HATUA ZA KUSHINDA VITA VYA KIROHO KWA MAOMBI
1. Mtambue kwanza adui yako.
Waefeso 6:12
”Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damuna nyama; bali ni juu ya falme
na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika
ulimwengu wa roho.”
MAADUI
TUNAOPAMBANA NAO NI HAWA.
-Falme za
giza.
-Mamlaka za
kishetani.
-Wakuu wa
giza
-Majeshi ya
pepo wabaya.
Yakobo 4:7
”Basi mtiini MUNGU. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.”
Adui yetu ni
shetani na ana nguvu lakini taarifa ni kwamba tukimpinga na kumharibu kwa jina
la YESU anaharibika.Katika vita yako ni muhimu kutambua uwezo wa adui yako.
3. Tambua mbinu za adui yako.
2 Kor 2:11
”Shetani asije akapata kutushinda; kwa maana hatukosi kuzijua fikira zake.”
-Mbinu za
shetani ziko wazi sana kama wewe ni muombaji.Kupitia maombi utanoa macho yako
ya rohoni ili yaone kila hila za adui dhidi yako hivyo utaomba kwa uhakika
maana utakuwa unajua unapambana na nani na yuko wapi.
4. Fahamu unapigana vita ya namna gani.
Siku zote ni
muhimu sana kila mtu kujua kwamba vita ya kiroho hupiganwa rohoni.Kwenye vita
hiyo ni lazima ujue kwamba ili ushinde vita unatakiwa uwe upande wa BWANA ndipo
utashinda. Ili uwe upande wa MUNGU kwanza ni lazima uokoke na kisha ni lazima
uongozwe na ROHO wa MUNGU. Ukishakubali kuongozwa na ROHO wa MUNGU basi hakika
utajua Neno hili kwamba ”….. BWANA
awaambia hivi, Msiogope, wala msifadhaike kwa ajili ya jeshi kubwa hili; kwani
vita si yenu bali ni ya MUNGU.2 Nyakati 20:15”
5. Pima silaha zako, je zinauwezo wa kukufanya
uanzishe vita?
Waefeso 6:13
”Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za MUNGU, mpatekuweza kushindana siku ya
uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.”
Silaha za
MUNGU ni;
-Damu ya
YESU.
-Jina la
YESU.
-Matoleo.
-Matendo
mema n.k
Vita ya
ushindi inaanza kwanza kwa wewe mpiganani kuwa mtoto wa MUNGU na kuongozwa na ROHO MTAKATIFU huku
ukizijua haki zako.
Warumi 8:14
”Kwa kuwa wote wanaoongozwa na ROHO wa MUNGU, hao ndio wana wa MUNGU.”
1 Yohana 5:5
”Mwenye kuushinda ulimwengu ni nani, isipokuwa ni yeye aaminiye ya kwamba YESU
ni Mwanawa MUNGU?”
”Ninyi,
watoto wadogo, mwatokana na MUNGU nanyi mmewashinda, kwasababu yeye aliye ndani
yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika dunia.-Yohana 4:4”
MUNGU
AKUBARIKI SANA
MAOMBI NA
MAOMBEZI
WASILIANA
NA MCHUNGAJI LAURENT MPOMA
0762756542,
0782859946,
WATSAP:
0762756542
0 Comments