Mwenye haki wangu ataishi kwa imani, naye akisitasita Roho yangu haina furaha naye” (Waebrania 10:38).

Dawa kubwa ya hofu ni Imani (Marko 11:22). Unapohofia baya usilolihitaji ni ushindani kati ya mwili na imani, iite roho; inajua hilo ni baya, mwili unadai ni zuri. Thibitisha kuwa ni baya kwa kuliacha. Aina za hofu ni pamoja na kukosolewa, kuchekwa, umaskini, kufilisika, kuachishwa kazi,kustaafu, kufiwa n.k

7. IMARISHA UNYOOFU WAKO/UAMINIFU.

Ukiwa mnyoofu, mwaminifu utasaidiwa na kila MTU,utawekwa juu ya Mali nyingi na watu wengi (utawaongoza VIZURI).

Mwanzo 41:37-44 “Neno hilo likawa jema machoni pa Farao na machoni pa watumishi wake wote.  Farao akawaambia watumishi wake: “Farao akawaambia watumwa wake, Tupate wapi mtu mwingine kama huyu mwenye Roho wa Mungu ndani yake?. Farao akawaambia Yusufu kwa kuwa Mungu amekufahamisha hayo yote, hapana mwenye akili na hekima kama wewe. Basi wewe utakuwa juu ya nyumba yangu, na kwa neon lako watu wangu watatawaliwa katika kiti cha enzi tu nitakuwa mkuu kuliko wewe. Farao akawaambia Yusufu, tazama nimekuweka juu ya nchi yote ya Misri. Farao akavua pete yake ya muhuri mkononi mwake akaitia mkononi mwa Yusuph; akamvika mavazi ya kitani nzuri na kumtia mkufu wa dhahabu shingoni wake. Akampandisha katika gari lake lile la pili alilokuwa nalo na watu wakapiga kelele mbele yake……”

Katika maisha unaweza kuwadanganya wengi sana, lakini huwezi kuwadanganya hawa wawili yaani nafsi yako na Mungu wako. Ukiwa mnyoofu kwa hawa wawili utapata mafanikio makubwa sana.

8. ONA UNACHOTAKA KUPITIA HICHO KIDOGO ULICHONACHO SASA.

-Kama unataka upate amani, furaha, upendo,afya n.k Ione amani, furaha, upendo au afya hiyo NDANI ya moyo wako kwanza. Hivyo ndivyo kupanda mbegu ya mafanikio kulivyo. Kama moyoni mwa mtu hakuna anachotaka, atakipataje?

Tujifunze kwa Mama huyu katika 2Wafalme 4:1-6 “Basi mwanamke mmoja miongoni mwa wake za wana wa manabii alimlilia Elisha, akasema mtumishi wako mme wangu amekufa; nawe wajua ya kuwa mtumishi wako alikuwa mcha BWANA; na aliyemwia amekuja ili ajitwalie wana wangu wawili kuwa watumwa. Elisha akamwambia, nikufanyie nini?, Niambie; una kitu gani nyumbani.

Mungu akubariki sana

MAOMBI NA MAOMBEZI

MCHUNGAJI LAURENT MPOMA

0762756542

WATSAP: 0762756542

YOUTUBE: Upenyo Wa Mungu Tv


Post a Comment

0 Comments