SOMO: ZIJUE FAIDA ZA KUMTUMIKIA MUNGU
“Mtu akinitumikia, na
anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu
akinitumikia, Baba atamheshimu”. Yohana 12:26
Kumtmikia Bwana ni nini?
Kumtumikia
Mungu sio kuwa mchungaji, mwinjiristi, muhubili, mwimbaji, nabii, mtume n.k.
bali kuna zaidi ya hapo. Kuna tafsiri mbalimbali za kibiblia zinazoelezea maana
ya kumtumikia Mungu. Na baadhi ya maana hizo ni kama ifuatavyo;
1. Kumwabudu Mungu na kumsujudu
yeye peke yake.
Ukiamua
kumtumikia Mungu sio kuomba tu au kuhubili tu bali ni kumsujudia Mungu na
kumwabudu yeye peke yake. Tunainama kwa Yesu peke yake na wala sio kwa watu,
mizimu, waganga, mashetani n.k. bali tunainama kwa Yesu pekee.
“Nanyi mtamtumikia
Bwana, Mungu wenu, naye atakibarikia chakula chako, na maji yako; nami
nitakuondolea ugonjwa kati yako”.Kutoka 23:25
”Kwa kuwa ulikuwa wa thamani machoni pangu, na mwenye
kuheshimiwa, nami nimekupenda; kwa sababu hiyo nitatoa watu kwa ajili yako; na
kabila za watu kwa ajili ya maisha yako”. Isaya 43:4
“Yesu akamjibu, Imeandikwa ya kwamba mtu hataishi kwa mkate
tu. Akampandisha juu, akamwonyesha milki zote za ulimwengu kwa dakika moja.
Ibilisi akamwambia, Nitakupa wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwa kuwa imo
mikononi mwangu, nami humpa ye yote kama nipendavyo”. Luka 4:4-6
2. Kumtii na kumtegemea yeye
pekee.
Maana nyingine
ya kumtumikia Mungu ni kumtii na kumtegemea yeye pekee, ukimfanya mwanadamu
kuwa tegemeo lako na moyoni mwako umemwacha Mungu basi ujue kwamba umeliwa.
Haimaanishi kwamba usitegemee msaada kutoka kwa mtu hapana bali unatakiwa
kumtegemea Mungu moyoni mwako, kumtii yeye pekee kisha Yeye anatoa watu kwa
ajili yako. Kama mtu hana tegemeo lingine utamwona kanisani masaa yote yaani
Mungu atakuwa ndio tegemeo lake lakini kama moyoni mwake hakuna Mungu basi
utamwona anategemea fedha, kazi, elimu yake n.k. na moyoni mwake amemwacha
Mungu.
“Kama
mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi”; Isaya 1: 19
3. Kuwa na bidii katika kufanya
kazi za Mungu.
Kazi za Mungu
zipo nyingi sana sio kuhubili pekee. Mungu alipomwumba mwanadamu alimpa kazi ya
kufanya duniani, unapokuwa na bidii katika kuifanya kazi yake, ukikamata kanuni
ya Mungu ambayo ni biblia na kuyafanya yale yaliyoagizwa humo basi unakuwa
unamtumikia Mungu. Kwenye nchi kuna kitu kinaitwa ilani hii ni lazima iendane
na katiba ya nchi na sisi katiba yetu ni neno la Mungu ambalo ndio sheria ya
Mungu ndani ya katiba kuna maagizo ya Mungu ambayo tunatakiwa kuyafanya.
Kuzishika sheria za Bwana na kuzifanyia kazi ni kumtumikia Bwana.
“Lakini
mjibidiishe sana kuzifanya amri na sheria, ambazo Musa, mtumishi wa Bwana,
aliwaamuru, kumpenda Bwana, Mungu wenu, na kwenenda katika njia zake zote, na
kuzishika amri zake, na kushikamana na yeye, na kumtumikia kwa moyo wenu wote
na nafsi yenu yote”. Yoshua 22:5
Ukiizishika sheria za Bwana na kuzitenda ndio utumishi huo
haikuhitaji uwe mchungaji. Unapowaleta watu nyumbni mwa Bwana umewajari na
kuitimiza sheria ya Bwana. Yesu alipokuja duniani hakufungua shule kwa ajili ya
kuwafundisha watu, hakuja kufungua kituo kwa kulelea watoto yatima n.k. alikuja
kuondoa mapepo na ndio maana akawaita theneshara akawapa amri juu ya pepo wabaya
ili kwamba wawatoe, unapofanya kwa bidii kazi ya kumtumikia Bwana maana yake
unaishika sheria ya Bwana na kuwaleta watu nyumbani mwa Bwana kwa jina la Yesu
Kristo.
“Palikuwa na mtu Kaisaria, jina lake Kornelio, akida wa
kikosi kilichoitwa Kiitalia, mtu mtauwa, mchaji wa Mungu, yeye na nyumba yake
yote, naye alikuwa akiwapa watu sadaka nyingi, na kumwomba Mungu daima. Akaona
katika maono waziwazi, kama saa tisa ya mchana, malaika wa Mungu, akimjia na
kumwambia, Kornelio! Akamtazama sana, akaogopa akasema, Kuna nini, Bwana?
Akamwambia, Sala zako na sadaka zako zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za
Mungu…….” Matendo 10:1-37
FAIDA ZA KUMTUMIKIA BWANA.
1. Kuokolewa kutoka gerezani ki
muujiza.
“Akaondoka
Kuhani Mkuu na wote waliokuwa pamoja naye, (hao ndio walio wa madhehebu ya
Masadukayo), wamejaa wivu, wakawakamata mitume wakawaweka ndani ya gereza;
lakini malaika wa Bwana akafungua milango ya gereza usiku, akawatoa, akasema”,
Matendo 5:17-19
Magereza yapo mengi sana yapo ya mateso, kukosa fedha,
kukataliwa n.k. wanaokaa gerezani ni wafungwa na kufungwa ni kunyimwa uhuru wa
kutenda. Mfungwa siku zote huwa anachaguliwa nini cha kula kwa kuwa anakuwa
hana uwezo wa kuamua, unaweza ukawa kwenye kifungo cha uchumi yaani unakosa
fedha hata ya kununua chakula. Leo hii ukiamua kumtumikia Mungu anakutoa kutoka
kwenye gereza ulilo fungwa kwa jina la Yesu Kristo.
2. Kutoka kwenye mikono ya
farao.
Kila mtu ana
farao wa maisha yake, Farao ni ishara ya shetani anawakilisha shetani. Wana wa
Israeli waliteseka sana wakatekwa na kuwekwa kwenye mikono ya farao, walikuwa
watumwa miaka mia nne. Mungu alijua kwamba watu wale wanatakiwa kwenda kwenye
nchi ya starehe yaani nchi ya ahadi lakini hatari yake ni kwamba walikuwa
hawaendi. Kuna sehemu leo hii unahitaji kwenda lakini huendi kwa sababu ya
farao wa maisha yako amekuzuia leo hii njia pekee ni kumtumikia Bwana.
“Kwa kuwa
Bwana, Mungu wako, yuakuingiza katika nchi nzuri, nchi yenye vijito vya maji,
na chemchemi, na visima, vibubujikavyo katika mabonde na milima”; Torati 8:7
Kuna mahali ni
pazuri sana ambako unatakiwa kwenda, maisha yako yanatakiwa kuwa mazuri lakini
leo hii huyaishi wala huyafikirii kwa sababu ya farao aliyekuzuia ili kwamba
usiende. Nchi ambayo Bwana amekuaidia kuna mambo mengi mazuri ni mahali pazuri
sana lakini farao amekuzuia kwa nguvu zote hataki kukuachia lakini faida ya
kumtumikia Bwana ni kwamba Bwana akuondoa kwenye shida, mateso, akutoe kwenye
mikono ya farao ili kwamba uishi maisha mazuri.
“Nawe umwambie
Farao, Bwana asema hivi, Israeli ni mwanangu mimi, mzaliwa wa kwanza wangu;
nami nimekuambia, Mpe mwanangu ruhusa aende, ili apate kunitumikia, nawe
umekataa kumpa ruhusa aende; angalia basi, mimi nitamwua mwanao, mzaliwa wa
kwanza wako”. Kutoka 4:22-23
Mungu alimtuma
Musa aende kwa farao ili kwamba amwambie awaache watu wa Mungu yaani wana wa
Israeli ili kwamba waende wakamtumikie Bwana kanaani.
“Bwana
akamwambia Musa, Ondoka asubuhi na mapema, ukasimame mbele ya Farao, umwambie,
Bwana, Mungu wa Waebrania, asema, Wape watu wangu ruhusa waende ili
wanitumikie”. Kutoka 9:13
3. Mungu atabariki chakula na
maji
“Nanyi
mtamtumikia Bwana, Mungu wenu, naye atakibarikia chakula chako, na maji yako;
nami nitakuondolea ugonjwa kati yako”. Kutoka 23:25
“Kwa hiyo Bwana MUNGU asema hivi, Tazama, watumishi wangu
watakula, bali ninyi mtaona njaa; tazama, watumishi wangu watakunywa, bali
ninyi mtaona kiu; tazama, watumishi wangu watafurahi, bali ninyi mtatahayarika;
tazama, watumishi wangu wataimba kwa furaha ya moyo, bali ninyi mtalia kwa
huzuni ya moyo; mtapiga kelele kwa sababu ya uchungu wa roho zenu”. Isaya
65:13-14
4. Ukimtumikia Bwana anaondoa
ugonjwa kati yako.
Kuna mambo
mawili tofauti kuna uponyaji na kunakuondoa magonjwa. Ikiwa una malalia unapewa
dawa ili kwamba zipambane na wale wadudu ndani yako sio kuondolewa ugonjwa. Ila
ukiamua kumtumikia Bwana Mungu wako Mungu anaondoa ugonjwa ndani yako. Mkwe
wake petro aliwahi kushikwa na homa na Yesu alipomwona na kumwombea akaondoa
ule ugonjwa. Kuna magonjwa mengine hayajapona kwako ni kwa sababu hujaamua
kumtumikia Bwana, leo hii amua kumtumikia Bwana kwa jina la Yesu Kristo.
Kuna mtu,
joka, mchawi anakuwekea magonjwa lakini ukimtumikia Bwana Mungu anakuja na
kuyaondoa magonjwa hayo wala hayatakuwepo kwako.
5. Hapata kuwa na mtu atakaye
haribu mimba.
Ukimtumkia
Mungu hapana kuharibu mimba kabisa, kuharibu mimba maana yake ni kuondokewa
uhai, maana yake kitu kilikuwa hakijakomaa mpaka mwisho kinafia njiani.
Inawezekana wewe ni mwanafunzi lakini kabla hujamaliza form four umepata
ujauzito na kufukuzwa shule maana yake umeharibu mimba ya shule, unaweza kuwa
unajambo zuri ambalo ulitakiwa ulizae lakini linaishia njiani. Umeenda kufuata
nyanya ili kwamba upeleke dar es salaam kuuza ili upate faida unafika kitonga
gari linapata ajari nyanya zile zinaharibika maan ayke umeharibu mimba ya
biashara.
Bwana anasema
kwamba ukimtumikia Bwana hutaharibu mimba, nyumba yako haitaishia njiani kwa
jina la Yesu Kristo. Ukimtumikia Bwana hutaanza jambo na kuishia njiani kwa
jina la Yesu Kristo
6. Hakuna utasa.
Ukimtumikia
Mungu hakuna utasa, utasa ni ile hali ya kutozaa. Tumejifunza kwamba mwaka huu
ni mwaka wa mavuno wachawi wanaweza kumzuia mtu asizae ili kwamba awe tasa,
unajaribu kuongeza mitaji lakini haiongezeki kwa namna yeyote ile. Unaweza
ukawa umechukua mtaji wako na kupanda shambani ili kwamba uvune mahindi mengi
umewekeza milioni nne ili kwamba upate milioni kumi unashangaa mara ghafla jua
limetoka huko na mvua imekataa mahindi yanakauka na baada ya kukauka mvua
inanyesha lakini ukimtumikia Bwana Mungu ansaema kwamba hapata kuwa na tasa kwenye
maisha yako.
7. Mungu atazitimiza siku zako.
Utimilifu wa
siku ni kwamba kila mwanadamu unayemwona ana siku zake za ukamilifu. Kuna siku
unatakiwa ufanikiwe hakuna kufa kabla ya wakati, hakuna kuanza jambo likaishia
njiani ukiamua kumtumikia Bwana.
8. Mungu atawafanya adui zako
wakukimbie.
Ukimtumikia
Bwana yeye atasababisha adui zako wakimbie mbele zako
9. Mungu ataweka utiisho mbele
yako
Ukimtumikia
Bwana unaweza ukakaa na mawaziri lakini wakakuogopa na kusema mzee njoo na
wakati huo wewe ni kijana kwa sababu ya kumtumikia Bwana. Kuna ndugu zako
wanasema kwamba huyu ameokoka ametuasi tumuitishe aje kwenye kikao ama aache
wokovu aingie kwenye ukoo au aendelee na wokovu tumtenge kwenye familia. Kama
unamtumikia Yesu kwa ukweli ukifika kwenye kikao hicho wanasema kwamba
tumekuita kwa sababu hatuja kuona siku nyingi tumekuita ili kwamba tukusalimie
shauri lao linapotelea hapo.
Ukimtumika
Bwana Mungu kuna utiisho anaweka mbele yako, bila utumishi wa Bwana ukitumikia
fedha au mizimu utaangamia kabisa, leo hii amua kumtumikia Bwana kwa jina la
Yesu Kristo.
0 Comments